Wewe hukujua? Sii uliahidiwa maisha bora kwa kila mtanzania ukakubali? Tena tunalalama huku tukiacha kazi kwenda kusikiliza mbwembe za kufunguliwa viwanda na kujengewa barabara za angani. Utajenga kiwanda bila umeme? Yaani tunaahidiwa tu huku escrow ikiokota hadi dawa, mashule, mahospitali, tembo wetu, kuuwa kilimo, nk. Tutaamka lini? Tunapanguswa machozi na chepeo, kanga, na tisheti za njano. Wale werevu zaidi wanaongezewa na chumvi juu ya kwenda kukoleza umaskini walio nao. Wasijue ni kodi yako wanadhihakiwa nazo badala ya maendeleo.