PreGE2025 Geita: Erick Shigongo atoa msaada wa vifaa vya michezo

PreGE2025 Geita: Erick Shigongo atoa msaada wa vifaa vya michezo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, ametoa msaada wa vitendea kazi vya michezo kwa wanamichezo wa Jimbo la Buchosa. Hafla hiyo ilifanyika katika kata ya Bupandwa, ambapo Shigongo alikabidhi mipira kwa ajili ya wanamichezo wa kata hiyo.

Shigongo alikuwapo kupitia diwani wa kata ya Bupandwa, Masumbuko Bupamba, na alisisitiza umuhimu wa wanamichezo kuendeleza vipaji vyao. Aliahidi kuwa atakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanamichezo hao wanapata fursa ya kufikia malengo yao.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwataka wanamichezo hao kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya katika kutumikia wananchi wa Tanzania.

Soma Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

 
Aisee!! mwaka wa uchaguzi ndo anatoa vifaa vya michezo miaka mingine holaaa🙄
 
Back
Top Bottom