Elias Msuya
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 173
- 671
Mwenyekiti wa zamani wa Chadema, Freeman Mbowe ameeleza sababu ya kukaa kimya tangu wakati wa uchaguzi mkuu wa chama hicho, Januari 22, 2025, akisema wanaotakiwa kusema kwa sasa ni viongozi waliokabidhiwa mamlaka na chama.
Katika uchaguzi huo, Tundu Lissu alishinda nafasi ya uenyekiti kwa kupata asilimia 51.5 dhidi ya Mbowe (asilimia 48.3), huku John Heche akishinda nafasi ya makamu mwenyekiti dhidi ya Ezekia Wenje.
Soma pia: Ukimya wa Mbowe
Tangu wakati huo, Mbowe aliyetangaza kuwa atajikita kwenye biashara zake, amekuwa kimya, licha ya misukosuko iliyoibuka ikiwamo ya kuibuka kundi la G55 lenye makada wengi waliomuunga mkono, ambao sasa baadhgi yao wametangaza kukihama chama hicho.
Soma pia: Wataka Mbowe ajitokeze
Alipoulizwa sababu ya kuwa kimya, Mbowe alisema: “Niseme nini? Wasemao ni wenye mamlaka.. wasije wakadai "tunawashwawashwa.”
Kauli ya Mbowe imekuja siku moja baada ya Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Boniface Jacob maarufu Boniyai, kutangaza kwamba hakihami chama hicho na kuwaonya baadhi ya makada wa chama hicho wanaohama wakitumia jina la Mbowe.