Gadner G. Habash arudi rasmi Clouds FM

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,542
108,858

Ni Kwamba Muda Si Mfupi Mtangazaji Wa Zamani Wa Clouds FM Gadner G. Habash Ambaye Baadae Hadi Hivi Sasa Alikuwa Akitangaza Kituo Cha Redio Cha E FM Ametoka Kumalizana Na Uongozi Wa Clouds Media Group Na Kwamba Sasa Ni RASMI Kuwa Kuanzia Jumatatu Ijayo Atakuwa Akitangaza Katika Kipindi Cha JAHAZI.

Pongezi Kwake Gadner G. Habash Na Uongozi Mzima Wa Clouds Media Group Kwani Hakika Sasa Tutaanza Kuiona Ile Clouds Ya KITEGA UCHUMI Yenye Mafundi Watupu Akina Fina Na Kipanya Katika Power Breakfast Na Gadner Katika Jahazi.

Naomba Kuwasilisha Na Nirudie Tena Kusisitiza Kuwa TAARIFA HII HAINA CHEMBE YOYOTE YA DHANA NZIMA YA SIKU YA WAJINGA Kwani UKWELI Ndio Huo.


=======================


RASMI

Screenshot-4.png

Gadner akisaini mkataba wa kujiunga tena na Clouds FM akiwa na Meneja wa Vipindi wa kituo hicho, Shafii Dauda.

Hatimaye zile taarifa nyeti za dodoso kuhusu kurejea kwa Gadner Clouds FM zimethibitika pasi na chembe ya shaka.

Gadner amerejea tena Clouds Fm akitokea EFM alikokuwa akifanya kipindi cha jioni kiitwacho Ubaoni. Kabla ya kuajirwa na radio EFM, 'G' alikuwa mtangazaji wa kipindi cha Maskani cha Times FM. Kwa sasa, mtangazaji huyo anatarajiwa kurejea kwenye kipindi chake cha jioni cha Jahazi ambacho kilijizolea umaarufu mkubwa chini ya uendeshaji wake wa enzi hizo.

Gadner almaarufu kwa jina la utani ‘Captain’, anaingia kwenye kikosi cha Clouds FM ambacho hivi karibuni kiliweweseka kufuatia watangazaji wake wawili, Gerald Hando na Paul James wa kipindi cha PowerBreakfast kuacha kazi na kudaiwa kuingia mkataba mnono na E-FM radio.
 
kuna jamaa aliweka uzi hapasiku chache nyuma kuwa, PJ, Mwihava na Hando hawatakuwa tena na clouds power breakfast kuanzia tarehe moja april, kweli leo asubuhi nakutana na sauti za Fina na Masoud kwenye power breakfast, ila fedwa na Babrah bado wapo. by the way Hando na PJ ndo walikuwa wananifanya nisikilize PB. Ngoja tuone kama fina na masoud wateweza kurejesha ile ladha asili ya PB iliyokuwa kabla hawajaondoka clouds.
 
Daaaah naona Kusaga kaamua kurudisha watu walioipaisha clouds... Safi sana, nashawishika kurudi kusikiliza PB na jahazi sasa manake nilishaachaga kusikiliza

Mkuu Hujafurahi Kama Mimi Nilivyofurahi. Yaani Sijui Niwape Pongezi Gani Uongozi Mzima Wa Clouds Media Group Kwani WAMENIKUNA PANAPOTUKUKA Na Sasa Mimi Na Clouds FM Na Clouds FM Na Mimi. Nilipowasikia Akina Dada Fina Na Kaka Masoud Kipanya Asubuhi Na Kuthibitishiwa Kuwa Wamerudi Nyumbani Rasmi NILIRUKA Kwa Furaha Kubwa Mno.
 
Kuna kamgomo kwa watangazaji wengi wa sasa ndo maana kaamua kuwarudisha wa zamani

Hakuna Mgomo Mkuu Ila Mazoea Yalizidi Pasipo UELEDI Halafu Usisahau Kuwa Clouds Sasa Inakwenda Kuwa Ya KIMATAIFA Hivyo Inataka Pia Kuwa Na Watangazaji Wenye Exposure Kubwa Na Ya Kutosha Ni Siyo Wa " Oya Oya " Ambao Walikuwa Wamejazana Hapo.
 
Mkuu Niamini Kuwa Gadner G. Habash Amerudi Rasmi Clouds FM Na Jumatatu Utamsikia Rasmi. Huniamini Mkuu? Kuna Nililolileta Humu La Uwongo?
Hakika umekuwa ukitupatia habari za ukweli kila wakati, ila samahani kwa ushereheshaji mbaya.
 
Mkuu Hata Wewe Huniamini? Anyways Kuanzia Jumatatu Ijayo Andaa PONGEZI Zangu Kwani Nina UHAKIKA 100% Na Hii TAARIFA.
Mkuu hujanielewa nimesema mwisho wa kudanganya ni saa nne asubuhi na taarifa hii umeleta baada ya saa nne hivyo hazitakua za uongo
 
Back
Top Bottom