Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,703
- 218,230
Kuwa wa kwanza kufahamu kwamba Yule Mwamba wa siasa za Tanzania , Freeman Mbowe , ambaye pia anafahamika kama Mtemi Isike , Laingwanaan ama Ustaadh Aboubakar Mbowe, Leo amekutana na Kamati ya Utendaji ya chama chake ya Jimbo la Hai , ambako ndiko alikopatia kadi ya uanachama wake.
Ikumbukwe kwamba Viongozi wa Chadema wa Jimbo la Hai , ni miongoni mwa lundo la viongozi wa Chadema Tanzania nzima walioteswa mno na siasa za kidikteta za awamu ya kikatili iliyowahi kutokea Tanzania , ile Awamu ya kishamba sana, awamu ya 5, Wengi wa viongozi wa Chadema Hai wameuawa na kuteswa , huku wengi wao wakifilisiwa mali zao kwa sababu za kisiasa.
Leo Kaka yao amekutana nao ili kuwafariji kwa kuombea Makaburi ya waliouawa , kufariji Majeruhi na kupanga mikakati mipya ya kisiasa.
Mungu ibariki Chadema