....don't mix -up the two sides of Warioba buddy!.......no doubt the guy is brilliant ktk issues za Kitaifa...........however, him being brilliant just like Chenges et al......does not exclude him from being insane (if proven) in some of his involvements........
Mkuu FMES, nadhani kuna mapungufu kudhani kuwa Warioba anatakiwa kuongea hasa kile anachoona kinahitaji kuongelewa. Pamoja na kuwa ni haki yake kusema lolote bila kuvunja sheria, pia ni hulka yake kutoa mawazo yake katika mambo mbalimbali. Na mengi ambayo amekuwa akiyaongelea yamekuwa hayalalamikiwi kama hili.
Imeelezwa katika taarifa aliyotoa kwenye vyombo hivyo vya habari alivyokutana navyo nia halisi ya kukutana nao. Kwa kifupi naweza kuelewa nia hizo kama zifuatazo;
1. Fununu zinazoendelea kutolewa na vyombo mbalimbali vya habari kumhusisha na Ufisadi kupitia Mwananchi Gold
2. Usumbufu anaopata kutokana na Ndugu na Jamaa zake kuwa na wasiwasi wa yanayosemwa na vyombo hivyo vya habari
3. Kuweka wazi ukweli kuhusu uanzishwaji na uendeshwaji wa Mwananchi Gold
4. Kuelezea kutopendezwa na vitisho visivyotekelezwa kuhusu kushitakiwa kufuatia kinachoitwa tuhuma za ufisadi kupitia Mwananchi Gold. Na kuonnyesha kuwa yuko tayari kwa kesi zinazosemwa zitamkabili.
Kwa mawazo yangu, lolote linaweza kutokea. Ila Mtu wa Hadhi ya Mh. Warioba, hawezi kukaa kimya kila siku akisikia mambo yakisemwasemwa bila hatua zozote kuchukuliwa. Kumbukeni Wakuu, kwamba uhusiano wake na Mwananchi Gold umeanza kuongelewa muda mrefu. Yeye kama mtu anaeshindwa kuvumilia kuona akisemwa hivyo, ameamua kuzungumza na amesema alichokuwa tayari kukisema. Si vyema kutaka azidishe maongezi zaidi.
FMES,
Mkuu wangu swala la kujitoa hadharani halina ubaya wowote kwani hata Mwinyi na Kikwete wamewahi kusema mali walizokuwa nazo bila hata kuulizwa wakati Ufisadi ukizungumziwa na hakuna mtu aliyepelekwa mahakamani..
Wenye jeuiri ya kutosema Ufisadi wao ni kina Yona, Mramba, Chenge ambao kweli wamechukua na hawawezi kuwa na ubavu wa kuzungumza na waandishi wa habari kwa sababu wanafahamu kila watalkalo sema litachukuliwa against them in the court of law - IF arrested...
Tuhuma zipo?... yes zipo kwani kama zisingekuwepo msingekuwa na maswali yote mliyouliza. Mkuu unakuwa kama hukai nchi za majuu ambako kila siku unaona watu wakifuta tuhuma ktk magazeti hata kabla ya kufikishwa mahakamani!... NI watu kama Mkapa, Yona, Chenge, Mramba na Governor Blagojevich wanaokimbia media wakisubiri wafikishwe mahakani..Huyo Chenge aliposema Vijisenti alikuwa mahakama gani?..Mwinyi aliposema against Ufisadi akisema yeye alipokuwa rais hakuchukua kitu zaidi ya mshahara na ruzuku alizopewa au Kikwete kudai yeye ana shamba tu kulikuwepo na chombo cha Upelelezi kilichowauliza?..Na mbona walizungumza na waandishin wa habari tu wala sio ktk sheria mnazotaka nyie zitumike kwa Warioba..
Mkuu wangu binafsi sioni kosa kabisa la Warioba kama Mwanasheria na Mwananchi Gold, haya madai ya Mtanzania hayana hata uzito isipokuwa ndio tuhuma zenyewe hizo...Mang'ula hawezi kujua kitu ndani ya CCM wala hata siku moja hawezi kusema Ukweli kwani hata issue zote za Richmond, EPA na kadhalika kasema Uongo mara mia kidogo..Hawa ni watu wanaozungumza tu kile walicho agizwa kusema..Huyu kaingia lini uongozi wa chama, si majuzi tu tena kwa kukamatiwa na watu..
Kutokana na statement zenu nitakuwa mjinga kumuamini Mang'ula against Warioba ambaye ni Mwanasheria, Mwenyekiti na mwenye share ndani ya Mwananchi Gold..Ati Mang'ula amekataa iwe jukumu la Warioba kujisafisha..does this make sense kweli jamani!..
Kisha nikirudi ktk swali la Masanja, Ajira za Tanzania ni kama hivyo na ndio sababu siku zote tunapiga makelele humu JF kuhusiana na Conflict of interest, hili Azimio lenu la Zanzibar limetuletea miujiza ya uongozi ktk Utandawazi na soko huria, lakini haina maana watu wote wanaoshika madaraka ni wezi.. Majuzi tu CCM mmemchagua Bi. Sophia Simba kuwa mwenyekiti wa UWT.. na Uanasheria wake umetumika kama kigezo cha juu ktk CV yake kushika wadhifa huo..na kasifiwa na kina Mwanakijiji hapa..
Huyu sasa hivi ni Mwanasheria, Mbunge, Waziri, Mwenyekiti wa UWT na mjumbe wa kamati kuu wa blaa! ablaa blaaa! bado hatufahamu yupo ktk board gani za mashirika ya serikali..Uongozi wote nchini ni watu wale wale wanarudiwa kila sehemu unayokwenda..WHY?.. waulize CCM!. wala sidhani ni hoja ya kumuuliza Warioba ikiwa nchi nzima inatumia mfumo wa ajabu ajabu kulindana. My be walifikiria Warioba ni mwenzao sasa kawatoka imekuwa yeye ndiye fisadi..
Mkuu wangu ni system nzima ya CCM ambayom bado imeukumbatia Ujamaa wakidai wameondokana nao.. Mwananchi kama shirika binafsi linalomilikiwa na serikali (Wananchi by 80% ulifikiria kwa nini wasiwe na wakili?... iweje atumike mwanasheria mkuu wakati serikali ina only 20 ya share 80 za wananchi!..wananchi ambao tunaambiwa toka mwaka 1995 to 2005 in 10 years walikwisha invest zaidi ya Usd 2.5/b ktk madini... I mean guys kama mnashindwa kulitazama hili mtaweza vipi kuangalia maswala mazito zaidi mkipewa madhifa!..
Warioba hakukurupuka kwenda kwa waziri wa sheria Chikawa wala hakuenda Polisi, au Takukuru kujieleza isipokuwa ametumia vyombo vya habari kama watu wote wenye kutuhumiwa wanavyofanya iwe nchi za Ulaya au Afrika..Na kama kuna mashtaka yoyote mpelekeni mahakamani.. Ubishi wa nini hapa kijiweni, who said what!..
Mbona huyo waziri Chikawe kayasema alosema hakusubiri aitwe na mahakama au vyombo vya Upelelezi..
Hizo documentary evidence ampe nani? Ndio maana amesema kama wana kesi wampeleke mahakamani, au mimi ndiyo mbumbumbu?utetezi wake ungeambatana na documentary evidence, na kuruhusu maswali yanayo pingana na utetezi wake
Hizo documentary evidence ampe nani? Ndio maana amesema kama wana kesi wampeleke mahakamani, au mimi ndiyo mbumbumbu?
Kwani alikataa kujibu maswali ya waandishi habari? Kwa kuwakaribisha kuongea nao aliwapa nafasi tosha ya kuuliza maswali. Put the blame where it belongs.katika uhandishi wa habari unatakiwa upate taarifa za pande zote, sasa mzee kasema magazeti etc wamemuandika kama atafikishwa mahakamani kwa madai kadha wa kadha, sasa yeye hili suala lime mkera hivyo nae akatoa taarifa kutokana na anavyo jua yeye, lakini inaonekana kama si kamilifu kutokana na kutotoa taarifa toshelezi kama barua ya uamuzi wa serikali, hakuongelea umiliki wake wa , hakuongelea mali wali zo nazo hiyo kampuni , hakuwakilisha mahesabu yalio kaguliwa kuonyesha yeye hakula hela etc, hivyo ameacha vitu vingi, pili angewapa nafasi ya kuuliza maswali ili nao wakiandika habari iwe inajitosheleza
August,
Ebu rudia kusoma maelezo yake.. Nyaraka alisema anazo kama watakuja na waje haraka alisisitiza!...Giiii hadi leo hii tunaingia week ya tatu..Yaleyale ya Masha na Mengi! - for I can see where FMES comes from..
Kwani alikataa kujibu maswali ya waandishi habari? Kwa kuwakaribisha kuongea nao aliwapa nafasi tosha ya kuuliza maswali. Put the blame where it belongs.
August,
Mkuu hata sikuelewi..
Lakini kama unasema hivi nitakavyokusudia kujibu then nimekuelewa..
Kwa mfano mtu akisema yeye ni baba yangu kwa sababu analala na mama yangu! well mtu wa kwanza mimi kumuuliza ni mama yangu... Huyo baba wala Mama hawana haja ya kunionyesha ushahidi, ushahidi gani nitakao utaka kutoka kwao...itakuwa sina adabu.
Na ikiwa madai yake ni kuwa yeye ni baba yangu kwa uzazi, bado jibu kamili nitalipata kwa mama..Anyway, sijui hasa uliposema hivi umelenga kitu gani.
Nikirudi kwa Warioba, kumbuka yeye ni mwanasheria, hakuna mtu yeyote duniani anaweza kuanika ushahidi wake kwa waandishi wa habari isipokuwa kule ushahidi huo unapohitajika..
na ikiwa wewe mkisiwa (suspect) ktk janga fulani uunaweza kusema unayo Alibi kuonyesha sio mhusika not necessarily uwaonyeshe ticket yako ya ndege kuonyesha hukuwepo nchini lakini unaweza sema sikuwepo nchini na ushahidi ninao..
Sasa kama mnataka maswala haya yafike mahakamani ya nini mnachelewa kunishtaki!..Mkuu ni yaleyale ya Masha kuweka vitisho vingi kwa Mengi ati kwa sababu kasema kuna kiongozi kijana ametishia maisha yake basi liwe kosa na kudai kwa nini hakwenda ktk vyombo vya sheria. Mkuu sote tunajua system ya Bongo inavyofanya kazi na kila siku ukijitokeza mapema huondoa kabisa njama zinazopangwa hivyo kukuacha huru na salama.
Ukilala watu watakushughulikia kikweli.. Warioba kafunika mkuu wangu hutasikia cha Said mwema, Hosea wala nani kwa sababu swala la Mwananchi ni zito kuliko Warioba..
1. Nne, je kilichoandikwa hapa chini kina ukweli gani? Kwanini pamoja na tuhuma hizi kutolewa mara nyingi, ilikuwaje hakuongelea wamiliki wote wa makampuni haya hapa chini?
Quote:
Kampuni ya Umoja inamilikiwa na familia ya Warioba, kampuni ya VMB inamilikiwa na familiaya Mahalu, kampuni ya YM inamilikiwa Yussuf Mushi, kampuni ya CCM Trust wenye hisa ni Warioba na Yussuf Mushi na si wadhamini wa CCM.
Tano, mabilioni yaliyopotea toka BOT yameenda wapi? Je Warioba amefaidika vipi na mabilioni hayo? Sita, CCM wamekanusha kuwa na share Mwananchi Gold na Mangula alishasema kwamba Warioba na kundi lake waliomba kutumia jina la CCM trust, kama anachosema Mangula na CCM sio sahihi, mzee Warioba amechukua hatua gani dhidi yao?
..nadhani katika huu mradi wa Mwananchi Gold Jaji Warioba amekuwa mzembe kidogo. Jaji Warioba alijisahau na matokeo yake watu wabaya wamemtumia.
FMES,
Mkuu na wewe mzee wa dataz kweli umeuvaa mkenge huu!.. duh ama kweli mapenzi ya CCM ni kama ushanga theory ya ndugu yangu Zakumi..
Ebu twende kwa kituo tusitake kutaja majina hapa ila tuangalie zengwe zima linavyobadilika kama Kinyoinga..
Kama alivyosema Jokakuu kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa Mwananchi Gold ni sehemu ya project za viongozi ambazo tumeona ktk miaka ya mwisho ya Utawala wa Mkapa..Tumeona mashirika kama Meremeta ambayo yamelitumia Jeshi letu kumiliki migodi na nina hakika kabisa kuwa Jeshi halina habari hizo isipokuwa viongozi hawa hawa wanatuambia kwamba Meremeta ni shirika la serikali..Up to now hakuna kati yetu anayefahamu lolote kuhusiana na Meremeta na jinsi gani serikali inahusika..CCM inafanya biashara tena kubwa lakini mnatuficha wananchi..Hilo Azimio la Zanzibar limekuwa donda ndugu la mwananchi..
Kuanzishwa kwa Mwananchi Gold ilikuwa officially commissioned na Mkapa, I repeat MKAPA! hivyo huwezi kunambia CCM hawafamu kitu, na nimeiweka habari nzima ya ufunguzi wake na tumemwona bangusdilo Msabah akitoa taarifa ambazo zinaiweka serikali mbele ya kila kitu kwa kuvihusisha vyombo muhimu sana kwa nchi yetu BoT na NDC..Warioba hana ubavu huo hata kidogo..
Kumbukeni tu wakati huo Governor wa BoT alikuwa Ballali na hata kuwepo kwa Mayalla ni mwakilishi wa BoT ambao wana share zile 20% za serikali..
Wapi Warioba katumiwa bado sijafahamu lakini nina hakika katumiwa ktk mpango wa kuifilisi nchi na hakika ningekuwa na wasiwasi zaidi kama angekaa kimya kama kina Mkapa.. Mkuu wangu wote hao uliwataja toka Mkapa hadi kina Mramba hawawezi kujitokeza ktk magazeti watasema nini?.. Mkapa hadi kesho anakimbia waandiushi wa habari.... Why? ina maana ndiye mkweli zaidi ya Warioba inapofikia swala la Ufisadi!..Nambioe Fisadi hata mmoja aliyewahi kuja wazi kwa waandishi wa habari kaa sio kina RO kutishia watu wanaomfuata fuata..
Yes nina hakika kabisa hapa kuna mchezo kwanza BoT kama chombo cha Taifa as central bank haitakiwi kabisa kujiingiza katika biashara kama hizi..
Pili, nimeshtuka zaidi pale share zinapobadilika ghafla ya kuwa kama alivyozungumza Warioba as a fact Warioba kaja juu kutokana na serikali kujaribu kuiondoa BoT baada ya maji ya shingo kuwafikia baadhi ya wahusika..Warioba kama mwanasheria na mkisiwa mkubwa he has all the right kuwakilisha shirika na kusafisha jina lake wakati akitaja wahusika wenyewe..
Mkuu najua kabiusa jinsi Tanzania inavyofanya kazi.. nawafahamu WATU na MAZINGIRA ya bongo vizuri sana kiasi kwamba huwei kutumia jina la CCM trust fund bila CCM wenyewe kuwepo ndani, kisha Warioba alikwisha poteza nguvu ya kiutawala. Then again Mkapa hawezi kwenda kufungua shirika la watu binafsi kwa baraka za serikali akitumia mfuko wa serikali na maelezo yote yanayohusiana na hisa...Something was going on!..
Kwa hiyo leo hii unaponambia ati mang'ula amekana kuhusika kwa CCM wakati habari hizi za kuhusika kwa CCM< zimetoka kabla hata JK hajakamata madaraka iweje wamwachie Warioba kwa muda wa miaka mitatu akiendelea kutumia jina la chama..come on guys think acheni unazi wa chama hapa..
Mimi nadhani Kikwete amekuja juu na anataka kuona chama hakitumiwi na baadhi ya watu hata kama madhumuni ya chombo hicho yalikuwa na nia njema.. Huu ndio mchezo wa Mkapa from day one, huja na strategy baabu kubwa kiuchumi lakini kumbe hutufungia kanyaboya..tukifika nyumbani kufungua mzigo ni makaratasi matupu..
Hivyo tusiwe na mukhu, Warioba kazunguma aliyowqeza kusema kama kuna kesi tunaomba haraka ifikishwe mahakamani iwe kumshtaki Warioba au kumwita kama shahidi mbele ya Special Commissioned MPs..Ni swala ambalo mimi binafsi siwezi kumhukumu Warioba kwa sababu namfahamu mzee huyu. Amefanya kazi na marehemu ndugu yangu Mh. Mundeba kwa miaka mingi..He is the honest leader U can possibly get! na naamini kabisa kuwa hili ni kanyaboya alichofanya Warioba ni kuubeba mzigo bila kujua alichofungiwa. Does he own share!.. that's not a question hata mimi ningenunua ktk shirika ambalo lina matumaini makubwa ya kufanikiwa..lakini kutokana na maelezo ya Warioba kuwa CCM ndio wenye share kubwa na CCM wenyewe wamekaa kimya wakizungumzia pembeni hao kina Mang'ula ambao wako radhi kuua mbwa aliyevkwa jezi ya CCM, leo washindwe kumwajibisha Warioba kwa kutumia jina la chama..
Can't buy that... Try again!