Funzo kwa upinzani wa Tanzania kutoka Afrika Kusini

View attachment 1107494
Kiongozi wa Upinzani rasmi Afrika kusini Mmusi Maimane.

Uchaguzi wa Afrika kusini umeisha juma kadhaa zilizopita kwa chama cha ANC kuibuka mshindi ingawa kwa asilimia pungufu tokea uhuru wa watu weusi mwaka 1994. Uchaguzi huu tuliona vyama vya upinzani vikiongeza wabunge huku ANC ikipoteza viti zaidi ya 20. Na kubwa kabisa ni mikakati ambayo vyama vya upinzani Afrika kusini vilifanya ndio ilipelekea mafanikio haya na baadhi ya mafunzo wanaowapa wapinzani wa Tanzania ni kama yafuatayo.

1.Uhalisia wa malengo
Vyama vya upinzani Afrika kusini vinafahamu fika kuwa ANC ni zaidi ya chama dola bali DINI kabisa maana kuna watu wanakiona kama nembo ya ukombozi wa muafrika hivyo huwaambii kitu kuhusu ANC hivyo kuwachomoa huko inahitaji nguvu kubwa sana hivyo wana malengo ya "taratibu" yaani wanachagua Mikoa ambayo wanataka kuikomboa moja baada ya jingine hivyo wanawekeza nguvu maeneo hayo tu ili vyama vyao vizidi kukua kuliko kujikita kitaifa tu ambako inahitaji rasilimali nyingi na nguvu kazi ambayo kwa vyama vidogo ni ngumu kupambana na ANC. Mfano chama kikuu cha upinzani DA kiliweka malengo makuu matatu kuutetea "MKOA'' wa western cape na kushusha kura za ANC MKOA wa Gauteng na mkoa mwingine mmoja.

Hivyo rasilimali zote na nguvu kazi iliwekezwa maeneo hayo matatu hivyo wameweza kuyafikia na ndio maana wamekubali matokeo ila kama wangekuwa na malengo ya kukomboa mikoa yote 9 wangekuta hawapati hata mmoja sababu bado hawana rasilimali watu na pesa kulinganisha na ANC.

2. Uandaji Ilani
Hapa nimeambatanisha ilani ya chama cha DA ambacho kimetengeneza ilani yenye taarifa za undani zaidi jinsi ya kutekeleza ilani. Yaani wanaelezea kwa undani kabisa pesa fulani itapatikana wapi kwa kutumia data zilizopo na makadirio hivyo kuonyesha kweli wanauwezo wa kutekeleza walioahidi sio tu kusema kwenye ilani kuwa tutapunguza matumizi ya serikali bila kueleza shingapi zimetumika na wwe utapunguza kwenye maeneo gani na uweke tarakimu kabisa. Hii itaweza kushawishi mpiga kura kuwa unakielewa unachokiongelea kuliko maneno matupu.

3. Kujikita kwenye mafanikio ya chama sio udhaifu wa serikali.
Nilichojifunza kwa kupitia ilani ya chama kikuu cha upinzani DA ni jinsi walivyoandaa ilani zao kujikita zaidi kwenye mafanikio waliyopata majimbo/halmashauri zilizowachagua kwenye chaguzi zilizopita. Mfano ukiweka ahadi ya Elimu bure basi onesha mfano kwenye majimbo/halmashauri zinayoongozwa na upinzani jinsi ambavyo mmetatua shida ya gharama kwenye Elimu. Hii itawafanya waone mnaweza tekeleza mlichoahidi sababu majimbo mnayoongoza mmefanikiwa sio unaahidi maji wakati hakuna jimbo la upinzani lenye maji ya uhakika.

4.Kujikita kwenye kurejesha majimbo wanayoongoza(Retention).
Shida moja niliiona kwenye uchaguzi wa 2015 Tanzania Bara ni upinzani kuongeza majimbo mengi mapya lakini vilevile kupoteza majimbo mengi waliokuwa wanatawala mfano huko kanda ya ziwa walipoteza zaidi ya majimbo 90% waliokamata ila wakapata zaidi ya majimbo 5 mapya!!! Sasa hii haifai kwa upinzani unaotaka kukuaa. Nguvu kubwa iwekezwe kwenye kuimarisha chama kwenye majimbo ulionayo ili yasirudi chama tawala alafu uanze kazi upya ni bora uwe na majimbo 10 ambayo yatakuchagua milele kuliko kupata majimbo 5 mapya na kupoteza 5 uliyokuwa nayo unazidi kukiua chama maana yakirudi chama tawala huwezi washawishi wengine wakuchague ilihali majimbo uliyoongoza wamekukataa. Hili lifanyike kwa kuwekeza hata pesa za chama kwenye miradi ya Maendeleo kma elimu,afya,maji,ajira hapo majimbo hayawezi rudi chama tawala hata siku moja hivyo kujenga ngoma imara za upinzani kama walivyofanya DA huko western Cape ambako ANC ni chama cha upinzani kwa miongo kadhaa sasa.

Cc: Salary Slip chige kabombe Malcom Lumumba
Hivi hiki chama ndio anatoka malema cyo?
 
Naona umejikita kwenye chama mamluki cha DA. Katika uchambuzi wako nataka ufahamu kuwa upinzani wa Tanzania huwezi kuulinganisha na upinzani wa SA kutokana na uhuru wa kidemokrasia uliopo. Kwa hicho walichonacho Tanzania wapinzani wanahitaji sifa
 
Siasa za Afrika Kusini ni tofauti sana na Tanzania...Kwanza si ukweli kuwa kilichoibeba DA huko Western Cape ni strategies au sera ila ni kutokana na ukweli kuwa wakazi wengi wa huko ni asili ya kizungu na makaburu. Na kama tujuavyo sote DA ni chama cha makaburu na Maimane yupo tu lakini sio kiongozi halisi wa chama
Ningeona hii komenti yako wala nisingechangia. DA ni chama mamluki cha makaburu na wanamtumia tu huyu black katika kuwazubaisha Waafrika. Mwanamke aliyesimama na kusema NO ni Julius Malema na EFF yake. Kwa kifupi DA ni kama CUF ya Lipumba Tz
 
Naona umejikita kwenye chama mamluki cha DA. Katika uchambuzi wako nataka ufahamu kuwa upinzani wa Tanzania huwezi kuulinganisha na upinzani wa SA kutokana na uhuru wa kidemokrasia uliopo. Kwa hicho walichonacho Tanzania wapinzani wanahitaji sifa
Umamluki wa DA ni upi?? Kwa taarifa yako tu uchaguzi uliopita ndio kimepata kura nyingi zaidi za watu weusi kuliko wakati wowote ule.... Kiufupi ndio chama kikuu cha upinzani SA kwahyo kma weusi wana imani nacho je mtanzania ndio pekee umeona umamluki wao??

Kingine nmetoa mawazo ya namna ya kuandika ilani zao je hilo linahitaji uhuru wa kisiasa?? Kuandaa miswada mbadala kama ule wa Vijana alioandaa mnyika unahitaji uhuru wa kisiasa?? Kueleza kwa takwimu mchanganuo wa utekelezaji wa Ilani unahitaji uhuru wa kisiasa??

Jmn kuna mengine yapo ndani ya uwezo wa upinzani yafanyike yasiyo ndani ndio tulaumu ccm!!

Mfano Website ya chadema au cuf unajua mara ya mwisho kuwa updated lini?? Hotuba za KUB au kitabu cha sera hukipati kwa PDF mtandaoni?? Sasa unategemea wananchi watapata wapi taarifa ilihali bunge limezimwa??

Tusilaumu kila kitu CCM tujifunze hata kwa wenzetu
 
Ningeona hii komenti yako wala nisingechangia. DA ni chama mamluki cha makaburu na wanamtumia tu huyu black katika kuwazubaisha Waafrika. Mwanamke aliyesimama na kusema NO ni Julius Malema na EFF yake. Kwa kifupi DA ni kama CUF ya Lipumba Tz
Acheni kuexaggerate nguvu za Malema na EFF bado ni wachanga sana kwa DA.... Kitaifa hawajafikia malengo yao na kwa taarifa yako tu uchaguzi wa serikali za mitaa malema aliunda coalition na hao DA unaowaita mamluki na wakafanikiwa kubeba maeneo mengi sana hadi Gauteng walinyoosha ANC.

Sasa kama malema ndio unamuita mzalendo huku alishirikiana nao ni nani kusema ni mamluki?? Ina maana unaijua sana DA kuliko malema aliyeshirikiana nao??

Tuacheni ushabiki DA ni mfano wa kuigwa kwa vyama vya bongo.... Kina mfumo mzuri malema bado chama kidogo kikianza kukua kitakuwa na changamoto nyingi kuwahandle wale vijana wake hapo ndio mtapima ukomavu wa EFF.

Zitto alipohamia ACT alidhani kuendesha chama ni rahisi ila wote tuliona kilivyomuelemea hasa migogoro ilipoanza na viongozi waandamizi kuhama.... Kikabaki mikononi mwake tu. So EFF is too young to be compared to DA.
 
Hio ccm inamiaka mingap wew punga?
Achana naye huyo hajui CCM kimewahi kuwa na mweyekiti mmoja miaka zaidi ya 25!!

Tena akirudi muulize ni lini cheo cha mwenyekiti kimewahi gombewa kidemokrasia huko CCM zaidi ya mtu kupitishwa bila kupingwa??
 
View attachment 1107494
Kiongozi wa Upinzani rasmi Afrika kusini Mmusi Maimane.

Uchaguzi wa Afrika kusini umeisha juma kadhaa zilizopita kwa chama cha ANC kuibuka mshindi ingawa kwa asilimia pungufu tokea uhuru wa watu weusi mwaka 1994. Uchaguzi huu tuliona vyama vya upinzani vikiongeza wabunge huku ANC ikipoteza viti zaidi ya 20. Na kubwa kabisa ni mikakati ambayo vyama vya upinzani Afrika kusini vilifanya ndio ilipelekea mafanikio haya na baadhi ya mafunzo wanaowapa wapinzani wa Tanzania ni kama yafuatayo.

1.Uhalisia wa malengo
Vyama vya upinzani Afrika kusini vinafahamu fika kuwa ANC ni zaidi ya chama dola bali DINI kabisa maana kuna watu wanakiona kama nembo ya ukombozi wa muafrika hivyo huwaambii kitu kuhusu ANC hivyo kuwachomoa huko inahitaji nguvu kubwa sana hivyo wana malengo ya "taratibu" yaani wanachagua Mikoa ambayo wanataka kuikomboa moja baada ya jingine hivyo wanawekeza nguvu maeneo hayo tu ili vyama vyao vizidi kukua kuliko kujikita kitaifa tu ambako inahitaji rasilimali nyingi na nguvu kazi ambayo kwa vyama vidogo ni ngumu kupambana na ANC. Mfano chama kikuu cha upinzani DA kiliweka malengo makuu matatu kuutetea "MKOA'' wa western cape na kushusha kura za ANC MKOA wa Gauteng na mkoa mwingine mmoja.

Hivyo rasilimali zote na nguvu kazi iliwekezwa maeneo hayo matatu hivyo wameweza kuyafikia na ndio maana wamekubali matokeo ila kama wangekuwa na malengo ya kukomboa mikoa yote 9 wangekuta hawapati hata mmoja sababu bado hawana rasilimali watu na pesa kulinganisha na ANC.

2. Uandaji Ilani
Hapa nimeambatanisha ilani ya chama cha DA ambacho kimetengeneza ilani yenye taarifa za undani zaidi jinsi ya kutekeleza ilani. Yaani wanaelezea kwa undani kabisa pesa fulani itapatikana wapi kwa kutumia data zilizopo na makadirio hivyo kuonyesha kweli wanauwezo wa kutekeleza walioahidi sio tu kusema kwenye ilani kuwa tutapunguza matumizi ya serikali bila kueleza shingapi zimetumika na wwe utapunguza kwenye maeneo gani na uweke tarakimu kabisa. Hii itaweza kushawishi mpiga kura kuwa unakielewa unachokiongelea kuliko maneno matupu.

3. Kujikita kwenye mafanikio ya chama sio udhaifu wa serikali.
Nilichojifunza kwa kupitia ilani ya chama kikuu cha upinzani DA ni jinsi walivyoandaa ilani zao kujikita zaidi kwenye mafanikio waliyopata majimbo/halmashauri zilizowachagua kwenye chaguzi zilizopita. Mfano ukiweka ahadi ya Elimu bure basi onesha mfano kwenye majimbo/halmashauri zinayoongozwa na upinzani jinsi ambavyo mmetatua shida ya gharama kwenye Elimu. Hii itawafanya waone mnaweza tekeleza mlichoahidi sababu majimbo mnayoongoza mmefanikiwa sio unaahidi maji wakati hakuna jimbo la upinzani lenye maji ya uhakika.

4.Kujikita kwenye kurejesha majimbo wanayoongoza(Retention).
Shida moja niliiona kwenye uchaguzi wa 2015 Tanzania Bara ni upinzani kuongeza majimbo mengi mapya lakini vilevile kupoteza majimbo mengi waliokuwa wanatawala mfano huko kanda ya ziwa walipoteza zaidi ya majimbo 90% waliokamata ila wakapata zaidi ya majimbo 5 mapya!!! Sasa hii haifai kwa upinzani unaotaka kukuaa. Nguvu kubwa iwekezwe kwenye kuimarisha chama kwenye majimbo ulionayo ili yasirudi chama tawala alafu uanze kazi upya ni bora uwe na majimbo 10 ambayo yatakuchagua milele kuliko kupata majimbo 5 mapya na kupoteza 5 uliyokuwa nayo unazidi kukiua chama maana yakirudi chama tawala huwezi washawishi wengine wakuchague ilihali majimbo uliyoongoza wamekukataa. Hili lifanyike kwa kuwekeza hata pesa za chama kwenye miradi ya Maendeleo kma elimu,afya,maji,ajira hapo majimbo hayawezi rudi chama tawala hata siku moja hivyo kujenga ngoma imara za upinzani kama walivyofanya DA huko western Cape ambako ANC ni chama cha upinzani kwa miongo kadhaa sasa.

Cc: Salary Slip chige kabombe Malcom Lumumba
Vyama vingi tawala vilivyopo madarakani Africa vilipata madaraka toka Uhuru na vimejitengenezea utaratibu wa siri na wa muda mrefu kwenye nyanja zote kuanzia kidola,kidini,kifedha na kiutawala.Wananchi wengi wa Africa wanaaminishwa kwamba vyama pinzani ni dhaifu na havina sera na mikakati itakayo weza kusaidia nchi.
Hii ni dhana isiyofaa. Kwenye ulimwengu wa nchi zilizoendelea vyama vinapimwa kwa sera zao sio mali na nguvu kwenye chama. Na maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana bila kubadili vyama katika utawala vinginevyo tutaishia kulea vyama vyenye mizizi mirefu ya rushwa isiyotibika!
 
Back
Top Bottom