Gari canter tipper limeibiwa Stop over

Gari canter tipper limeibiwa Stop over

Wizi wa magari umechanganya miezi ya hivi karibuni.
 
WAPENDWA TUMEIBIWA GARI MITSUBISH CANTER TANI 2 AINA YA DAMPLER MAENEO YA STOP OVER BARABARA YA ZAMANI YA MOROGORO KARIBU NA KWA MBUYEKU.
NAMBA YA GARI NI T815DJF. RANGI BLUU NA ANGALIA PICHA HAPO JUU
TAARIFA kwa 0754750568 joseph mugyabuso au 0718800537/9754890664 margreth Kyai Mugyabuso

TAFADHALI SAMBAZA UJUMBE HUU KADIRI UWEZAVYO, MUNGU ATAKULIPA NDUGU YANGU

View attachment 433606
NIKUPE POLE, MUNGU ATWASAIDIA MTALIPATA...
 
WAPENDWA TUMEIBIWA GARI MITSUBISH CANTER TANI 2 AINA YA DAMPLER MAENEO YA STOP OVER BARABARA YA ZAMANI YA MOROGORO KARIBU NA KWA MBUYEKU.
NAMBA YA GARI NI T815DJF. RANGI BLUU NA ANGALIA PICHA HAPO JUU
TAARIFA kwa 0754750568 joseph mugyabuso au 0718800537/9754890664 margreth Kyai Mugyabuso

TAFADHALI SAMBAZA UJUMBE HUU KADIRI UWEZAVYO, MUNGU ATAKULIPA NDUGU YANGU

View attachment 433606


Pole sana, waungwana wapo nawe
 
Kwanza pole..lakini nikutie moyo kama ni jasho lako la halali basi utalipata..
 
Mkuu toa taarifa Polisi Kibaha, Mlandizi, Chalinze na Polisi wa Bagamoyo, baada ya hapo anza na watu wa karibu yako bila kuwasahau watu wa Gareji na dereva kwani hao ndio zao za kuchonga funguo na kulifuatilia kwa karibu
 
Polen sana, uwizi na ujambazi utashika kasi sana mwezi huu kwa sbb wana jiandaa na krismas huko Kilimanjaro
 
Pole sana Mkuu
a)Toa taarifa vituo vya polisi,na pia ikiwezekana fanya iwezekanavyo ipigwe patrol ya maana,na ungekumbuka haraka ungekodi kama bodaboda za kituo chote cha karibu yako wavamie mitaa basi ungelipata mapema,maana madereva wa bodaboda kwa issue kama hizo wangetoa ushirikiano wa awali

b)Ndugu zako wa karibu,hapa pia angalia watu wako wa karibu wakiwemo mandugu na marafiki zao.Huu mchezo kuna mazingira huwa unafanyika kwa watu wa karibu ambao wanakufuatilia.
c)Nenda na vituo vy TV kama ITV utoe tangazo,maana huu wizi zamani watu walikuwa wakiibia wanatafuta kimya kimya ila siku hizi ni rahisi,na ikisha vuja issue ya kutafutwa gari basi hakuna mtu atakae kubali gari ihifadhiwe kwake na ndio maana baadhi ya magari huachwa sehem

Ujumbe kwa Rais na wamiliki wa Magari
Tusiwe na mazoea kwamba ukiisha ibiwa ndioa kili ije.
Hivi unamiliki Gari jiji La Dar bila kuwa na GPS Tracking Systme?
Hii siku hizi imekuwa rahisi mno unalipa kwa mwaka na pia kuna bundle ambazo kama unamiliki hata boaboda unaweza kulipia.
Sasa kwa kwa vile hawa wezi wameishajua kwamba tumelala huu mchezo kila mtu asiekuwa makini analia.
Nakuambia kwa Ushuhuda,kwamba mie namiliki V Carry hapo Dar na vyote nimevifunga,na Pika kuna bodaboda zile aia ya Boxers nazo nimeziunga system na nimewaambia kwamba Drivers wangu wakivamiwa tu basi waliache gari na wasifanye ubishi.Maana almost kila baada ya masaa mawili huwa naifuatilie mwenendo wake.
Na pia ukifungiwa unakuwa trained kujua kama driver ndie au sie,so hata kama driver amechukuliwa sim basi utajua.Inasaidia sana.Ila wa TZ ni wabishi saana mpaka mtu limkute,na likimkuta basi muda mfupi tu anasahau

Jeshi La Polisi na Meya wa Jiji
Ningheomba kwamba muwe mnasikiliza vilio vya wenye magari,naamini kwamba kuna maduka kwa kumbukumbu zangu za miaka 20,yapo maduka ambayo yanauzwa vifaa vya wizi na yapo City Center na nje ya mji.
Hembu wekeni mfumo rasmi wa kuyafunga na kufuatilia hili,maana haya mtoto mdogo anayajua itakuwa nyie askari?na zamani walikuwa jeuri kweli,unakitua kitu hadi na number zako ila wanakuuzia,ila siku hizi ndio wanaona wafute ushahidi

Pole sana mkuu,ila utalipaa
 
Aisee huu wizi wa magari umekuwa tatizo, tutashindwa kupaki magari yetu sasa
 
Back
Top Bottom