Forget Magufulisation, here is the reality

Umejibu vyema sana sana tuna tatizo la kujibu bila kusoma na kuelewa, hata hivyo hongera kwa kuchukua muda kumueleza kwa upole. unarejesha heshima ya JF
 

Safi mkuu
 
Natumaini takwimu za mwakani zitakuwa juu zaidi kama ni kila mwaka wanafanya utafiti huu

Inawezekana. Lakini inahitaji kufanya kazi kweli zaidi ya kucheza na mindsets za watanzania. Inahitaji mabadiliko makubwa sana ya mfumo wa uongozi na uwajibikaji. Hii inamaanisha, inahitaji Magufuli ajitenge kikwelikweli na 'zigo' la CCM. Na namna ya kujitenga inafahamika na ipo ndani ya uwezo wake kama rais. Akiweza kufanya hivyo, hakika ndani ya miaka 5, prosperity index yetu yaweza kuwa bora.
 
Siku inzi wakiwa na busara na hekima. Wataacha kueneza magonjwa na kuanza kutenegeneza asali.
 
Nchi ya kimagumashi chini ya utawala wa CCM
 
This is outrageous! We were in the same position at independence in 1961, i.e., 25th from the bottom (!), though the ranking then covered fewer nations and it was less comprehensive. Our position then was at per with the likes of Malaysia and South Korea. Whilst we are now worse off (54 years down the road) these nations are among the world's top industrialised powers. Strictly speaking, the figures in the ranking are not intended for akina Magufuli as they would just brush them off as nonsense, they for us to ponder and seriously chart out the future of our nation.
 

Wewe Hauna Akili!


Mi sikushangai kwani akili yako ilivyo kamwe huwezi kuelewa vitu makini! Huu ni mfano mmojawapo wa jinsi ulivyo tupu kichwani! Hata kukurupuka hakupo hivi! We bure kabisa!
Usipende kukurupukia mambo ambayo huyaelewi!
 

Great. However, as akina Magufuli are the ones to lead and make decisions on 'our behalf', we can't avoid them, can we? Unless, we adopt the Swiss way of governing: a truly direct democracy.

As much as I'm a believer in critical discussions about our nation's future, I'm afraid at this moment we need less discussions. Everything (to move our nation forward) has been researched, documented and discussed. As I have said, all the means and ways are on Magufuli's table and reach. He needs to act on them NOW as a statesman.
 
Sidhani kama uko realistic mkuu. Yaani survey ya mwaka mzima wa miezi 12 unaihusishaje na utawala uliokaa mwezi 1tu? JK kakaa miezi 10 na Magufuli miezi 2, ukitoa ripoti ya mwaka kwa serikali 1 hii ripoti itamhusu ile ya mwezi 1 ama ile ya miezi 10?

Labda rudia tena kusoma utaelewa! Sasa hivi Magufuli ndo Mkuu wa nchi ulitaka wamwongelee kikwete tena hapa? Magufuli afikrie anatutoaje huko! Na hii kwenye governance mwakani lazima tuporomoke tu, kwa haya mambo ya Zanzibar na kuzuia mikutano ya wapinzani huku wenyewe ccm wakifanya mikutano ni upumbavu uliopita kiwango cha upumbavu! Mwakani tutakuwa wa 140!
 
Nzi,Hii mada ni nzuri sana nafikiri unaweza ukabookmark ili kila mwaka tuwe tunaangalia tunakwenda wapi,Watawala wetu waliopita wameifikisha nchi sehemu mbaya sana kwa kujali maslahi yao.Magufuli ameonyesha ni kiongozi anayeweza kutusaidia sana.Kuna vipengele ambavyo vinapaswa kupewa kipaumbele na hadi sasa Raisi amejitahidi hasa

Economy,Governance,Education,Health,Entrepreneurship and opportunity,Mwisho wa mwaka tukutane tena kufanya assesment hapa naamini tutakuwa tumepiga hatua
 
Last edited by a moderator:
And, according to what is being evangelised, Tanzania shall be midle income country by 2025 - a dacade journey from now.
The point in discussion is far beyond being in bottom, middle, or top. It is about prosperity. About economic development, not economic growth.
Please! Our leaders pave the way in a good will.
Most of our countries lack 'leadership succession'. Once a leader step down, he step with all 'bags' and hints.
 
Watu hawataki Raisi Magufuli ashahuriwe ,akishalewa etc.wanataka apongezwe tuuu Kama walivyofanya kwa Kikwete.Constructive criticism ni nzuri kuliko kupingwa Kila kitu Kama vile mtawala ni malaika.Halafu mwisho wa Siku baada ya utawala mnaanza kutoa mapovu. Mko wapi mliokuwa mkija juu Kikwete akikosolewa?Sasa hivi nanyi mwamponda.Tabia ya ovyo.
 
Sidhani kama uko realistic mkuu. Yaani survey ya mwaka mzima wa miezi 12 unaihusishaje na utawala uliokaa mwezi 1tu? JK kakaa miezi 10 na Magufuli miezi 2, ukitoa ripoti ya mwaka kwa serikali 1 hii ripoti itamhusu ile ya mwezi 1 ama ile ya miezi 10?
Nakuunga mkono utafiti wa maana ni lazima uwe wa kipindi kirefu cha kutosha, ndiyo maana inanishangaza wanaomhukumu Rais wetu kwa siku chavhe alizokaa madarakani ikifikia wengine kupendekeza hata kusiwe na chaguzi vipindi vinne vujavyo! Angalia pande zote usiangalie upande mmoja tu
 

Mkuu, unafahamu maana ya kulaumu? Hapa nimetumia hiyo prosperity index report kutoa ushauri kwa rais; hususani kwa kumshauri aweke nguvu zaidi katika maeneo yanayolifanya taifa liwe chini kabisa katika dunia hii.

Kwa upande mwingine kwa kuwa ni muendelezo wa serikali ya chama kilekile sioni ubaya kutoa lawama pia. Kwa kuwa kilichofanyika ni kubadili mtu anayeongoza tu. Pia nimeleta ripoti kuonyesha kuwa kama taifa bado tuna kazi kubwa sana. Tusipende 'kuwehuka' kwa mambo ambayo yanafanyika sasa (haswa na viongozi wetu kwa kucheza na mindsets za waTZ) ilhali hali halisi maishani, mtaani na mifukoni mwa waTZ wengi siyo nzuri kabisa. Hiyo ripoti haimzungumzii Magufuli, inazungumzia Tanzania iliyo chini ya utawala wa CCM (chama kinachompa Magufuli uhalali wa kuwa rais) tokea Uhuru. Kwa hiyo Magufuli hawezi kuepuka kubeba lawama na kupokea ushauri wa kumtaka yeye awekeze jitihada zaidi katika kupambana na hayo matatizo.

Ripoti inapaswa kutufungua macho na masikio yetu, kuwa sisi bado sana. Tanzania si kisiwa cha amani kama tunavyoaminishwa. Mfumo wa elimu yetu ni mbovu sana, sekta ya afya ni mbovu sana. Haya ndiyo mambo ya muhimu. Na ninaamini kabisa, rais anaelewa fika kwamba njia za namna ya kuyatatua anazo mezani kwake.

Pamoja na hilo, tusichoke kumpa ushauri rais (naye awe ni mtu wa kupokea na kufanyia kazi ushauri) ili aweze kutumia njia na uwezo alionao kikatiba kubadili status quo ili kuleta prosperity katika taifa letu.
 

Kabisa. Nasikitika sana watu wanavyojadili humu kwa minajili ya unazi na ushabiki wa kisiasa usio na tija. Hii ripoti inatuvua nguo kama taifa, lawama haziwezi kukwepeka kwa serikali zilizopita na iliyopo sasa. Licha ya hivyo, kama ulivyosema, angalau Magufuli ameonyesha kidogo nia ya kufanya tofauti na wenzake. Sasa aende mbele zaidi kwa kubadili status quo (ambayo naamini kabisa ndiyo sababu kubwa ya taifa kuwa ranked chini hivyo) na kuweka misingi imara ya kiuongozi na kiuwajibikaji.
 
Last edited by a moderator:
Mi nadhani hata kama chadema wangetangazwa kushida uchaguzi uliopita namba zingebaki kuwa hizohizo tu,cha msingi tumpe mda magufuri tuone kama namba zitachange kitu ambacho kwa mtazamo wangu naona kitashindikana kwa approach aloanza Nayo.
 
Mi nadhani hata kama chadema wangetangazwa kushida uchaguzi uliopita namba zingebaki kuwa hizohizo tu,cha msingi tumpe mda magufuri tuone kama namba zitachange kitu ambacho kwa mtazamo wangu naona kitashindikana kwa approach aloanza Nayo.

Hili ndilo tatizo nimetoka kulisema hapo juu. Huwezi kujadili jambo bila kuweka maneno kama hayo? Kwa nini ufikirie hapa mjadala ni CHADEMA vs. CCM? Kwanini huwezi kujadili kama mtanzania tu? Ndiyo maana nikashauri kuwa ili mambo yabadilike inapaswa hata rais afanye kazi kama statesman, akiingia tu kwenye mkumbo wa kuwa partisan, basi indexes zaweza kuwa mbaya zaidi ya zilivyo sasa.

Na ni kweli, alivyoanza siyo vibaya sana na wala siyo vizuri sana kwa minajili ya matatizo tuliyo nayo, ambayo hayajafahamika leo wala jana (chanzo chake kikiwa ni mfumo wa serikali za CCM), na namna ya kuyatatua zinafahamika miaka na miaka. Shida ni uwepo wa kiongozi aliye tayari kufanya mambo kinyume na mfumo uliopo, kwa manufaa ya watanzania wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…