Gari la manispaa lakamatwa na meno ya tembo

COMPLICATOR2011

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
253
35
ASKARI wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi wilayani Mpanda Mkoa wa Rukwa, wanalishikilia gari la Manispaa ya Kigoma Ujiji, baada ya kulikamata likiwa na meno matatu ya tembo yenye uzito wa kilo tisa.

Dereva wa gari hilo alilitelekeza na kutokomea kusikojulikana.

Thamani ya nyara hizo za Serikali haikuweza kupatikana mara moja. Gari hilo aina ya Land Cruiser namba DFP 4383 mali ya Manispaa ya Ujiji mkoani Kigoma, lilikamatwa juzi saa 5:46 asubuhi katika Mtaa wa Kotazi katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, askari wa Hifadhi walimkamata mtuhumiwa, Elias Chambati (25) mkazi wa Mkoa wa Kigoma akiwa ndani ya gari hiyo ambaye anatuhumiwa kuhusika na tukio hilo akishirikiana na dereva wa gari hilo.

Chanzo hicho kinadai kuwa Chambati alikamatwa kutokana na taarifa walizokuwa nazo askari wa Katavi na uchunguzi walioufanya wa kumfuatilia nyendo zake za kujihusisha na biashara ya meno ya tembo.

Kutokana na taarifa hiyo, walimfuatilia siku hiyo ya tukio kuanzia kwenye nyumba ya kulala wageni aliyokuwa amefikia, Family chumba namba sita iliyopo katika Mtaa wa Mjimwema mjini Mpanda ambako walimfuatilia hadi walipomkamata akiwa ndani ya gari hilo.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, Chambati alikamatwa akiwa ndani ya gari hiyo na askari hao wa Hifadhi ya Katavi ambapo dereva wa gari hilo alifanikiwa kukimbia na kutokomea kusikojulikana.

Inadaiwa kuwa baada ya dereva kukimbia, askari wa hifadhi walifanya upekuzi katika gari ambapo walikuta meno matatu ya tembo yenye uzito wa kilo tisa ambayo thamani yake haijajulikana yakiwa yamefichwa chini ya viti vya gari hilo.

Baada ya kumkamata, askari hao wa Hifadhi ya Katavi, walifanya mawasiliano na uongozi wa Manispaa ya Ujiji Kigoma ili kupata msaada wa kumtambua dereva ambaye Chambati alikataa kumtaja.

Uongozi huo wa Manispaa ya Ujiji Kigoma ulimtaja dereva huyo kuwa ni Masoud Yassin ambaye ni mtumishi wa Hospitali ya Mkoa wa Kigoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage, amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo.

Alisema gari hilo lililotelekezwa limechukuliwa na kupelekwa kuhifadhiwa katika Ofisi ya Hifadhi ya Katavi, na Polisi kwa kushirikiana na askari wa Hifadhi wanamsaka dereva aliyekimbia.
 
ASKARI wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi wilayani Mpanda Mkoa wa Rukwa, wanalishikilia gari la Manispaa ya Kigoma Ujiji, baada ya kulikamata likiwa na meno matatu ya tembo yenye uzito wa kilo tisa.

Dereva wa gari hilo alilitelekeza na kutokomea kusikojulikana.

Thamani ya nyara hizo za Serikali haikuweza kupatikana mara moja. Gari hilo aina ya Land Cruiser namba DFP 4383 mali ya Manispaa ya Ujiji mkoani Kigoma, lilikamatwa juzi saa 5:46 asubuhi katika Mtaa wa Kotazi katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, askari wa Hifadhi walimkamata mtuhumiwa, Elias Chambati (25) mkazi wa Mkoa wa Kigoma akiwa ndani ya gari hiyo ambaye anatuhumiwa kuhusika na tukio hilo akishirikiana na dereva wa gari hilo.

Chanzo hicho kinadai kuwa Chambati alikamatwa kutokana na taarifa walizokuwa nazo askari wa Katavi na uchunguzi walioufanya wa kumfuatilia nyendo zake za kujihusisha na biashara ya meno ya tembo.

Kutokana na taarifa hiyo, walimfuatilia siku hiyo ya tukio kuanzia kwenye nyumba ya kulala wageni aliyokuwa amefikia, Family chumba namba sita iliyopo katika Mtaa wa Mjimwema mjini Mpanda ambako walimfuatilia hadi walipomkamata akiwa ndani ya gari hilo.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, Chambati alikamatwa akiwa ndani ya gari hiyo na askari hao wa Hifadhi ya Katavi ambapo dereva wa gari hilo alifanikiwa kukimbia na kutokomea kusikojulikana.

Inadaiwa kuwa baada ya dereva kukimbia, askari wa hifadhi walifanya upekuzi katika gari ambapo walikuta meno matatu ya tembo yenye uzito wa kilo tisa ambayo thamani yake haijajulikana yakiwa yamefichwa chini ya viti vya gari hilo.

Baada ya kumkamata, askari hao wa Hifadhi ya Katavi, walifanya mawasiliano na uongozi wa Manispaa ya Ujiji Kigoma ili kupata msaada wa kumtambua dereva ambaye Chambati alikataa kumtaja.

Uongozi huo wa Manispaa ya Ujiji Kigoma ulimtaja dereva huyo kuwa ni Masoud Yassin ambaye ni mtumishi wa Hospitali ya Mkoa wa Kigoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage, amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo.

Alisema gari hilo lililotelekezwa limechukuliwa na kupelekwa kuhifadhiwa katika Ofisi ya Hifadhi ya Katavi, na Polisi kwa kushirikiana na askari wa Hifadhi wanamsaka dereva aliyekimbia.

hehe uandishi mwingine
 
Maisha magumu maliasili lazima ziishe, ili kujazia mishahara na ukali wa maisha.

Hapa kila mtu atatafsiri kula kwa aina yake, Kina Rostam hawatangazwi na mkapa na wengineo
ila hawa ndg wanaojisaidia ili waishi watatangazwa ile mbaya kila kona.
 
Kesi hii itaenda haraka mno lakinin ile ya KIA na twiga unaweza kusikia mashitaka hayajakaa vyema hivyo wameachiwa jamani Tanzania ni ya ajabusana .Tutege masikio .
 
Wakuu nataka kujua bei ya kila jino la tembo. Mpaka mwaka uishe wengi washakuwa vibogoyo.
 
Back
Top Bottom