Fumbo la Maisha ya Binadamu: JICHO LA MUNGU

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,063
40,724
Kuwa hai ni bahati kubwa sana, lakini kuwa kiumbe chenye akili kuliko viumbe vyote duniani ni bahati mara 10,000 zaidi! (Hongera!)

Hivyo mpaka hapo wewe ni unique kwa kiwango ambacho ubongo wako hauna uwezo wa kung'amua. Imethibitika kwamba dunia ni sawa na chembe ya vumbi kwenye bahari isiyo na mwisho, lakini vilevile uwezekano wa kukuta chembe nyingine ndani ya bahari hiyo yenye uwezo wa kutunza uhai ni mdogo karibia sawa na sifuri, Dunia ni ya kipekee sana na wewe uko ndani yake, entity ya kipekee kama wewe kuwa ndani ya sayari ya kipekee kama hii ni bahati mara trillioni zaidi! (Hongera!)

Chukua dakika chache kujiuliza swali moja la msingi na la kipekee mno, "Je, ni kwanini nataka kuishi?" Hapa watu tofauti wanaweza wakaja na majibu tofauti, mimi nahisi jibu utakalotoa pengine ni haya au baadhi ya haya:

1.) "Nataka kuendelea kuishi kwa sababu maisha ni matamu na nataka nifaidi maisha haya". Chakula ni kitamu na kila mtu hufanya kila awezalo ndani ya dunia hii ili aweze kupata chakula kilicho bora na kitamu kuliko vyote! Ngono ni tamu na kila mtu hufanya kila awezalo ndani ya dunia hii ili aweze kupata mpenzi alie bora na mtamu kuliko wote! (Hongera!)

2.) "Nataka niendelee kuishi kwa sababu nataka niwe maarufu na mwenye kupendwa na kuabudiwa na mashabiki wangu". Power and respect (nguvu na heshima) ni vitamu sana na kila mtu hufanya kila awezalo ndani ya Dunia hii ili aweze kupata 'nguvu' na 'heshima' iliyo bora na tamu kuliko zote! (Hongera!)

3.) Ongezea ya kwako (Umepewa ubongo). (Hongera!)

Cha ajabu na cha kushangaza, jibu lolote utakalo kuja nalo halitakuwa sahihi..,lakini the reverse will be correct. Tuchukulie jibu lako no.1, Unaweza ukafikiri unataka uishi ili ufaidi chakula, lakini ukweli ni kwamba unafaidi chakula ili uishi, period! tena chakula kinafanywa kiwe kitamu zaidi pale uwezekano wa kukusaidia kuishi unapokuwa mkubwa na pia chakula hicho hufanywa kiwe kichungu zaidi pale uwezekano wake wa kukuondolea uhai wako unapokua mkubwa zaidi.

Unaweza ukafikiri unataka uishi ili ufaidi ngono, lakini ukweli ni kwamba unafaidi ngono ili binadamu waendelee kuishi milele, period! Tena ngono hufanywa kuwa tamu zaidi pale uwezekano wa kusaidia binadamu kuendelea kuishi unapokuwa mkubwa na pia ngono hufanywa kuwa chungu zaidi pale uwezekano wa kusaidia binadamu kuendelea kuishi unapokuwa mdogo.

Dadavua jibu No.2 na mengine yote utakayokuja nayo kwa mtindo huu huu wa 'reverse thinking' na utastaajabika.

Sasa kumbe tunarudi pale pale, hatuishi ili tufaidi bali tunafaidi ili tuishi, sasa je, NI KWANINI TUNATAKA KUISHI?!

DON FRANCIS


============================================
Update: 14/07/2021

 
Hili swali bado linanitesa jamani.., em' changansheni akili hizo.., its gud for your mental health!
 
Nataka kuishi ili nimuabudu zaidi Mungu aliyenileta hapa duniani, maana mimi ni kazi ya mikono yake. Na katika kumuabudu huko, nataka kuishi zaidi ili nikamilishe majukumu aliyonipatia hapa duniani k.v kuijaza dunia, na kutawala vilivyoumbwa naye.
Wewe ni mgumu sana kuelewa. (Nilishaatahadharisha kuhusu reverse thinking), haya ona;

1.) "Nataka kuishi ili nimuabudu Mungu", the reverse is correct, unamuabudu Mungu ili uendelee kuishi. Kivipi: wanaomuabudu Mungu hubarikiwa mali na watoto wengi.., hivyo wanaendelea kuishi kwa kutumia hizo mali na kwa kupitia watoto wao. Sasa Je, ni kwanini unataka kuishi?!

2.) "Nataka kuishi ili niijaze dunia na kutawala vilivyoumbwa naye", the reverse is correct, unaijaza dunia na kutawala vilivyoumbwa nae ili uendelee kuishi. kivipi: Kwa kuijaza dunia unafanya binadamu tuendelee kuishi, na kwa kutawala wanyama kama ng'ombe na kuwageuza kitoweo ni ili tuendelee kuishi. Sasa je, ni kwanini unataka kuishi?!
 
Wejamaa nikuheshim tuu kwasabab umetupa swali ambalo majibu yake tunayo sie wenyewe,sasa Mimi nitakuja na majibu sahihi,NGOJA NI ANDIKE KATIKA NOTEBOOK THEN NIWE NA PITIA KILA SIKU HILI SWALI. HAKIka NITA LIJIBU VYEMA MKUU
 
Wejamaa nikuheshim tuu kwasabab umetupa swali ambalo majibu yake tunayo sie wenyewe,sasa Mimi nitakuja na majibu sahihi,NGOJA NI ANDIKE KATIKA NOTEBOOK THEN NIWE NA PITIA KILA SIKU HILI SWALI. HAKIka NITA LIJIBU VYEMA MKUU

“God is not some goal-oriented planner who then judges things by how well they conform to his purposes. Things happen only because of Nature and its laws. “Nature has no end set before it … All things proceed by a certain eternal necessity of nature.” To believe otherwise is to fall prey to the same superstitions that lie at the heart of the organized religions.”
 
Kuwa hai ni bahati kubwa sana, lakini kuwa kiumbe chenye akili kuliko viumbe vyote duniani ni bahati mara 10,000 zaidi! (Hongera!)

Hivyo mpaka hapo wewe ni unique kwa kiwango ambacho ubongo wako hauna uwezo wa kung'amua. Imethibitika kwamba dunia ni sawa na chembe ya vumbi kwenye bahari isiyo na mwisho, lakini vilevile uwezekano wa kukuta chembe nyingine ndani ya bahari hiyo yenye uwezo wa kutunza uhai ni mdogo karibia sawa na sifuri, Dunia ni ya kipekee sana na wewe uko ndani yake, entity ya kipekee kama wewe kuwa ndani ya sayari ya kipekee kama hii ni bahati mara trillioni zaidi! (Hongera!)

Chukua dakika chache kujiuliza swali moja la msingi na la kipekee mno, "Je, ni kwanini nataka kuishi?" Hapa watu tofauti wanaweza wakaja na majibu tofauti, mimi nahisi jibu utakalotoa pengine ni haya au baadhi ya haya:

1.) "Nataka kuendelea kuishi kwa sababu maisha ni matamu na nataka nifaidi maisha haya". Chakula ni kitamu na kila mtu hufanya kila awezalo ndani ya dunia hii ili aweze kupata chakula kilicho bora na kitamu kuliko vyote! Ngono ni tamu na kila mtu hufanya kila awezalo ndani ya dunia hii ili aweze kupata mpenzi alie bora na mtamu kuliko wote! (Hongera!)

2.) "Nataka niendelee kuishi kwa sababu nataka niwe maarufu na mwenye kupendwa na kuabudiwa na mashabiki wangu". Power and respect (nguvu na heshima) ni vitamu sana na kila mtu hufanya kila awezalo ndani ya Dunia hii ili aweze kupata 'nguvu' na 'heshima' iliyo bora na tamu kuliko zote! (Hongera!)

3.) Ongezea ya kwako (Umepewa ubongo). (Hongera!)

Cha ajabu na cha kushangaza, jibu lolote utakalo kuja nalo halitakuwa sahihi..,lakini the reverse will be correct. Tuchukulie jibu lako no.1, Unaweza ukafikiri unataka uishi ili ufaidi chakula, lakini ukweli ni kwamba unafaidi chakula ili uishi, period! tena chakula kinafanywa kiwe kitamu zaidi pale uwezekano wa kukusaidia kuishi unapokuwa mkubwa na pia chakula hicho hufanywa kiwe kichungu zaidi pale uwezekano wake wa kukuondolea uhai wako unapokua mkubwa zaidi.

Unaweza ukafikiri unataka uishi ili ufaidi ngono, lakini ukweli ni kwamba unafaidi ngono ili binadamu waendelee kuishi milele, period! Tena ngono hufanywa kuwa tamu zaidi pale uwezekano wa kusaidia binadamu kuendelea kuishi unapokuwa mkubwa na pia ngono hufanywa kuwa chungu zaidi pale uwezekano wa kusaidia binadamu kuendelea kuishi unapokuwa mdogo.

Dadavua jibu No.2 na mengine yote utakayokuja nayo kwa mtindo huu huu wa 'reverse thinking' na utastaajabika.

Sasa kumbe tunarudi pale pale, hatuishi ili tufaidi bali tunafaidi ili tuishi, sasa je, NI KWANINI TUNATAKA KUISHI?!

DON FRANCIS


===================================================================
14/07/2021

Kaburi lafukuliwa
 
 
Tunaishi ili tuvumbue: utamaduni, dini, uashi, uhunzi, muziki, sheria za ulimwengu, akili bandia, hadithi, kushangaa, vita, silaha
 
Back
Top Bottom