Fursa 2016 by Clouds Media ile ilikua ni siasa

Fursa 2016 by Clouds Media ile ilikua ni siasa

Nelson Kileo

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2011
Posts
3,054
Reaction score
3,263
Sijui ni kwanini manendelea kucheza na dira za vijana wa hii nchi .

Juzi mlikua mwanza mkatumia muda mrefu saana kukasanya vijana na kufanya kile mnachokiita ni utengenezaji wa fursa , sina uhakika tafsiri ya fursa kwenu ni nini haswa but mm natamfsiri kile kilichofanyika pale ni Siasa , Lobbing na

siasa
Necture ya watu mliowaalika wengine walikua ni wanasiasa , wengine hata walikua hawahusiki na mkoa husika , mkageuza tukio lile kuwapa wanasiasa uwanja wa kuendelea kupata coverage za media bila kuongea kilichokusudiwa .

Lobbing.
Kwa vile lengo lenu lilikua ni Fiesta basi mliona ule ndio muda wenu kamili kutumia njia ya kuita FURSA kumbe ni kujitangazia Fursa ninyi wenyewe . Ila kwa mtu mwenye akili pana lengo lenu lilikuwa wazi kabisa ni kuwaita na kuwahamasisha watu kuja kwnye FIESTA siku iliyofuta .

Mkitaka mjue hakuna kilichofanyika juzi kwa kile mlichokiandaa, kapitieni Notebook za baadhi ya vijana walihudhuria , kila mmoja akuambie ni nini alinote , hakika hutakuta kitu zaidi ya kichwa cha habari .FURSA 2016...NA NENO ''IMOOO''

Nataka niwashauri kitu kwa ufupi tu ,

Fusra si kualika watu na kututolea Ushuhuda wa Maisha yao toka wanazaliwa mpaka hapa walipo, tena wengi wenu mnaowatumia hawajua hata ni kwanini wapo hapo walipo.

Fursa ni kumsukuma mtu kwa nyenzo aweze kutoka mahala flani kwenda hatua niyngine .

Ni nn mfanye ,

Mkiwa kama Media kubwa mna nguvu kubwa ya kufanya na kuleta tangible impact kuliko kuwa na wazungumzaji tu kila siku studio.
Hiz naration za maisha ya watu zimeandikwa sana kwnye vitabu nadhani zinatosha kabisa kua kama chachu . Kwa sasa yatupasa kufanya hatua fulani kila tunapokutana kwa mwamvuli wa kutengeneza Fursa .


Iteni watu/vijana wenye Idea zao , mzichambue kisha mziwekee mitaji ninyi wenyewe kama clouds , hapo ndipo tutazalisha Fursa .

Fanyeni Fundraising.
Kuna wengi sana wenye uwezo wa kutoa nguvu za pesa pamoja na Machine , waiteni wawekeni chini na vijana hao wenye idea kisha kazi ifanyike .

Maswala ya kuita watu kutoa simulizi Fupi za Maisha yao ni kupotezeana muda na kutiana moyo katika njia za kudanganya huku mkibaki kunufaika ninyi wenyewe .
naisifu saana Project ya Kina Salama Jabir ,nadhani ile projrct ya BSS ni FURSA kuliko chochote Clouds Mlichowahi kukibuni nyie kwa Ground ya Fursa .

NNACHOKILAANI ZAIDI MNATUMIA WATU AMABAO HATA WAO UKIWAULIZA WAMEFIKAJE HAPO WALIPO HAWAJUI.
 
Sijui ni kwanini manendelea kucheza na dira za vijana wa hii nchi .

Juzi mlikua mwanza mkatumia muda mrefu saana kukasanya vijana na kufanya kile mnachokiita ni utengenezaji wa fursa , sina uhakika tafsiri ya fursa kwenu ni nini haswa but mm natamfsiri kile kilichofanyika pale ni Siasa , Lobbing na

siasa
Necture ya watu mliowaalika wengine walikua ni wanasiasa , wengine hata walikua hawahusiki na mkoa husika , mkageuza tukio lile kuwapa wanasiasa uwanja wa kuendelea kupata coverage za media bila kuongea kilichokusudiwa .

Lobbing.
Kwa vile lengo lenu lilikua ni Fiesta basi mliona ule ndio muda wenu kamili kutumia njia ya kuita FURSA kumbe ni kujitangazia Fursa ninyi wenyewe . Ila kwa mtu mwenye akili pana lengo lenu lilikuwa wazi kabisa ni kuwaita na kuwahamasisha watu kuja kwnye FIESTA siku iliyofuta .

Mkitaka mjue hakuna kilichofanyika juzi kwa kile mlichokiandaa, kapitieni Notebook za baadhi ya vijana walihudhuria , kila mmoja akuambie ni nini alinote , hakika hutakuta kitu zaidi ya kichwa cha habari .FURSA 2016...NA NENO ''IMOOO''

Nataka niwashauri kitu kwa ufupi tu ,

Fusra si kualika watu na kututolea Ushuhuda wa Maisha yao toka wanazaliwa mpaka hapa walipo, tena wengi wenu mnaowatumia hawajua hata ni kwanini wapo hapo walipo.

Fursa ni kumsukuma mtu kwa nyenzo aweze kutoka mahala flani kwenda hatua niyngine .

Ni nn mfanye ,

Mkiwa kama Media kubwa mna nguvu kubwa ya kufanya na kuleta tangible impact kuliko kuwa na wazungumzaji tu kila siku studio.
Hiz naration za maisha ya watu zimeandikwa sana kwnye vitabu nadhani zinatosha kabisa kua kama chachu . Kwa sasa yatupasa kufanya hatua fulani kila tunapokutana kwa mwamvuli wa kutengeneza Fursa .


Iteni watu/vijana wenye Idea zao , mzichambue kisha mziwekee mitaji ninyi wenyewe kama clouds , hapo ndipo tutazalisha Fursa .

Fanyeni Fundraising.
Kuna wengi sana wenye uwezo wa kutoa nguvu za pesa pamoja na Machine , waiteni wawekeni chini na vijana hao wenye idea kisha kazi ifanyike .

Maswala ya kuita watu kutoa simulizi Fupi za Maisha yao ni kupotezeana muda na kutiana moyo katika njia za kudanganya huku mkibaki kunufaika ninyi wenyewe .
naisifu saana Project ya Kina Salama Jabir ,nadhani ile projrct ya BSS ni FURSA kuliko chochote Clouds Mlichowahi kukibuni nyie kwa Ground ya Fursa .

NNACHOKILAANI ZAIDI MNATUMIA WATU AMABAO HATA WAO UKIWAULIZA WAMEFIKAJE HAPO WALIPO HAWAJUI.
Habari ni nzuri lakini ungeiandika vizuri zaidi na kuifupisha.
Kuna mtu anajiita street university lakini pesa kubwa anapatia katika kuandika udaku.
Nahisi kuna siku ataalikwa changu aliyefanikiwa nae atoe ushuhuda wa mafanikio yake.
Clouds ina wapenzi wengi na kuna wakati wanabuni vitu vizuri mno kama KIPEPEO lakini kuna wakati ukisikiliza kipindi kama JAHAZI unaona dhahiri upande gani wapo.
Maoni mazuri mmepewa yatumieni.
 
Mm nilijua mapema ni Promo ya Fiesta tu hamna kitu pale hata sijasumbuka kuenda.
 
Wajinga ndio waliwao na wanatumia udhaifu wa watu kujinufaisha kama ile Social Darwinism inavyostate

Hatuhitaji tena hadithi za maisha ya watu maana utasikia hata Bakhresa alikuwa anapiga kiwi
 
Ukweli wako ni mchungu kwa Ruge mana ni mzee wa fursa akinusa noti mahali
 
Hata kama ni motivation speak bado wapo superficial yaani juu juu sana.hakuna cha maana wanachofaidi hao vijana wanaowasikiliza zaidi ni mazungumzo mafupi tu. Kwa kifupi wanataja sekta zilizopo katika nchi na kuziita fursa kila mtu anajua kuwa kuna kilimo, real estate, ujasiriamalo.nk. hata wasemaje hawana mafanikio ya maana. Nadhani wazo lao ni zuri lakini linaitaji uboreshaji wa hali ya juu ili kuwe na faida yeyote na matokeo kwa walengwa.
 
Ukifanya impact evaluation ya waliopata hizo trainings za fursa na wasiopata unaona wapo sawa wote.
 
wapo walioongea point kama mrisho mpoto uliskia maneno yake lakini?
 
Msaada si lazima iwe ela, hata USHAURI au NENO likutialo nguvu na kukujenga ni msaada tosha, kwani hujui Kuna watu wanalipwa kwa kupitia ushauri wao, ambao unatokana na experience yao ktk fani husika.
 
Ruge fursa anaitumiaga vizur sana hafanyagi makosa ona jinsi alivyoitumia kujipatia zamaradi
 
Hiki kitu mm hua nawashangaa hata wanaokwendaga kupoteza mda wao,, maana watoa mada ni wanatoa ushuhuda tu na kujisifu, na wengi ni makada wa ccm
 
Clauds kama ingebaki neutural kama zamani ingekuwa ndiyo radio bora kabisa lkn kwa sasa ni radio ya hovyo kabisa na hasa pale wafanyakazi wake wanavyojipambanua na upande fulani wa siasa badala ya kuwa natural ukiangalia kwenye fb baadhi ya wafanyakazi wachopost had nashangaa na taaluma yao
 
Mwanasiasa anaetegemea maisha ya kuteuliwa na kura za wananchi ndo muhamasishaji wa fursa
 
Clauds kama ingebaki neutural kama zamani ingekuwa ndiyo radio bora kabisa lkn kwa sasa ni radio ya hovyo kabisa na hasa pale wafanyakazi wake wanavyojipambanua na upande fulani wa siasa badala ya kuwa natural ukiangalia kwenye fb baadhi ya wafanyakazi wachopost had nashangaa na taaluma yao
Ahadi za UDC zimeua taaluma ya uandishi wa habari nchini!!!!
 
Back
Top Bottom