Nimependa makala ya "Chama kichafu, hakitoi rais msafi" Mengi yameanikwa na kuwekwa wazi kwamba Magufuli hawezi kamwe kuwa rais bora kwa sababu ni tunda la mfumo maalumu ndani ya chama unaoandaa viongozi.
Pamoja na ukweli kwamba kuteuliwa kwake kunaonekana ni kwa bahati mbaya kwa sababu ya siasa za makundi ndani ya chama cha CCM, bado yeye anabaki kuwa tunda la mfumo huo. Hawezi kusimama hadharani kudai anao ubavu wa kuleta mapinduzi na mageuzi ndani ya chama hicho. Hii ni kwa sababu viongozi wa CCM wanasema CCM ina wenyewe. Magufuli SI miongoni mwa wenyewe hao.
Wana CCM wanaotaka kukibadilisha chama huishia na kukutana na wakati mgumu na kuamua kukaa kimya au kujiunga na waliomo katika kudumisha mfumo usioleta mabadiliko katika chama.
Kuna wakati, katika vikao vya ndani ya chama, joto la kutaka mageuzi ndani ya chama lilipopanda kwa kasi, Benjamin Mkapa aliwaonya wanaharakati ndani ya CCM kuwa wasidiriki 'KUFUNUA UCHI WA MAMA YAO' vinginevyo wangelaanika!
Hiyo ndo CCM na mambo yake........ wanatutawala wakijua hatuwataki.....