Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
Mjomba aliitikia shikamoo yangu huku akinitumbulia macho. Nilihisi kuna zaidi ya tatizo, haikuwa kawaida yake kuniangalia kwa macho ya vile.
Nilijiuliza kama nina kosa nitakimbilia wapi maana ndani ya nyumba tulikuwa tukiishi wawili tu. Mimi na mjomba Msafiri. Yeye alitengana na mke wake mama Muna miaka minne iliyopita.
Wakati wanatengana mimi nilikuwa bado nyumbani, Ngamiani Tanga nasoma Shule ya Msingi Usagara. Baada ya kumaliza
darasa la saba, nilikosa nafasi ya kuendelea na masomo ndiyo akanichukua mjomba, kaka yake mama yangu.
Mjomba Msafiri alinichukua mwaka mmoja mbele baada tu ya kutengana na mama Muna. Mama yangu yaani dada yake
mjomba ndiye aliyemuomba kunichukua kuja kusoma hapa Dar.
Alinitafutia sekondari binafsi ipo maeneo ya Ubungo Kibangu. Sasa hivi nipo kidato cha tatu.
Maisha yetu nyumbani na mjomba yalikuwa mazuri sana, nyumba nzuri, ina geti, mjomba ana gari, msichana wa kazi na mlinzi. Mjomba anafanya kazi kampuni ya wazungu.
"Shani," mjomba aliniita kwa sauti iliyojaa utulivu wa hali ya juu baada ya kumaliza kuniangalia kwa kunitumbulia macho.
"Unajua wajibu wako uliokuleta Dar es Salaam?"
"Najua mjomba," nilimjibu huku nikichekacheka.
"Ni nini?" aliniuliza akiwa amekunja uso kuashiria kwamba hanitanii.
"Kusoma."
"Unasoma?"
"Nasoma mjomba."
Haya Tena Baada ya kumaliza Sherehe za sikukuu ya Eid El Fitri ninawaleteeni Kitu kipya hicho hadithi ya kusisimuwa mukiipenda mubonyeze neno hili (Like) hapo chini nitajuwa munaipenda na nitaiendeleza musipo bonyeza neno (Like) sitoweza kuendelea kazi kwenu wapenzi wangu.........
Nilijiuliza kama nina kosa nitakimbilia wapi maana ndani ya nyumba tulikuwa tukiishi wawili tu. Mimi na mjomba Msafiri. Yeye alitengana na mke wake mama Muna miaka minne iliyopita.
Wakati wanatengana mimi nilikuwa bado nyumbani, Ngamiani Tanga nasoma Shule ya Msingi Usagara. Baada ya kumaliza
darasa la saba, nilikosa nafasi ya kuendelea na masomo ndiyo akanichukua mjomba, kaka yake mama yangu.
Mjomba Msafiri alinichukua mwaka mmoja mbele baada tu ya kutengana na mama Muna. Mama yangu yaani dada yake
mjomba ndiye aliyemuomba kunichukua kuja kusoma hapa Dar.
Alinitafutia sekondari binafsi ipo maeneo ya Ubungo Kibangu. Sasa hivi nipo kidato cha tatu.
Maisha yetu nyumbani na mjomba yalikuwa mazuri sana, nyumba nzuri, ina geti, mjomba ana gari, msichana wa kazi na mlinzi. Mjomba anafanya kazi kampuni ya wazungu.
"Shani," mjomba aliniita kwa sauti iliyojaa utulivu wa hali ya juu baada ya kumaliza kuniangalia kwa kunitumbulia macho.
"Unajua wajibu wako uliokuleta Dar es Salaam?"
"Najua mjomba," nilimjibu huku nikichekacheka.
"Ni nini?" aliniuliza akiwa amekunja uso kuashiria kwamba hanitanii.
"Kusoma."
"Unasoma?"
"Nasoma mjomba."
Haya Tena Baada ya kumaliza Sherehe za sikukuu ya Eid El Fitri ninawaleteeni Kitu kipya hicho hadithi ya kusisimuwa mukiipenda mubonyeze neno hili (Like) hapo chini nitajuwa munaipenda na nitaiendeleza musipo bonyeza neno (Like) sitoweza kuendelea kazi kwenu wapenzi wangu.........