Gharama ya Wivu wa Mapenzi hii hapa

Gharama ya Wivu wa Mapenzi hii hapa

PMNBuko

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2010
Posts
967
Reaction score
155
Katika hali isiyo ya kawaida mwanamke mmoja (Mhasibu) amejikuta akilazimishwa na mume wake kuacha kazi kwa kisa cha wivu mkubwa wa mwanaume anayehofia kuwa mkewe anaweza kutongozwa na wanaume. Je, hii ni halali? Wanaharakati wa haki za binadamu na wanawake mnasemaje?
 
wala hii haihitaji harakati za haki za binadamu, huyo mwanamke kiazi. Anatakiwa afanya harakati za haki ya mhasibu.
 
huyo mke kama kaacha kazi, nitamshangaa sana........... ulisomeshwa na huyo mume? ya mbele huyajui, huyo mume kesho aki-dead?
huyo kaka anafikiri nyumbani hakuna wanaume wa kuweza kumtongoza huyo mkewe, watongozaji wapo ofisini tu?
 
Naye akaacha kweli?😱 Bora wazazi wake wasingemsomesha, bora asingesoma.
na huyo kaka angetaka kuoa mama wa nyumbani si angeenda kutafuta wale waliomaliza shule za Kata? wamejaa kibao hawana pa kwenda, tunawafanya maHG
 
Kama Mumewe anakipato kizuri na anaweza kumfungulia biashara sioni tatizo lakini wivu halafu mivuko inatumandu,atokomee zake.
 
na huyo kaka angetaka kuoa mama wa nyumbani si angeenda kutafuta wale waliomaliza shule za Kata? wamejaa kibao hawana pa kwenda, tunawafanya maHG

Chaguo lake lilikuwa mwanamke msomi, muhasibu na mwenye experirnce ya miaka........ndo huyo sasa not from Kata Sec bana Fixed Point.............fixed mmmh...ndo mana Rigid eenh
 
hiyo biashara itakayomkutanisha na wanawake tu ni ipi?

Wateja, saplayaz, mikopo?

Kama Mumewe anakipato kizuri na anaweza kumfungulia biashara sioni tatizo lakini wivu halafu mivuko inatumandu,atokomee zake.
 
Jamaa ana wivu gani huo??..ila wahasibu wazuri hao..ukimkuta mwanadada wa benk au popote pale,lazima atongozwe..Pesa inatema,na ukute anakua kujiremba,lazima utupe nyavu.kama kaoa,aache ujinga.Amwamini mkewe.
 
na huyo kaka angetaka kuoa mama wa nyumbani si angeenda kutafuta wale waliomaliza shule za Kata? wamejaa kibao hawana pa kwenda, tunawafanya maHG

Hapo sasa. . .
Kidogo kidogo ataona hata kuwa mama wa nyumbani haitoshi, itabidi aache kwenda sokoni, then dukani na mwisho asotoke kabisa bila mume maana hata akikaa barazani tu anaweza akatamaniwa na kutongozwa.
 
Chaguo lake lilikuwa mwanamke msomi, muhasibu na mwenye experirnce ya miaka........ndo huyo sasa not from Kata Sec bana Fixed Point.............fixed mmmh...ndo mana Rigid eenh
huo usomi na experience ya uhasibu alitaka kwa ajili ya kuhesabia hela za kununulia nyanya sokoni? maana ukiwa mama wa nyumbani cha zaidi hela utakazokuwa unahesabu mara kwa mara ni zile za kununulia matembele
 
Watu wengine bana, sasa huyo mwanaume alitongozaje huyo mke kama anahisi kutongoza ni kosa la kuachishwa kazi?
 
unongea kwa kusikia ama kwa kuona?

Ukitaka kujua, jichanganye na wafanyabishara wa kike ndo utajua kama bank ndo sio waaminifu sana.

Hakuna lakini sio sawa na Bank kama anaona hapo kuna watu wenye pesa zao anaonananao kila siku.
 
Katika hali isiyo ya kawaida mwanamke mmoja (Mhasibu) amejikuta akilazimishwa na mume wake kuacha kazi kwa kisa cha wivu mkubwa wa mwanaume anayehofia kuwa mkewe anaweza kutongozwa na wanaume. Je, hii ni halali? Wanaharakati wa haki za binadamu na wanawake mnasemaje?

Kwa hili mwanaharakati mkubwa ni mwanamke mwenyewe! Kwani iwapo anatimiziwa kila kitu ana haja kweli ya kufanya kazi ya kuajiriwa?
 
Hivi karne hii bado kuna wanawake wajinga kiasi hicho??siamini!
 
Looh, jamani shule ilivokuwa ngumu na mikikimikiki kibao mara supplementary, mara umenusurika ku disco..Leo hii uniambie niache kazi ntakuelewa? Huyo mwanaume ana wivu wa kijinga..
 
Back
Top Bottom