sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
[h=2][/h] Ijumaa, Agosti 24, 2012 05:47 Na Arodia Peter, Dar es Salaam
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, amewaonya wanachama wa chama hicho, wanaoigeuza CCM sawa na mali yao.
Amesema kuwa, tabia ya wanachama hao haiwezi kuvumiliwa, kwa kuwa inakiangamiza chama na pia inakipaka matope chama.
Guninita aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akihutubia mkutano wa Baraza Kuu la Vijana, Mkoa wa Dar es Salaam. Mkutano huo ulifanyika katika ofisi za chama hicho, Wilaya ya Kinondoni.
Tangu kuanzishwa kwa CCM, chama hakijawahi kushuhudia ubaguzi wowote wa kidini wala ukabila, lakini kadri muda unavyokwenda, kuna dalili ya kuwepo mtandao wa watu wanaotaka kufanya chama kuwa kama mali ya ukoo kwa maslahi yao binafsi.
Kuna kamtandao kanaanza kujitokeza, baadhi ya watu wanataka kufanya chama hiki kiwe cha ukoo, hili haliwezi kukubalika, lazima vijana mlikatae kwa nguvu zote.
Viongozi wa Serikali ya CCM, akiwamo Rais Kikwete hatuoni familia zao zikijihusisha moja kwa moja kwenye siasa, lakini baadhi ya wanachama miongoni mwetu tunataka kuharibu utaratibu huo, baadhi yetu tunataka chama kiwe mali ya ukoo.
Tukifanya hivyo, tunawajengea hofu wasio na ndugu kwenye chama, unakuta viongozi wa ngazi mbalimbali wanatoka familia moja, matatizo hayo yapo, hatuwezi kuyafumbia macho, tunajenga mazingira ya vitisho, alisema Guninita na kushangiliwa.
Katika hatua nyingine, Guninita ambaye tayari ameshachukua fomu kutetea kiti chake, aliwataka vijana kuwa tayari kujibu hoja za vyama vya upinzani.
Nataka kuanzia sasa muanze kujibu hoja za upinzani, msiwaache watambe peke yao, mimi nitajibu zile za Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa Chadema), huyo ndiye saizi yangu, nitammudu, lakini si akina Mnyika (John Mnyika, Mbunge wa Ubungo).
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, amewaonya wanachama wa chama hicho, wanaoigeuza CCM sawa na mali yao.
Amesema kuwa, tabia ya wanachama hao haiwezi kuvumiliwa, kwa kuwa inakiangamiza chama na pia inakipaka matope chama.
Guninita aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akihutubia mkutano wa Baraza Kuu la Vijana, Mkoa wa Dar es Salaam. Mkutano huo ulifanyika katika ofisi za chama hicho, Wilaya ya Kinondoni.
Tangu kuanzishwa kwa CCM, chama hakijawahi kushuhudia ubaguzi wowote wa kidini wala ukabila, lakini kadri muda unavyokwenda, kuna dalili ya kuwepo mtandao wa watu wanaotaka kufanya chama kuwa kama mali ya ukoo kwa maslahi yao binafsi.
Kuna kamtandao kanaanza kujitokeza, baadhi ya watu wanataka kufanya chama hiki kiwe cha ukoo, hili haliwezi kukubalika, lazima vijana mlikatae kwa nguvu zote.
Viongozi wa Serikali ya CCM, akiwamo Rais Kikwete hatuoni familia zao zikijihusisha moja kwa moja kwenye siasa, lakini baadhi ya wanachama miongoni mwetu tunataka kuharibu utaratibu huo, baadhi yetu tunataka chama kiwe mali ya ukoo.
Tukifanya hivyo, tunawajengea hofu wasio na ndugu kwenye chama, unakuta viongozi wa ngazi mbalimbali wanatoka familia moja, matatizo hayo yapo, hatuwezi kuyafumbia macho, tunajenga mazingira ya vitisho, alisema Guninita na kushangiliwa.
Katika hatua nyingine, Guninita ambaye tayari ameshachukua fomu kutetea kiti chake, aliwataka vijana kuwa tayari kujibu hoja za vyama vya upinzani.
Nataka kuanzia sasa muanze kujibu hoja za upinzani, msiwaache watambe peke yao, mimi nitajibu zile za Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa Chadema), huyo ndiye saizi yangu, nitammudu, lakini si akina Mnyika (John Mnyika, Mbunge wa Ubungo).
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]