Geita: Kangi Lugola, awasimamisha kazi Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD), Mkuu wa Kituo cha Polisi(OCS)

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amewasimamisha kazi Mkuu wa Polisi Wilaya ya Geita (OCD),Mkuu wa Kituo cha Polisi Geita(OCS) na Mkuu wa Upelelezi Wilaya hiyo (OC CID),kwa kosa la Mahabusu kutoroka Mahakamani. Na pia ameelekeza Askari 8 wa kituo hicho wawekwe Selo.

Hivi karibuni Mahabusu 17 waliofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Geita wakikabiliwa na mashtaka mbalimbali walitoroka.

Mahabusu hao walikuwa wamewekwa katika ukumbi wa jengo jipya la mahakama wakisubiri kusomewa kesi zinazowakabili wametoroka Jumanne Mei 21, 2019.

Taarifa zinaeleza kuwa walitumia moja ya milango iliyokuwa katika jengo jipya la mahakama na kutoroka wakati askari wakiwa nje ya lango kuu la kuingia katika ukumbi huo.

Mkuu wa Magereza Mkoa wa Geita, Kamishina Msaidizi wa Magereza (ACP), Robert Rumanyika akizungumzia tukio hilo alisema jeshi hilo halijaanza utaratibu wa kuwapeleka mahabusu mahakamani kama ilivyo kwa mikoa mingine na kwamba kwa sasa mahabusu wanaopelekwa mahakamani wanakuwa chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi.

Alipoulizwa kuhusu jambo hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo alisema ni kweli wametoroka ila hakuweza kuzungumzia tukio hilo kwa undani kwa maelezo kuwa yupo katika ziara ya ufunguzi wa masoko ya dhahabu wilayani Geita.

zaidi, soma;


1106569
 
Nawapongeza sana masela waliosepa mahabusu kusikie tu.
Siku wakija kuvunja na kuiba nyumbani kwako uwapongeze kama unavyowapongeza leo, wakija kuiba kwa kutumia silaha na kufanya mauaji kwenye familia yako au ndugu zako uje utoe pongezi tena.

Siku mwanao au mkeo au mama yako mzazi au dada yako akibakwa na kulawitiwa urudi hapa kuwapongeza wahalifu hao, na siku wakipiga mapanga uwapongeze tusije kuona unarudi kulaumu hapa.

Mhalifu sio mtu mzuri kwasababu hana huruma kwa yeyote hata mzazi wake anaweza kumtendea uhalifu, usifurahie wahalifu kutoroka kwasababu kuna wengine wanakwenda kulipa kisasi au kukamilisha mipango yao
 
Namuona Afande alivyojikunyata mbele ya "boss" kuna wakati huwa najiuliza "kuajiliwa" maana yake ni nini? Bora mtu ukachukue ndoano zako na chambo ukavue samaki ukipata poa ukikosa poa tu!
Huyo sio afande ni RC Geita, Robert Gabriel
 
Siku wakija kuvunja na kuiba nyumbani kwako uwapongeze kama unavyowapongeza leo, wakija kuiba kwa kutumia silaha na kufanya mauaji kwenye familia yako au ndugu zako uje utoe pongezi tena.

Siku mwanao au mkeo au mama yako mzazi au dada yako akibakwa na kulawitiwa urudi hapa kuwapongeza wahalifu hao, na siku wakipiga mapanga uwapongeze tusije kuona unarudi kulaumu hapa.

Mhalifu sio mtu mzuri kwasababu hana huruma kwa yeyote hata mzazi wake anaweza kumtendea uhalifu, usifurahie wahalifu kutoroka kwasababu kuna wengine wanakwenda kulipa kisasi au kukamilisha mipango yao
Ntaendelea kuwapongeza masela na kuwaponda hao polisi wazembewazembe waliotorokwa kiboyaboya ni kulitia aibu jeshi letu tukufu.Hongereni sana masela mtenda haki ni mungu tu.
 
Hawa walala nje(polisi) Wana maisha magumu Sana mara nyingi wanakuwa confused na kazi zao....
Kuna muda nawaonea huruma Sana na muda naona poa Tu Acha wapate shidaa tu
kuwa polisi hakuna maana ya kulala nje, unaweza ukawa mfanyakazi wa Tanesco, TRA, Ewura n.kna ukalala nje.

Jeshi la polisi linasimamia usalama wa Raia na mali zake hiyo kazi huwa ni ya magereza wangepaswa kuwajibishwa kwa kuchelewa kwa kiasi kikubwa kuanza kupeleka mahabusu mahakamani.
 
dili hilo...hela imekuwa ngumi sana aisee!!
.....ila aisee kama umesepa wakakunasa utapigwa mpaka ufanane sura na mbunge wa zamani wa bunda. sijui anaitwaga nani yuleeeee. Pia nashauli polisi wote waliokua zamu siku iyo wapelekwe jeshini wakapigwe mpaka wachakae watasema ukweli walipewa ngapi
 
. ...polisi sio watu kabisa ukiwa na kesi watakugeuza mpesa tena kwa biti Kali ata akitaka kwenda kuhonga lazima akubebeshe wewe...bora wafukuzwe kazi waje kitaa machinga tuongezeke mzee baba aendelee kuuza vitambulisho vyake.
Hujawahi kukaa mahabusu, huwa unaishia vituo vya polisi tu ndio maana unaropoka.

Siku ukikaa mahabusu ndio utaelewa somo
 
.....ila aisee kama umesepa wakakunasa utapigwa mpaka ufanane sura na mbunge wa zamani wa bunda. sijui anaitwaga nani yuleeeee. Pia nashauli polisi wote waliokua zamu siku iyo wapelekwe jeshini wakapigwe mpaka wachakae watasema ukweli walipewa ngapi
Wasira hahaaa.
 
Waziri Kangi Lugola amewasimamisha kazi mkuu wa Polisi, mkuu wa kituo cha Polisi na mkuu wa upelelezi wa Wilaya ya Geita kutokana na mahabusu kutoroka mahakamani. Pia ameelekeza askari 8 wa kituo hicho wawekwa mahabusu.
IMG_20190524_174314.jpeg
 
Alivyokuwa mbunge alitetea maslahi ya polisi lakini sikuiz ni kuwapelekesha tuu polisi anapewa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo auze kweli?ndiyo kazi yao?
 
Back
Top Bottom