gari!

gari!

Zamaulid

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2009
Posts
19,955
Reaction score
16,006
[video]http://www4.autotrader.co.uk/classified/advert/201303125723837/sort/default/usedcars/engine-size-cars/1-7l_to_1-9l/quantity-of-doors/5/maximum-age/up_to_7_years_old/model/grand_vitara/make/suzuki/onesearchad/used/onesearchad/nearlynew/onesearchad/new/radius/1500/page/1/postcode/rm109xe?logcode=p[/video]
 
wakuu kwa wajuzi wa magari nataka kuvuta haka kamkoko toka uingereza, kanasifa hizi:
[h=3]bei paund 4990
2007 (56 reg), 4x4[/h]


  • 99,000 miles
  • Manual
  • 1.9L
  • Diesel

je niandae shilingi ngapi hadi kukaweka barabarani?

nini tofauti ya kununua gari uingereza na zile za japan?

natanguliza shukrani!



 
Utaingia cha kike mkuu,gari nyingi za uingereza hazina spare bongo inaweza ikawa the same brand na ya japan but kuna baadhi ya vifaa haviingiliani
 
Bwana zamaulid kwanza nadhani device yangu ina tatizo maana najaribu kuifungua hiyo link lakini mpaka sasa haijafunguka hivyo bado sijajua aina hiyo ya gari....pili utofauti kati ya uingereza na japan ni kwamba kuna baadhi ya magari kama toyota land cruiser wawezakupata bei ndogo uk kuliko ata japan...wauzaji wengi wa magari ya japan wanatumia njia zilezile za uk na dubai..uwa kuna mnada kila siku saa kumi na moja wao wanakwenda huo wananunua magari na wanafanya ufundi kama yalikuwa na kasoro yanatengenezwa na kuyatangaza katika internet,hakuna tofauti yoyote sema east afrika tumezoea kuagiza magari japan/dubai ni mazoea tu..lakini wawezapata gari safi sana na kwa bei nzuri uk...kisha kama ujuavyo uk ni strictly sana hivyo gari za magumashi ni vigumu kupata utapata gari nzuri sio zile auto zinageuzwa manual..right hand zinageuzwa left nk..so nunua tu hakuna tatizo....ila sasa suala lipo hapo kwenye ushuru...nchi yetu bado ushuru haueleweki vizuri hiyo gari ya 2007 ni model mpya kabisa sasa tra wanawezaku uplift sana CIF ikawa juu kama ujuavyo hizo gari manual zipo juu sokoni lakini nachokushauri chukua chasis namba ya hiyo gari mpe agent yeyote mzuri atakupa makisio mazuri sana na ushuru...
 
Grand Vitara imetulia haswa, ukiangalia kwa ebay unaweza pata<rahisi zaidi ya hapo
 
Jamani hiyo ni 2007 na ni manual..sasa ukitaka bei ya chini yawezekana kabisa hisiwe original manual hiyo bei kwa hilo gari ni sawa kabisa...nilibahatika kufanya kazi kwenye showroom ya al aweer dubai(hii ndio showroom kubwa kuliko zote duniani ya magari ya right hand)husikimbilie cheap... watu kibao wanaagiza gari uk..kama navyokwambia hiyo ni original manual chukua
 
Utaingia cha kike mkuu,gari nyingi za uingereza hazina spare bongo inaweza ikawa the same brand na ya japan but kuna baadhi ya vifaa haviingiliani

Hii si kweli kabisa na sijaona. Nimeshatuma magari mengi sana ya kijapani toka UK na hakuna tatizo kama hili..mkuu. Magari ya UK ni poa sana, imara na Mileage zake mara nyingi ni za ukweli. Na UK kama limesema ni 2007 ni kweli hakuna uchakachuaji. Chukua mchuma huo hutajilaumu. Kwa kuongezea hizi Suzuki zinatengenezwa Japana na kusafirishwa UK.
 
Hii si kweli kabisa na sijaona. Nimeshatuma magari mengi sana ya kijapani toka UK na hakuna tatizo kama hili..mkuu. Magari ya UK ni poa sana, imara na Mileage zake mara nyingi ni za ukweli. Na UK kama limesema ni 2007 ni kweli hakuna uchakachuaji. Chukua mchuma huo
hutajilaumu. Kwa kuongezea hizi Suzuki
zinatengenezwa Japana na kusafirishwa UK.[/QUOTEh]hiyo ni kweli kabisa soko la japan limeingiliwa na wahuni ambao wanachakachua sana magari..baadaye wanatangaza $2500 sisi tuona tumepata..ni wachache hawachanganyichanganyi...wao ni mafundi wa kubadilisha auto iwe manual nk,japani kuna sehemu nyingi wanaposaga magari wahuni wanakwenda kule wananunua kabda halijasangwa anaweka kapeti jipya..na rangi mpya..kisha sokoni ila uhuni huu hauwezifanyika UK
 
nchi yetu bado ushuru haueleweki vizuri hiyo gari ya 2007 ni model mpya kabisa sasa tra wanawezaku uplift sana CIF ikawa juu
ahsante kwa ushauri lucky sabasaba!vipi kaka weweza kuwa unafahamu japo kwa maksio yaweza kunigharimu kiasi gani hadi naiweka barabarani!sina uzoefu wa kuagiza magari na mambo ya ushiri (japo wa bongo haueleweki kama ulivyosema) na je hakuna namna ya kuukwepa hata kwa kupita mlango wa nyuma,maana naona ndo umekuwa utaratibu!!!
 
Japo haina uchakavu..ukipata agent mzuri unapashwa uandae 8.5ml..maana tra wataweka cif ya juu maana ni 2007 model(bongo ni jipya sana hilo)
 
wakuu kwa wajuzi wa magari nataka kuvuta haka kamkoko toka uingereza, kanasifa hizi:
bei paund 4990
2007 (56 reg), 4x4





  • 99,000 miles
  • Manual
  • 1.9L
  • Diesel

je niandae shilingi ngapi hadi kukaweka barabarani?

nini tofauti ya kununua gari uingereza na zile za japan?

natanguliza shukrani!




Mimi nina Toyota Rav4 ilinunuliwa kutoka Uingereza na kuingizwa nchini mwaka 2009, Ni Manual Transmission, ya mwaka 1999, Sports Ream, Mileage ni 120,000km na imelipiwa kodi na leseni hadi May. Nataka kwenda kusoma ndio maana naiuza. Ipo Dsm, kama utaihitaji tuwasiliane kupitia 0719077297.
 
Grand Vitara imetulia haswa, ukiangalia kwa ebay unaweza pata<rahisi zaidi ya hapo
sasa Mfikilwa!!haya magari yako ya ebay mbona yananipa maamuzi magumu!!ni mazuri lkn mbona hizo system za bei sijazielewa! mara bid mara buy now!which is which!mnada na mimi niko Pandagichiza nitauweza!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom