Gairo, wakati wa kutipuana umefika

Gairo, wakati wa kutipuana umefika

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,506
Reaction score
123,777
Gairo? or is it Cairo?

JF turudi kujadili mada zenye manufaa kwa Watanzania.

Kampuni inayoitwa Serengeti, jina la Kitaifa kabisa na la Kitanzania, ilipatiwa mradi wa kuwapa maji wana Gairo, kwa fedha nyingi sana. Jee, imewapa maji? kama jibu ni ndio! basi wanastahili kila sifa, kama jibu ni sio! Kwa nini? Tuchambuwe.

Kampuni hiyo hiyo sasa imepewa kutupa maji Darisalama. Jee, wataweza?

Nasikia wana mradi mwingine huko Zanzibar. Jee, wamewapa maji?

Cha kushangaza na kusikitisha, hii sio kampuni ya Kitanzania, ni kampuni inayomilikiwa na mtu anaeitwa Ali Talebi, ni Muiran ingawa ana Uraia wa Kitanzania wa kupewa. Si mzaliwa wa Tanzania, wala wazee wake. Na kajaza wafanyakazi wa Kiiran, seuse ya kuwa wana vikwazo vya Kimataifa.

Miradi yake yote kajaza menjimenti za WaIran, na haikamiliki.

Kwa nini watu kama huyu wanapewa miradi ya Kitaifa? Inayohusu uhai wa Watanzania? wana nini zaidi?

Ingekuwa wanatimiza, ningewaunga mkono na ningwasifia na kuwatetea kwa sana tu, lakini kwa mujibu wa habari zilizopo, hawatimizi miradi yao na wanatamba kuwa hakuna ataewafaya kitu.

Tujadili.

Hivi, hiyo miradi waliopewa> ni kwa vigezo vipi? kampuni za Kitanzania zilishindwa? (Ingawa na wao wanajifanya ni kampuni ya Kitanzania) Ukweli ni kuwa ni waongo, si Watanzania.

Hivi wale wana Usalama wa Taifa wanajuwa kuwa maisha ya Watanzania yako mikononi mwa hawa watu? maji, maji, maji!

Hivi wale wa idara ya kupambana na rushwa wameshachunguza hawa watu wanapataje hii miradi?
 
sasa faiza foxy..inaelekea unawafahamu vizuri ila thread umeiweka kimaswali tena!ila ngoja watu waamke asubuhi wa huko gairo watupe majibu
 
ila watz bwana hata maji tu tunawekeza kwa waarabu koko?
 
ila watz bwana hata maji tu tunawekeza kwa waarabu koko?

Waziri wa nishati na madini profesa Muhongo alisema uwezo wa Watanzania ni kuwekeza kwenye juice na matunda. Kwa hiyo wageni watakuja sana kuwekeza kwetu kwani sisi bado sana.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Kuna kitu hujakisema.... spouse wako ana interest kwenye shughuli kama hii.
Nauliza hili linatoka moyoni ama ni vita ya maslahi? Na kama ndivyo kwa manufaa ya nani?

Na kwa nini iwe Gairo na si maeneo mengine ambapo "shughuli" kama hii inafanyika ama na Kampuni
hii au inayofanana na hii kiutendaji. Let say "Singida" for instance!
 
sasa faiza foxy..inaelekea unawafahamu vizuri ila thread umeiweka kimaswali tena!ila ngoja watu waamke asubuhi wa huko gairo watupe majibu

Ndio, nna-wajuwa vizuri sana lakini nna-wawachia Watanzania wachambuwe.

Nakubaliana nawe, wana Gairo waje watueleze kama wamepatiwa maji na hawa Serengeti.
 
Kuna kitu hujakisema.... spouse wako ana interest kwenye shughuli kama hii.
Nauliza hili linatoka moyoni ama ni vita ya maslahi? Na kama ndivyo kwa manufaa ya nani?

Na kwa nini iwe Gairo na si maeneo mengine ambapo "shughuli" kama hii inafanyika ama na Kampuni
hii au inayofanana na hii kiutendaji. Let say "Singida" for instance!

Si "spouse" wangu mwenye maslahi. Ni mimi mwenyewe. Jee, wewe huna maslahi kwenye hili?
 
oops hizi ni habari za lumumba..si ndio wameshika nchi..si ndio wana midahalo mingi sana ya kutetea taifa la iran?si ndio waliopokea madakatari wa kuja saidia nyamazisha migomo na hatari ya kuindoa CCM?Si issue za kuanzia UDSM political science ...wapiga tarumebeta..wamepigia sana hawa jamaa upatu kw akiasi ch akuwiata ndugu zetu ..sijui comrades....ni wazi wana CCM wana mengi ya kuwaumbua..na wale wanaowalinda wairan kwa kigezo cha dini nao sijui watsema wayahudi ndio wamezuia mradi....

Naona huna hoja bali umeanza kuleta viroja.
 
Nieleze kati ya hao, ni nani asiye tumia maji?

pengine ungeniuliza nani kaleta hiyo shida..hilo ndilo swalo zuri..kuuliza nani anatumia maji na nani hatumii haliwezi kuwa swali.Haswa kwa miradi ya kodi za watu wote.


Wewe unadhani nani atakutatulia tatizo?
 
Mama Faizafoxy, maneno na maswali uliyouliza ni muhimu sana hasa ukizingatia suala la maji kila mtu anatumia. Moja ya sababu kuu inayonifanya kuichukia CCM na serikali yake ni mambo kama hayo uliyozungumza. Viongozi wa serikali hii ya CCM inawathamini sana wageni, kiasi imefikia kuweka maisha yetu mikononi mwao. Nakumbuka mwaka Fulani nilikuwa pale JKNI Airport, masuala yote ya ulinzi waliachiwa kampuni ya Ultimatum security. Sera za CCM ni mzuri sana lakini hawa viongozi naona walizizika siku ile Mwalimu alipozikwa.
 
Kampuni inayoitwa Serengeti, ilipatiwa mradi wa kuwapa maji wana Gairo, Darisalama, Zanzibar. Jee, wamewapa maji?

Cha kushangaza na kusikitisha, hii sio kampuni ya Kitanzania, ni kampuni inayomilikiwa na mtu anaeitwa Ali Talebi, ni Muiran ingawa ana Uraia wa Kitanzania wa kupewa. Si mzaliwa wa Tanzania, wala wazee wake. Na kajaza wafanyakazi wa Kiiran, seuse ya kuwa wana vikwazo vya Kimataifa.

Miradi yake yote kajaza menjimenti za WaIran, na haikamiliki.

Hivi, hiyo miradi waliopewa> ni kwa vigezo vipi? kampuni za Kitanzania zilishindwa? (Ingawa na wao wanajifanya ni kampuni ya Kitanzania) Ukweli ni kuwa ni waongo, si Watanzania.

Hivi wale wana Usalama wa Taifa wanajuwa kuwa maisha ya Watanzania yako mikononi mwa hawa watu? maji, maji, maji!

Hivi wale wa idara ya kupambana na rushwa wameshachunguza hawa watu wanapataje hii miradi?
Ungekuwa hivi siku zote tungekuwa na umoja na kuunganisha nguvu kupinga udhalimu serikalini.
 
Kwa mara ya kwanza mradi unatangazwa ilidaiwa kuwa ungekamilika ndan ya miezi 18 lakn mpaka sasa hamna kitu hyo ilikuwa october 2010 wale wa iran wapo wawil pale gairo hakuna la mada maji shda mpaka aibu kwa mama zetu. Kuna kipind vijana wa pale walitaka ku organize maandamano lakn wakaona wasubir uchaguzi 2015
 
Kwa mara ya kwanza mradi unatangazwa ilidaiwa kuwa ungekamilika ndan ya miezi 18 lakn mpaka sasa hamna kitu hyo ilikuwa october 2010 wale wa iran wapo wawil pale gairo hakuna la mada maji shda mpaka aibu kwa mama zetu. Kuna kipind vijana wa pale walitaka ku organize maandamano lakn wakaona wasubir uchaguzi 2015

Ikiwa huo hawajaumaliza na wamepewa mradi mwingine mkubwa zaidi wa kutupatia maji Dar. Jee, itakuwaje?
 
JF.

Daah. Mada ya muhimu kama hii hamjaipa kipaumbele zaidi ya upuuzi wa wanasiasa?

Mnasikitisha sana.

Hapa ndipo JF ilipofika?

Nawauliza, mnajuwa kuhusu maji na umuhimu wa maji kwa Mtanzania? na au mwingine yeyote duniani?

Leo tunashindwa kujadili utapeli wa wachache unaohusu maji! au ni kwa kuwa wote mnaoingia humu mna uwezo wa kununuwa maji? au kuyapata maji bila "effort"?

Inasikitisha sana.
 
JF.

Daah. Mada ya muhimu kama hii hamjaipa kipaumbele zaidi ya upuuzi wa wanasiasa?

Mnasikitisha sana.

Hapa ndipo JF ilipofika?

Nawauliza, mnajuwa kuhusu maji na umuhimu wa maji kwa Mtanzania? na au mwingine yeyote duniani?

Leo tunashindwa kujadili utapeli wa wachache unaohusu maji! au ni kwa kuwa wote mnaoingia humu mna uwezo wa kununuwa maji? au kuyapata maji bila "effort"?

Inasikitisha sana.

Dada FaizaFoxy kweli maji ni muhimu sana cha ajabu hata wawakikishi wetu bungeni ilishangaza walipoigomea hoja ya John Mnyika kuhusiana na maji hapo gairo hakuna maji was there few weeks ago tabu tupu maji ya kwenye madimbwi isijekuwa ndo Kama yake mabomba ya Dar yasiyotoa maji yapo Kama mapambo
 
Last edited by a moderator:
ila watz bwana hata maji tu tunawekeza kwa waarabu koko?

Watanzania inatakiwa tuamke muda wa kulalamika haupo tena....... Ni miradi mingapi wawekezaji wa ndani kama akina Mengi walinyimwa afu wakapewa wazungu? Inasikitisha serikali inaona wabongo hatuwezi kuwekeza hata kwenye maji. Siyo kila kitu tumwamini mwarabu/mzungu, iko siku watatuwekea sumu kwenye maji...

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom