Freewill yenye adhabu baadae hiyo sio Freewill huru, Huo ni mtego. Uhuru na hiyari kamili havipaswi kuwa na shuruti, shinikizo wala adhabu

Freewill yenye adhabu baadae hiyo sio Freewill huru, Huo ni mtego. Uhuru na hiyari kamili havipaswi kuwa na shuruti, shinikizo wala adhabu

Infropreneur

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2022
Posts
12,845
Reaction score
27,270
Theists Hi... 👋

Moja kwa moja kwenye mada. Sasa ni hivi.

Uchaguzi na Hiari ya kweli, ili viwe huru na vyenye uhuru kamili, ni lazima vifanyike bila shuruti, vitisho wala adhabu.

Ili chaguo liwe la kweli na la hiari, ni lazima lifanywe bila shinikizo, shuruti, vitisho au adhabu.

Watu wa dini wanaamini kwamba Mungu alitoa freewill ya mtu kuamua na kuchagua kutenda matendo atakayo kwa uhuru, hiari na maamuzi yake mwenyewe.

Halafu hapohapo wanakwambia endapo mtu ataamua kuchagua kutenda matendo mabaya kwa kutumia freewill ileile iliyowekwa. Basi atakutana na adhabu kali ya moto wa milele, Jehanam la moto🔥

Sasa hebu tujiulize hivi....👇

Kwa nini freewill haiwezi kuwepo bila mabaya kuwepo?

Je freewill inategemea mabaya yafanyike ndio ionekane ipo?

Kwa nini uwepo wa freewill utegemee uwepo mabaya?

Inashindikana vipi, freewill iwepo yenyewe tu, bila kutegemea uwepo wa mabaya?


Kuna haja na sababu ipi ya msingi mabaya yawepo na yafanyike kuonyesha eti kuna freewill?

Huyo Mungu alishindwaje kuumba Dunia yenye freewill pasipo mabaya?

Kama toka mwanzoni, Huyo Mungu alijua kabisa hapendi mabaya, Sasa
alishindwaje kuumba Dunia isiyo na mabaya? Alishindwaje kuumba binadamu wema tu, watakao mtii na kutenda mema siku zote na wakati wote?

Kama tangu mwanzo, Mungu alijua hapendi mabaya yafanyike, Kwa nini aliweka freewill ya mtu kuweza kuchagua kutenda mabaya?

Kama huyo Mungu ni upendo na anapenda watu watende matendo mema tu, Kwa nini aliruhusu mabaya yawepo na yafanyike kwa kigezo cha freewill?

Kama huyo Mungu anajua kabisa kuna freewill ya mtu kuweza kutenda mabaya, Kwa nini aje atoe adhabu wakati anajua kabisa aliweka freewill ya mtu kuchagua kutenda jambo lolote, ikiwemo mabaya kwa hiari?

Baada ya kujiuliza hivyo, Sasa tuangalie hii mifano hapa chini...👇

1-MFANO WA BABA NA MTOTO.
Tu assume, Baba ana mwanae ambaye ni mwanafunzi wa shule. Imefika siku ya jumatatu. Baba anamwambia mwanae hivi "Leo una uhuru na hiari ya kuchagua kwenda shule au kubaki nyumbanu" Lakini endapo nikirudi kutoka kazini nikakuta hujaenda shule, nita kutandika viboko vya hatari.

Huu tayari ni mtego sio uhuru wala
hiari huru.

Kwa scenario hii, Ni kweli mtoto amepewa uhuru, lakini sio uhuru ulio huru na wenye hiari huru. Kwa sababu endapo akichagua kubaki nyumbani asiende shuleni, Baba akirudi atamchapa viboko. Hivyo ili mtoto ajiepushe na adhabu hii, itambidi aende shuleni. Hivyo mtoto hatakuwa na uhuru wenye hiari huru.

2- MFANO WA MAJAMBAZI AU WEZI.
Wezi au majambazi wanavamia nyumbani kwako halafu wanakwambia una uhuru kuchagua, uwape pesa zako bila ya wao kukuua au wakuue kwanza kisha ndipo wachukue pesa zako.

Huu tayari ni mtego wala sio uhuru wenye hiari huru.

Kwa situation hii, ni kweli umepewa uhuru wa kuchagua. Lakini option ya pili uliyopewa itaondoa uhai wako. Kwa hiyo ili ukwepe kifo, itabidi ukubali option ya kwanza utoe pesa zako tu, ziende ubaki salama.

Baada ya kuangalia mifano hii, sasa turudi kwenye hii "freewill" inayodaiwa kuwekwa na Mungu.

Ikiwa matokeo ya mtu kuchagua kutenda mabaya ni hukumu ya milele na moto🔥 wa milele basi "freewill" inayohubiriwa ni sawa na hiari anayokupa jambazi anaposema, “Ni chaguo lako: pesa zako au uhai wako.” Uko huru kubaki na pesa zako, lakini utalipia kwa damu yako.

Kwa maana hiyo, ili mtu akwepe adhabu ya moto wa milele, hata kama freewill ya kutenda mabaya ipo, itambidi atende mema tu, ili akwepe kuingia motoni.

Na hii inakua sio freewill yenye hiari huru bali ni MTEGO wa kupeleka watu wakaungue moto, endapo watatenda mabaya.

Freewill inge make sense kama ingekuwa hivi:

Tenda mema au mabaya vyovyote sawa tu. Mungu anatupenda sote watenda mema na mabaya, bila kujali wala kutoa adhabu kwa yeyote. Kwa sababu kila mmoja yuko huru kutenda vyovyote kwa kutumia freewill iliyowekwa kutenda vyovyote.

Lakini hii ya kusema eti uko huru kutenda vyovyote lakini endapo utachagua kutenda mabaya, utachomwa moto. HII SIO FREEWILL, BALI NI MTEGO WA KUNASA WATU, WAKA UNGUE MOTO.🔥

Uhuru na hiyari kamili havipaswi kuwa na shuruti, shinikizo, vitisho au adhabu.

Vinginevyo huyo Mungu kama alikuwa hataki mabaya yafanyike, angeumba binadamu wema tu, watakao tenda mema siku zote na wakati wote.

Freewill inayo tegemea mabaya hiyo ni freewill ya mchongo. Na ni mtego!

I'm out.

Seran, Mallerina, Lax Al Mukheef secretarybird Poor Brain Lamomy
Iceberg9
 
My take;

Freewill haimaanishi kutokuwepo consequences, uhuru wa kuchagua hauondoi matokeo ya chaguzi! Bila possibility ya mabaya hakuna uchaguzi wa kweli kungekuwa na programmed obedience, sio free will!

Mkuu Infropreneur we aren’t robots, you are confusing freedom with immunity! Freedom is not equal to freedom from consenquences!
 
Mfano mtu A ameamua kutumia freewill yake kufanya ubaya wenye dhumuni la kufanya mauaji kwa mtu B.

Mtu A akafanya ambush akamshambulia mtu B na kufanikiwa kumuua.

Ikiwa Mungu anajali sana kuhusu freewill, je freewill ya huyu mtu B katika kuchagua kuuwawa au kutokuuwawa iko wapi?

Kwanini freewill ya mtu mwingine iweze kuathiri freewill ya mwingine?
 
Mfano mtu A ameamua kutumia freewill yake kufanya ubaya wenye dhumuni la kufanya mauaji kwa mtu B.

Mtu A akafanya ambush akamshambulia mtu B na kufanikiwa kumuua.

Ikiwa Mungu anajali sana kuhusu freewill, je freewill ya huyu mtu B katika kuchagua kuuwawa au kutokuuwawa iko wapi?

Kwanini freewill ya mtu mwingine iweze kuathiri freewill ya mwingine?
Umeweka vizuri kabisa.

Watu wachangamshe bongo zao.

Watumie kichwa kutafakari. Wasitafakari kichwakichwa tu.
 
My take;

Freewill haimaanishi kutokuwepo consebquences, uhuru wa kuchagua hauondoi matokeo ua chaguzi! Bika possibility ya mabaya hakuna uchaguzi wa kwelikungekuwa programmes obedience, sio free will!

Mkuu Infropreneur we aren’t robots, you are confusing freedom with immunity! Freedom is not equal to freedom from consenquences!
Kama dhambi ni chukizo kwa Mungu, ingepaswa akunyime uwezo wa kuitenda.

Sasa anakutishia kukuchoma moto, akikuchoma moto ile dhambi inafutika? Madhara ya ile dhambi yanatoweka?

Sio kwenye dini tu, kimsingi mwanadamu ana hiari ndogo sana kwenye haya maisha yake mafupi.
 
My take;

Freewill haimaanishi kutokuwepo consequences, uhuru wa kuchagua hauondoi matokeo ya chaguzi! Bila possibility ya mabaya hakuna uchaguzi wa kweli kungekuwa na programmed obedience, sio free will!

Mkuu Infropreneur we aren’t robots, you are confusing freedom with immunity! Freedom is not equal to freedom from consenquences!
Freewill yenye consequences. Na mojawapo ya consequence ni kupewa adhabu. Hio sio hiari yenye uhuru, ulio huru.

Ni freewill yenye mtego wa kunasa watu waka ungue motoni.

Vinginevyo, Freewill haipo na wote tupo conditioned kutenda mema tu.

Huwezi kuwa huru na kuchagua kutenda mabaya wakati unajua kuna kuchomwa. Itakubidi utende mema tu, ili kukwepa kuchomwa.

Seran
 
Mfano mtu A ameamua kutumia freewill yake kufanya ubaya wenye dhumuni la kufanya mauaji kwa mtu B.

Mtu A akafanya ambush akamshambulia mtu B na kufanikiwa kumuua.

Ikiwa Mungu anajali sana kuhusu freewill, je freewill ya huyu mtu B katika kuchagua kuuwawa au kutokuuwawa iko wapi?

Kwanini freewill ya mtu mwingine iweze kuathiri freewill ya mwingine?
Freewill ya mtu mmoja inaweza kuathiri mazingira ya mwingine kwa sababu tunaishi katika ulimwengu wenye interaction sio isolation.

Kama Mungu angezuia kila tendo baya kabla halijatokea kuilinda free will ya wengine basi freewill ya A isingekuwa halisi! Angekuwa anaingiliwa kila mara anapochagua vibaya! Ingekuwa dunia ya programmed safety sio ya uchaguzi wa kweli!

Hilo swali kwann freewill ya A iathiri B ni kwa kwa sababu freedom in a shared world inevitability overlaps!uhuru hauji na guarantee ya kutokuathiriwa, unakuja na responsibility ndiomaana kuna justice!
 
Kama dhambi ni chukizo kwa Mungu, ingepaswa akunyime uwezo wa kuitenda.

Sasa anakutishia kukuchoma moto, akikuchoma moto ile dhambi inafutika? Madhara ya ile dhambi yanatoweka?

Sio kwenye dini tu, kimsingi mwanadamu ana hiari ndogo sana kwenye haya maisha yake mafupi.
Mungu akikunyima uhuru maana yake unakuwa programmed. Adhabu haipo kufuta dhambi ipo kuonesha kuwa matendo yana uzito na kuna justice!limited freedom is still freedom😊
 
Freewill yenye consequences. Na mojawapo ya consequence ni kupewa adhabu. Hio sio hiari yenye uhuru, ulio huru.

Ni freewill yenye mtego wa kunasa watu waka ungue motoni.

Vinginevyo, Freewill haipo na wote tupo conditioned kutenda mema tu.

Huwezi kuwa huru na kuchagua kutenda mabaya wakati unajua kuna kuchomwa. Itakubidi utende mema tu, ili kukwepa kuchomwa.

Seran
Hiyo kitu ni ngumu mkuu na ndiomaana tuna option ya kuomba rehema! Imagine unatubu tu na unasamehewa unaanza upya! Mbona rahisi sana na motoni huendi🤷🏽‍♀️💃🏽
 
Back
Top Bottom