Gambo: Awamu iliyopita kiongozi wa chini aliweza kuwa na nguvu kuliko hata Mimi Mkuu wa Mkoa

Enzi za utawala wa mwendakuzimu DC wa kakonko kigoma alikuwa anaweza kwenda namtumbo ruvuma au Dodoma na kupiga paranja la kufa mtu na hakuna RC ambaye angeweza hata kukema.
DC sabaya alikua anatoka hai anaenda Arusha kuwanyang'anya pesa wafanyabiashara na Hakuna anaehoji.

Hamnazo alikua dhalimu sana
 
"Watu wanasema mbona Gambo alikuwa m/kiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa lakini task force wakafanya unyang'anyi? Hawaelewi kuwa uongozi uliopita Ungeweza kuwa RC Ila kiongozi wa ngazi ya chini akawa na nguvu kutokana na anayemtuma kufanya mambo bila hata RC kujua". Mh Mrisho Gambo
Wewe Mrisho Gambo ulikuwa Snitch hata u-RC wako uliupata kutoka u-DC kwa kumchongea RC Ntibenda, yule Mhaya kwamba anashirikiana na Wapinzani.

Dhambi ya UNAFIKI itakuandama Sana,yetu Macho!
 
"Watu wanasema mbona Gambo alikuwa m/kiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa lakini task force wakafanya unyang'anyi? Hawaelewi kuwa uongozi uliopita Ungeweza kuwa RC Ila kiongozi wa ngazi ya chini akawa na nguvu kutokana na anayemtuma kufanya mambo bila hata RC kujua". Mh Mrisho Gambo
Mnafiki mkubwa huyu Gambo apunguze kuendelea kujisafisha kwa kauli zisizohitaji mtu awe na shahada ili amuelewe ana lengo gani.
 
Huo ndio ukweli mtupu!!watu watawalaumu sana, viongozi wengi waliopita, DPP, DCI, TAKUKURU, RC, DC, DED, IGP kwa mambo yaliyofanyika huku wakiwepo, lakini ki ukweli hawakuwa na namna ya kuyazuia, kwani mwendazake ndio alikuwa nyuma yake, labda njia waliyokuwa nayo ni kujiudhuru tu ili aone kuwa umekataa kutii, lakini ilikuwa lazima ujiandae kwa mateso(visasi)kwani usingeachwa hivi hivi tu!!!ndio maana wengi wao sasa matendo hayo yanawatesa sana!!ila tulikuwa ktk N.KOREA ya Afrika, MUNGU FUNDI
Sasa ndiyo watu wajue umuhimu wa katiba mpya..nchi hii ukipata Rais chizi anaweza hata kutembeza watu bila nguo...katiba hii inamruhusu na hakuna wa kuguna wala kushitaki popote.
 
Mbona hawakujiuzulu? maana kuna viongozi kibao walikataa teuzi. Na wengine waliomba kujiondoa
Hao wengi ni kina nani?aliyekataa uteuzi wa jiwe ni mmoja tu tena ya u DC, ila maswahibu yaliyomkuta , unayajua?je kwa ambaye angejiuzuru kisa kusimamia msimamo wake, uliotofauti na jiwe, kingemkuta nini??
Mbona hawakujiuzulu? maana kuna viongozi kibao walikataa teuzi. Na wengine waliomba kujiondoa
 
Why hakujiuzulu

Hata kama mimi siwezi jiuzulu,, hata wewe na uhakika huwezi fanya hilo! Nijiuzulu nikale wapi?

Kwanza Gambo bado kijana mdogo aliyekuwa anajijenga kisiasa na kiuchumi! Afadhali kuendelea kukomaa tu kwa unafiki hivyo hivyo tonge liende mdomoni! Na viongozi wengi wa awamu ya tano na uhakika ilikuwa siku ziende tonge liende mdomoni!

However, kwa watu wenye vision kubwa ya kiuongozi ndo hawawezi kuvumilia! Ila siyo kwa Tanzania hii ambayo ukikatiwa tu mshahara mwezi unaokuja hujui maisha yako yatakuwaje!

Watu waliojiwekeza na wenye uhakika na kesho ya maisha yao na familia zao ndo wanakuwa na maamuzi magumu kwenye uongozi wa hovyo hovyo!
 
"Watu wanasema mbona Gambo alikuwa m/kiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa lakini task force wakafanya unyang'anyi? Hawaelewi kuwa uongozi uliopita Ungeweza kuwa RC Ila kiongozi wa ngazi ya chini akawa na nguvu kutokana na anayemtuma kufanya mambo bila hata RC kujua". Mh Mrisho Gambo
ndio tatizo hilo la nchi kuendeshwa pasipo kufuata katiba na sheria zake,Mwendazake ndio chanzo cha yote hayo na si jambo la kuficha ukweli huo huo
 
Hao wengi ni kina nani?aliyekataa uteuzi wa jiwe ni mmoja tu tena ya u DC, ila maswahibu yaliyomkuta , unayajua?je kwa ambaye angejiuzuru kisa kusimamia msimamo wake, uliotofauti na jiwe, kingemkuta nini??

Pamoja na yoote, kuanza kuongea kwa namna ya kushutumu hakumuondoi kwenye lawama kama zipo. Na pia ni kinyume cha sheria kuanza kuongea mapungufu ya serikali uliyoitumia, eti kisa kwa sasa hauko nayo. Kiapo cha kutunza siri ni pamoja na mapungufu. Na unatunza wakati woote, hata kama hauko madarakani. Sasa kila mmoja akiongea aliyoyaona mbele ya umma itakuaje?
 
Sasa ndiyo watu wajue umuhimu wa katiba mpya..nchi hii ukipata Rais chizi anaweza hata kutembeza watu bila nguo...katiba hii inamruhusu na hakuna wa kuguna wala kushitaki popote.
Kwa CCM, kukubali kuruhusu mchakato wa katiba mpya ni ngumu sana, ile ya walioba ?kwani katiba hii mbovu ndio inayowalinda!!unasikia jitu linasema eti Mbowe ndio aliyeharibu mchakato kwa kuwatoa wapinzani kwenye bunge la katiba?!!katiba gani ile ya kihuni baada ya kuyatoa mapendekezo muhimu ya kuwatetea wananchi!!hata kama mama akiwa na nia ya dhati kwa hili la katiba ni gumu sana kwani huko nyuma kuna mijitu haitaki kabisa kwani yataona chama kinaenda kufa!!
 
Yeye Gambo alipokuwa anapambana na lema yalikuwa matakwa yake ama alikuwa anapokea maagizo? Mmbeya tu huyo! Hata yeye alikuwa anatumika sana. Asingepewa ukuu wa mkoa.
 
Hata ujioshe vipi husafishiki,umesahau wewe ulivyombishia waziri Magembe.
mnafiki mkubwa.
 
Back
Top Bottom