Fursa iliyojificha kati kati ya utapeli

Fursa iliyojificha kati kati ya utapeli

officialBossmtoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2019
Posts
370
Reaction score
1,227
Habari wana jamvi wenzangu. Poleni sana lakini pia hongereni sana kwa majukumu ya kutimiza ndoto zenu. Kwanza niseme kabla ya kuendelea kwamba uzi huu sio rafiki sana kwa mtu mvivu wa kusoma, pia uzi huu unahitaji kidogo kutuliza akili ili unielewe. Tuweke mihemko pembeni.

Turudi kwenye Mada. Kumekuwa na fursa nyingi sana hapa nchini na Duniani zikiahidi vijana kuwabadilishia maisha, zingine zinafika mbali na kutumia watu ambao husema kwamba wameacha ajira za maana au biashara zao za maana na kujikita kwenye fursa hizo. Wengine pia huonyesha Magari ya kifahari na majumba makubwa kusema kwamba wameyamiliki mara tuu baada ya kuchangamkia fursa.

Hali hii huleta mgawanyiko wa makundi mawili.
Kundi la kwanza ni wale wanaoingia na kundi la pili ni wale wanaopiga vita kwa kusema ni utapeli na ni upigaji. Naomba kusema kwamba wote wako sahihi kabisa. Huu ni mtazamo wangu.

Mara nyingi fursa kama hizi zinapotokea wengi huwa wanakuwa na hizia za kutapeliwa mwanzoni na wanakuwa wazito sana kuweka au kufanya maamuzi. Kuna ambao hufanya tafiti mbalimbali kujua uhalali na uhalisia wa kitu huku wengine wakikataa kabisa hata kusikiliza. Wapo ambao wakiskia fursa kama hizo haraka haraka wanaingia bila kupeleleza na kuweka hela kwa tamaa huku wengine wakiweka hela kidogo kidogo huku wakisoma mchezo.

USHAURI WANGU
Mara nyingi hizi fursa huwa na mwisho wake. Hata wakijitahidi vipi, naona lazima itafika tu siku watasepa na mkwanja. Fuata yafuatayo ili uweze kunufaika na fursa hizi au kupunguza machungu ya kupigwa:

1:- Sikiliza kwa makini sana anaekupa fursa hii. Msikilize kwa kumzingatia na kuangalia kwanza uelewa wake juu ya jambo hili. Zingatia uweze kujua kwamba anajua anachokuambia ama amemezeshwa? M-challenge kwa maswali ya hapa na pale yenye kudodosa na kuchimba zaidi.

2:- Usikurupuke kuweka hela. Kwanza tambua historia, kisha tambua utendaji kazi. Uliza hela inatoka wapi? Sio unaambiwa tu unamuunga huyu na huyu unapata pesa, fahamu kwanza inatoka wapi? Je hela yako unayoweka ina usalama gani?

3:- Je inatambulika kiserikali? Japo hii usiipe nguvu sana. Wanaweza kua wanatambulika na wakawapiga tuu vile vile. Ila ni njia moja wapo ya kupata kaangalau fulani.

4:-Usitumie zaidi ya mwezi kufanya maamuzi. Mara nyingi tumeona fursa hizi wanaofaidi sana ni wale wa mwanzo. Mfano kama Scatec waliofunga ofisi na kusepa zao, sio kwamba watu hawakupata faida, watu walipata Faida sana. Wapo walionona mashavu kupitia scatec. Unapowahi unakua miongoni mwa wale watakaopata pata wa mwanzo kuliko kuendelea kujivuta ukose au ujiunge kwa kuchelewa ndo wale hicho ulichokiweka


5:- Usiweke hela ya Ngama. Nikisema hivi namaanisha kwamba usiweke hela unayoitegemea, usitoe kwenhe mtaji, usiuze mali yako ili weke huku, usiweke ada wala kodi.
Huku kwenye hii michezo weka hela ambayo hata ikipotea au ikiliwa unaweza jikuta unacheka tuu. Hii iwe kama kubet, muhindi anakula kila siku na watu wanaelewa kwamba hii ni bahati na sib.

Weka hela uliopewa zawadi, weka hela uliopata kwenye udalali, weka hela uliopata baada ya kuuza au kufanya biashara kwa faida kubwa zaidi. Ukishaweka hii hela unakua na machale kama mwewe.


6:- Hii ni ya muhimu sana EPUKA TAMAA. Michezo kama kalyinda, unavozidi kupata ndo hela inazidi kuongezeka. Mtu anaweza kufika mpaka laki tano, ila anawaza akitoa laki tatu na kubaki na laki mbili atarudi nyuma sana hivo anaona bora aendelee na hio laki tano. Badae inafika milioni anaona yale yale, mwisho wa siku anko mzungu anasepa nazo. Kumbe ni heri angetoa ile laki tatu acheze tena apate ingine atoe, yeye anataka izidi tuu basi.

7:- Hii ni kama onyo, Zingatia anaekuunga. Maana wapo wanaoungwa na marafiki zao, huku marafiki hao wakiwazunguka na kuchukua password wanaingia kwenye account zao wanabeba pesa.

Binafsi nimeskia Kalyinda na Scatec na kama una zingine tusaidie. ila pia hata za zamani kama deci ukifuatilia utajua ndugu zetu wa zamani walipata kweli wale wa mwanzo mwanzo. Waliozembea na kuja kujiunga mwisho, Hawa ndo walilia kweli kweli deci wanasepa wao hawajala chochote.

USHAURI huu wa bure vijana tuzingatie tuu. Hii ni namba ninayotumia mimi kupima fursa na naona kuliko nibet kwa Mbet bora nibet style hii. Nacheza kistaarabu bila tamaa na nikiona dalili za kunimeza nawahi natoa pesa yangu mapema


HII NI KAMA BAHATI NA SIBU. WEWE WAHI, WEKA HELA ZA KUSKIZIA, KAA KWA MACHALE, SUBIRIA KUTOKA KIMAISHA AU KUWATOA MAKAMPUNI KIMAISHA
 
MFANO KWA MTU ALIOKO KALYNDA ALIEWEKA KIASI CHA 50,000 AFANYE HIVI

Mimi nahisi lengo la kwanza liwe kwanza kurejesha pesa yako. Hii kwa 50,000 inarudi ndani ya siku 18. Baada ya hapo sasa unapambana kutafuta hela za faida. Huu ndo mtiririko wa hela na faida ya asilimia 4 kila siku ndani ya Kalyinda

52,000
54,080
56,166
58,413
60,750
63,180
65,707
68,335
71,068
73,911
76,867
79,942
83,140
86,466
89,925
93,522
97,263
101,154

Huo hapo juu ndo mtiririko na ongezeko la hela zako ndani ya siku 18 ambapo hapo utatoa 50,000 yako na kuendelea sasa kucheza kwa hela yao, au utaamua kuongeza mtaji. Maamuzi ni yako


ILA SIKU KALYNDA AKIAMUA KUWA SCATEC NA YEYE AKASEPA BONGI JUA KAMA UMEEKA HELA NYINGI BASI NDO UMEISHA.

HII NI KAMA BAHATI NA SIBU. WEWE WAHI, WEKA HELA ZA KUSKIZIA, KAA KWA MACHALE, SUBIRIA KUTOKA KIMAISHA AU KUWATOA MAKAMPUNI KIMAISHA
 
hakuna taasisi zina elimu ya pesa kama za bank.

bank ukiwapa 1mln wakuwekee katika acc ya riba baada ya mwaka wanakupa elfu 25 kama faida.wakiwa na maana hii,pesa yako wameitumia katika biashara mbali mbali hasa kukopesha watu wengine,faida iliyoingiza ndio hiyo wamekugawia na wewe.labda wao pia kwa kwa kutoka jasho wamejipa elfu 10 tu tuseme.

sasa hawa jamaa zako ili waeleweke na watu wenye akili inabidi waeleze hiyo 50k wanaifanyia nini ndani ya masaa 24 wakupe elfu 2

ujue mjini hapa wajinga wengi.mimi mwenyewe ni mjinga nahitaji kuelimishwa kila siku saa na dakika.
 
MFANO KWA MTU ALIOKO KALYNDA ALIEWEKA KIASI CHA 50,000 AFANYE HIVI

Mimi nahisi lengo la kwanza liwe kwanza kurejesha pesa yako. Hii kwa 50,000 inarudi ndani ya siku 18. Baada ya hapo sasa unapambana kutafuta hela za faida. Huu ndo mtiririko wa hela na faida ya asilimia 4 kila siku ndani ya Kalyinda

52,000
54,080
56,166
58,413
60,750
63,180
65,707
68,335
71,068
73,911
76,867
79,942
83,140
86,466
89,925
93,522
97,263
101,154

Huo hapo juu ndo mtiririko na ongezeko la hela zako ndani ya siku 18 ambapo hapo utatoa 50,000 yako na kuendelea sasa kucheza kwa hela yao, au utaamua kuongeza mtaji. Maamuzi ni yako


ILA SIKU KALYNDA AKIAMUA KUWA SCATEC NA YEYE AKASEPA BONGI JUA KAMA UMEEKA HELA NYINGI BASI NDO UMEISHA.

HII NI KAMA BAHATI NA SIBU. WEWE WAHI, WEKA HELA ZA KUSKIZIA, KAA KWA MACHALE, SUBIRIA KUTOKA KIMAISHA AU KUWATOA MAKAMPUNI KIMAISHA
Subiri kutoka kimaisha au kuwatoa makampuni kimaisha
 
Hahhaha kalyinda washafanya yao. Tulioweka hela za kunywea bia tunacheka. Waliouza sim wakaweka hela huko saivi wanalia na kutafta waganga wakaroge watu
 
Ndugu zangu,kwa sasa kumekuwepo na biashara nyingi za kimtandao ambazo zina element ya utapeli.

Biashara hizi nyingi zina aina moja ya utendaji ambapo unaingia kwa kuweka hela kisha kuwaalika wenzako na kupata hela kutokana na kile wanachoweka pamoja na hela uliyoweka.

Biashara hzi kwa sasa zimeeenda mbali ambapo waanzilishi wanapata Vibali toka Brela,Tra,pamoja na leseni toka manispaa nk.Hii ni kuaminisha watu kuwa biashara ni halali na Fedha zao zitakuwa salama.

Vijana wengi kwa kupenda urahisi wa maisha tumejikuta wahanga wa hili na kusababisha pia maumivu kwa ndugu na jamaa zetu wanaotuamini kwa kuweka fedha zao.

Jamani,hakuna biashara inayoweza kukupa faida nyingi/kila siku kirahis.Biashara nyingi za uwekezaji halali ni hisa,hati fungani za serikali nk lakni si hizi network markerting za sasa.Biashara hzi zote ni Ponzi scheme ambazo ufa mda mfupi baaada ya kuanzishwa.

Nina mifano hai mingi i.e kuna D9sports,Qnet na sasa kuna scatec na Kalynda.Zote hizi zina mfumo wa aina moja wa kupanda level kwa kuleta member wapya.

Mfumo huu ni wa kuchangiana ambapo member wapya huli0a fedha ambazo hutumika kulipa commission member wa zamani na hakuna biashara halisi inayofanyika.

Vijana wenzangu ni vyema kufanya kazi na kuacha kuwa na ndoto za kupata fedha kwa urahis ,mwisho wa yote huwa ni majuto na kupoteza kuaminika kwa jamiii inayotuzunguka.
 
Hasa, makampuni ya kubet yamekua mengi na matangazo radio yamekua kero na hii ya kalynda naona watu sijui wameshapigwa huko twtter wengi naona walijiunga.
All in all vijana tuchakalike na tusichague kazi
 
Hasa, makampuni ya kubet yamekua mengi na matangazo radio yamekua kero na hii ya kalynda naona watu sijui wameshapigwa huko twtter wengi naona walijiunga.
All in all vijana tuchakalike na tusichague kazi
Kubet siyo utapeli mkuu, mfano ubeti Simba kesho itaifunga Yanga na ikiifunga unapata pesa sasa hapo utatapeli vipi? Kwenye kubeti hakuna kutapeli wala kutapeliwa maana matokeo yanakuwa wazi kabisa
 
Back
Top Bottom