Nataka kujiunga na Forever Living Products niwe nauza bidhaa zao za alovera kama nyia ya kuongeza kipato changu. Wenye uzoefu naombeni ushauri au wale mliojiunga na mko mpaka sasa au mliojitoa ningependa maoni yenu.
Je inalipa kweli?
Hi Mjali Tumbo,
Kama umealikwa kwenye mkutano wa Forever Living na umevutiwa na bidhaa zao na biashara yao, mimi nakushauri usisite. Ingia mara moja.
Ila kama huna uhakika na umekuja hapa kupata uhakika zaidi kuhusu hii biashara ya Forever living na Network Marketing, ni vizuri ukaelewa kuwa hapa kuna aina 4 za watu.
- Waliokuwa hawana uzoefu na biashara hii na wapo hapa kukwambia kuwa hiyo biashara ni ya kitapeli na kukushauri upeleke pesa zako kwenye shamba au biashara nyengine ya uhakika zaidi.
- Waliojiunga katika hii biashara (aidha ya forever au Network Marketing nyengine yoyote) wakawa hawajafanikiwa na kukushauri kutofanya. Kwa vile wao hawajafanikiwa wanaona hakuna mwengine atakayefanikiwa.
- Walokuwa katika biashara ya Network Marketing isiyokuwa ya Forever na kujaribu kuiponda Forever na kukuvutia katika biashara yake.
- Wachache sana wenye nia ya kukusaidia na kujaribu kukupa ushaura kutokana na uzoefu wao.
Labda niweke wazi kuwa
mimi si mwanachama wa Forever ila naikubali sana hii kampuni na nina marafiki katika hiyo kampuni ambao wamefanikiwa na wanaishi
Lifestyle nzuri. Kama unataka kujua kama biashara ya forever inafanya kazi usiwe na shaka nayo. Inafanya kazi na wapo wanaovuna pesa nzuri. Nenda kwa huyo aliyekuelezea kuhusu hii biashara ujiunge mara moja.
Lakini ukweli usiopingika (na hii data inatoka Direct Selling Association) ni kuwa 90% ya watu wanaofanya biashara ya mtandao (biashara kama Forever) wanatengeneza chini ya $10/wk.
..... Wanaofanikiwa ni wachache.
Ila usishtushwe na hizo takwimu kwani hao 10% kumi wanafanya kitu ambacho 90% hawakifanyi na nitakueleza kitu gani wanafanya hivi punde.
Ila kabla sijaeleza ni muhimu kuelewa kuwa Network Marketing ni taaluma kama taaluma ya udaktari, uhandisi, rubani n.k. Ukitaka kupata pesa nyingi katiba biashara hii hakikisha unakuwa tayari kujenga taaluma yako hii ya Network Marketing. Hii sio biashara ya kutafuta watu kama watu wengi wanavyodhania.
Soma "How To Build A Successful Network Marketing Business In Tanzania" kujifunza zaidi.
Kama upo hapa kuangalia options nyengine ya biashara ya mtandao, basi nakushauri usome nakala hii kabla hujajiunga katika biashara yoyote ya mtandao, "WARNING! Do NOT join any Network Marketing Business Before Reading This"
Kama ushaamua kufanya Network Marketing na unataka kuwa mtaalamu anayejenga biashara hii bila matatizo, hakikisha unafanya yafuatayo:
- Kuwa mwanafunza wa taaluma yako (Network Marketing Profession):
- Website nzuri ya kupata taaluma hii ni NetworkMarketingPro.Com. Vile vile unaweza kujifunza mengi kupitia blog yangu Earn-Money-From-Home.Net (Ila mimi nina focus zaidi kwenye kujenga biashara hii kupitia mtandao)
- Soma vitabu vya profession hii. Kuna vitabu vingi vya kusoma. Nimelist hivi vitabu kwenye thread ya "Matatizo Ya Network Marketing Tanzania"
- Jenga orodha ya watu (list building) ambao watakuwa na aidha niya ya kufanya biashara au kununua bidhaa. Unaweza kufanya bila mtandao au unaweza kufanya (kama mimi) kwa kutumia mtandao. Kujifunza jinsi gani ya kutumia mtandao kujenga hii biashara nakushauri usome kitabu cha Mike Dillardcha "Magnetic Sponsoring" hapa
- Hakikisha wanaona opportunity ya biashara yako kila siku. Usiwe mvivu. Fanya kazi kila siku. Kama una uvivu wa kuonesha biashara yako kila siku (kama mimi) hakikisha unatumia system ambayo itakuwa inakufanyia kazi kila siku. System ninayoitumia mimi inaitwa Big Idea Mastermind (unaweza kuicheki hapa).
- Hakikisha unafanya mauzo kila siku. Vile vile unaweza kufanya mwenyewe au kwa kutumia system ambayo itakuwa inakufanyia mauzo.
Natumai maneno hayo machacho yatakuwa yamekupa mwangaza kiasi fulani ya jinsi kuifanya hii biashara. Una mengi ya kujifunza na kuna pesa nyingi sana za kutengenezwa katika hii biashara ingawa ukweli ni kuwa wengi hawatengezi. Biashara hii kama biashara nyengine sio ya kila mtu ila ya wachache wenye
moyo wa chui (not for cry babies).
Nakutakia kila la heri na Mwenyezi Mungu atakusaidia kama
nia yako ni safi (
kuwasaidia watu wanaotaka kupata huduma na maisha bora na sio kupata watu wengi ili utajirike).
Dr. Said