Mkuu tatizo letu kuu ni baadhi ya watu kukariri taarifa za CNN, FOXNEWS, CBS nk na kuzichukulia wanayo sikia humo kama ni Gospel truth!! Katika masuala ya propaganda Wamerika wamefanikiwa sana kuteka nyara akili za watu ambao hawana uwezo wa ku-analyse masuala ya Geopolitics kiundani, hawajiulizi hata siku moja kwa nini Wanawasakama Wachina eti waonyeshe bajeti alisi ya jeshi lao, mara ooh Warusi uchumi wao unayumba kwa nini wanaendelea kuhunda Silaha kali, mara ooh ma-hackers wa Urusi wamevamia mifumo yote ya IT ya Merikani kuanzia Serikalini, viwanda vya Silaha nk wanasahau kwamba Wamerika waliwahi kutamba duniani eti Warusi hawana akili na uwezo wa kuingilia mifumo yao ya komputa - propaganda tu za kitoto, wanawasema vibaya Warusi huku wanakwenda kuwaomba/nunua injini za Urusi za kusaidia kurusha roketi za Wamerikani, vile vile ni roketi za Kirusi ndizo zinategemewa sana katika kupeleka wana anga, spae, vyakula, madawa nk kwenye Satellite ya Kimataifa!!
Juzi juzi hapa Meli ya Kimerikani ilihingia Black Sea, kumbe Warusi walikuwa wanaifatilia (track) wakitumia mfumo wao wa kipelelezi na walijuwa wazi wazi kwamba Meli hiyo ndiyo yenye mfumo mkali wa kiulizi - kama kawaida yao Wamerikani walikuwa wanatamba sana kuhusu uwezo mkubwa wa kivita meli hiyo, basi Warusi wakaona wamepata Golden Chance ya kuwapa fundisho Wamerikani - Meli ilipokaribia sehemu Warusi wakarusha ndege nne kutoka the nearest base, mbili zikaruka kwenye higher attitude mbili zikaruka kwenye low attitude - Rada za Meli ya Kimerikani ziliweza ku-detect kasi, mwelekeo, na attitude za ndege za URUSI zikiwa umbali wa 50km, Wamerika wanasema baada ya sekunde kama kumi hivi kupita mara Screens za Rada, Compyutas, mawasiliano ya Radio (groundwave,skywaves including Satellites coms) zikazima gafla i.e hakuna cha mawasiliano yoyote na the nearest American Command and Control base!! - watu wa IT wanajua maana ya Blue Death (Diplay Units zinawaka rangi ya Blue tu uoni chochote!) na hicho ndicho kilicho tokea kwenye Meli ya Kimerikani, wanamaji wataalamu wa meli hiyo walijuwa wazi wazi kilicho wasibu - hawakuwa na la kufanya wakabaki wanangalia Ndege zinavyo katiza anga lao na kwa kuwa hazikuwa armed, Wanamaji wa kimerikani hawakuwa na wasi wasi!!
Ukosefu wa mawasiliano na uingiliwaji wa mfumo mzima wa control system za silaha za Meli hiyo zikawa hazifanyi kazi!! Tukio hilo lilidumu kwa dakika zote ishirini ambazo ndege za Urusi zilikuwa zina zunguka Meli ya Merikani, baada ya ndege hizo kuondoka eneo hilo ndio mawasiliano na Control system zikafufuka!! Tukio hilo liliwashtua sana baadhi ya wanamaji wa meli hiyo, inasemekana baada ya Wanamaji hao kueleza Wakubwa wao tukio zima lililo tia aibu Merikani, basi baadhi Wanamaji waliwasilisha barua ya kuomba kuhacha kazi za kijeshi na kutafuta kazi nyingine.