Askari Kanzu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 4,598
- 1,233
Nonda, tukianza namna hii mwishoe tutapindisha mada. Kwa kifupi simuoni kiongozi yeyote "mwanamapinduzi" kwa viongozi wa kiafrika waliopo hivi sasa madarakani.Mkuu Katika orodha ya African revolutionaries uliyonayo ni nani na nani yumo humo?
Ok, hushabikii...unapendelea tu aondoke au aondoshwe! by who? Sifikirii kuwa unajali hili..bora apotezwe tu!
Na kama ni kweli, nyie "wanamapinduzi" mnaomsapoti Gaddafi si muende tu huko Libya na kuendeleza mapambano. Haisaidii kuendeleza malumbano hapa JF wakati Gaddafi maji yanaendelea kumzidi shingo. Gaddafi alianza kucheza na hao wa-"west" na sasa hao hao ndio wanaomchezea. Hilo ni funzo kubwa kwa viongozi wa bara la Africa katika karne hii ya ishirini na moja!!!!
Kwa upande wangu naona ni afadhali kujadiliana kuhusu tunajifunza nini kwa yaliyomtokea dikteta Gaddafi kwa mustakabali wa bara la Africa, badala ya kuendelea kusisitiza kwamba dikteta Gaddafi ni malaika wakati jamaa ni shetani flani nambari wani. Inaonekana kuna watu wana uoga wa kumkritisaizi Gaddafi ati tu kwa sababu wataonekana wanaunga mkono NATO/NTC. Hilo ni kosa lisilo na mshamaha (nionavyo mimi)!
Nawasilisha!