Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,445
- 7,816
Gavana wa Narok, Samuel ole Tunai amesema anaheshimu kauli ya mahakama ya juu ya kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa urais na kutoa wito kwa wakazi wa sehemu hiyo kumpigia kura rais Uhuru Kenyatta kwenye marudio ya uchaguzi huo. Tunai aliwahimiza viongozi katika kaunti hiyo ya Narok kushirikiana katika kuhakikisha rais Kenyatta anaibuka mshindi kwenye uchaguzi huo mpya wa urais. Mbunge wa Narok Kusini, Korei ole Lemein pia alitoa wito kwa wakazi wa sehemu hiyo kumuunga mkono rais Uhuru Kenyatta. Mbunge wa Narok Mashariki, Ken Aramat Kiloku aliwahimiza wakazi wa eneo hilo kujitokeza kwa wingi kumchagua tena rais Uhuru Kenyatta.