Wakuu,
Sisi wote ni vijana,hivyo ni vizuri kushirikishana.
Miye ningependa kwenda nchini Kuwaiti kuwa minajili ya kibiashara,na pia pia kwa makazi ya muda mfupi.
Ningependa kujuzwa na wale walio kwisha kwenda huko,je:
1)Ni biashara ipi ambayo naweza peleka,na taratibu za kuifungua?
Mathalani miye ni muuzaji wa asali mbichi,je nikiiboresha naweza uza huko?
2)Na je usalama kwa watu weusi ukoje?hawana ubaguzi?
Niko mbioni nafuatilia mwaliko wa kiutumishi na kiuchungaji kwenda huko,hivyo nimeonelea nianzie hapa.
Kwani sarafu ya Kuwaiti iko juu mno kuliko shilingi yetu,hivyo nimeonelea nichangamkie fursa hii.
Kwani Dinari moja ya Kuwait ni sawa na Shilingi 7509.47 ya kibongo!
Natanguliza shukrani!