Gobless Lema umetukosea sana, lakini tutakusamehe

Gobless Lema umetukosea sana, lakini tutakusamehe

Countrywide

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2015
Posts
21,193
Reaction score
33,580
Habari wanajf, leo kuna jambo ambalo nimeona lina ukakasi sana kuhusu Lema.

Lema ameondoka nchini kwa sababu vitisho anavyopewa kwa mujibu wake mwenyewe.

Inaweza kuwa kweli au la, lakini ambacho nimeshindwa kukielewa ni kuwa lema ameondoka na familia yake (mke na watoto wake tu) na hatujui lini atarudi maana wanaomtisha wanaweza kuendelea kumtisha kwa muda mrefu.

Hapa nimebaki na maswali mengi sana, pale nyumbani kwa lema kuna ndugu pia, kuna mtoto wa mawazo( yeye mwenyewe ndio alisema anamlea mtoto huyu nyumbabi kwake).

Leo imetokea hatari/vitisho kwake, kakimbia na mke na watoto wake tu, je hawa wengine nao wakimbilie wapi?

Na mara ulipokuwa kenya ukasema Tanzania hakuna uhuru wala haki na kuna ukiukwaji wa haki za binadamu.

Tuseme sawa, ila sisi ndugu zako wa damu kwa kabisa(mashangazi, wajomba, baba wadogo, wakubwa na watoto wa dada, kaka) wao wana haki ya kukandamizwa ila watoto wako hawana hiyo haki?

Kama kukimbia manyanyaso hapa Tanzania na ukiukwaji wa haki za binadamu basi ungeondoka na sisi pia ndugu zako wa karibu, au sisi sio binadamu? Sisi tuna haki ya kukandamizwa?

Wale uliowaacha pale nyumbani kwako arusha sio binadamu wale? Au wale hawakandamizwi?

Pia nimeshangaa sana, siku ya october 30, ulipost jambo la kishujaa sana kwa kusema "nipo tayari kwa lolote, sitaogopa vitisho vyovyote" , " tunatakiwa kumuogopa Mungu tu na sio binadamu"

Iweje leo usema unaogopa vitisho na waksti ulishasema hivyo sio lolote kwako, hakuna wa kukutisha ukaogopa? Leo hii unaogopa binadamu kuliko Mungu?
Au haya umesahau kama uliyasema?

Yote kwa yote, nina amini kuna kitu umejifunza na tumeshakusamehe sisi ndugu zako.

IMG_20201122_134102.jpg
IMG_20201122_134046.jpg
 
Comrade umeghafilika bila sababu hadi umeonyesha kama una hasira na Lema kwa sababu umemkosa-kosa.
 
Hayo majibu sasa mhh mtoa mada kashushie na pepsi baridi
 
Acha ufala wewe mbung'o. Atishwe yeye halafu aondoke na wewe shangazi yake? Una akili timamu kweli? Kwani na wewe umetishwa? Maccm mna laana sana nyie. Kama unaona amekuzidi kukimbilia kaskazini, wewe zama kusini, mjinga mkubwa wewe.
 
Yangemkuta akiwa nyumbani mngemsema Kiburi kwa kunukuu kauli zake za kishujaa. Sasa ameondoka imekuwa nongwa.
Even braves die once. Tujifu ze kubeshimiana.
 
CCM anamhurumia Lema wa Chadema. Acheni utani jamani. Mimi kila CCM akifa au kukatwa mguu nafungua bia nyingine
Wapi umesoma CCM anamhurumia Lema wa chadema? CCM siyo mtu, aliyeandika hii habari anajiita countrywide.
SEMA countrywide wa CCM anamhurumia Lema wa chadema anayemuogopa binadamu kuliko Mungu ndo maana kamkimbia mrisho gambo.
 
Ni kichaa tu ndio atakae muelewa lema, atishiwe wakati ameshindwa ila ilivyo kuwa anashinda hatishiwi, nimeamini inakubidi uwe msukule ili uweze kuielewa saccos
 
Wapi umesoma CCM anamhurumia Lema wa chadema? CCM siyo mtu, aliyeandika hii habari anajiita countrywide.
SEMA countrywide wa CCM anamhurumia Lema wa chadema anayemuogopa binadamu kuliko Mungu ndo maana kamkimbia mrisho gambo.
Na wewe unaumia Lema kukimbia🤣🤣🤣🙏
 
Back
Top Bottom