For those who fall in love with someone here

For those who fall in love with someone here

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Najua kuwa popote kwenye mkutano wa watu wa aina yoyote ile huwezi kuepuka baadhi ya watu kuvutiana kimapenzi
Hilo liko wazi

Kwenye hili ninalolizungumza hapa nadhani wengi walishasema lakini leo na mimi paroko nimeona niseme kutokana na kituko kilichotokea majuzi tu

Hapa watu wanakutana kwenye kujadili mambo mbali mbali hasa ya kimahusiano na mara nyingine utani na jambo hilo huoelekea baadhi ya watu kuanza kumuwaza mtu fulani kuwa ni wa aina gani kitendo kinachopelekea kuanza kuhisi kuvutiwa nae

Hili sio baya na ni kawaida kabisa na naliunga mkono

Lakini kuna jambo nataka niwahusie hawa watu wanaojikuta wanaingia kwenye kuvutiwa na watu hapa

Kwanza fahamuni kuwa hapa ni mahali ambapo mtu anaweza ku act au kwa kiswahili anaweza kuigiza tabia fulani na watu wakadhani ndivyo alivyo,kwa wale ambao ni watu wazima na wanafikiria vyema hili watakua wanalijua kabisa

Ni vyema sana mkawa makini sana na hawa watu hasa kama umeanza kuhisi kuvutiwa na mtu huyo,unaweza kumuona mfano Eiyer ni mtu mpole na mshauri mzuri kumbe kwenye maisha ya kawaida ni mtu ambae hata kumuita rafiki hafai ahilia mbali mpenzi hivyo ni vyema sana kuwa makini sana na udanganyifu huu

Jmambo lingime ni kuwa unaweza kuvutiwa na mtu hapa na ukaanza kujenga kwenye fikra zako jambo ambalo litakufanya uwe na matarajio fulani kwako.Unaweza kudhani labda mtu huyo ana elimu fulani,kazi fulani au uwezo wa kifedha wa aina fulani kumbe ni mtu wa kawaida sana na kiwango chake chake cha elimu na kipato ni karibu na kile cha chini kabisa na unapenda kukutana nae unaanza kujilaumu au kukata mawasiliano nae kisa umemuona sio kama vile ulivyokuwa unadhania

Ni vyema kusiwe na matarajio yoyote yale kwenu ili kuepusha haya matatizo lakini pia kama unahitaji mtu mwenye kiwango fulani kifedha au kielimu si uwatafute hao ambao unawaona huko kuliko kuja kuingia kwenye msongo wa mawazo kwa mtu usie mjua vizuri?

Ndugu zangu ninasema haya baada ya kijana mmoja ambae mimi ndie niliyemsababisha kujiunga JF kuingia kwenye mahusiano hapa kwa aina hii na member mmoja na baada ya kuonana dogo alinifuata na kuanza kulalamika na hapo hapo nilimpa za uso kwa kumueleza kuwa kama alikua anahitaji mwanamke wa viwango fulani si angewatafuta huko anaowajua na kuwaona?

Dogo hana hamu kabisa

Kama umevutiwa na mtu mfano nimevutiwa na Husninyo kama nahitaji mwanamke mwenye digrii kwanini nisimuulize kama anayo ili kama hana nichape lapa mapema?

Kama umevutiwa mfano na Eiyer na kilichokufanya ukavutiwa nae ni upole anaouonesha kwenye michango yake kwanini usitumie muda wako kukagua kama hayupo fake na ukajiridhisha?

Jamani hebu jaribuni kuwa makini na hii ili kepusha usumbufu usiohitajika

Kama umevutiwa na mtu kwasababu ya tabia fulani usijiingize kichwakichwa unaweza kujiingiza kwa jambazi halafu ukaja kumtafuta wa kumlaumu ukamkosa

Kama umejikuta uko kwenye mahusiano na mtu epuka kuwa na matarajio ya aina yoyote yale au muulize kabisa ili ujiridhishe na kama atakudanganya basi utakuwa na haki ya kumlaumu hapo utakapokuja kugundua sio kama alivyokuambia

Nawatakieni kila ka keri nyote na w/end njema sana kwenu

Nawapendeni nyote lakini sina matarajio yoyote yale kwenu ...Lol

Mbarikiwe...!
 
ujumbe mzuri baba paroko keep it up
bora uwaambie maana wengine wanaweza watu walioko jf ni wa viwango vya juu kumbe wengine ni wakawaida tu
 
Kuna mtu nilitaka kumuibukia,ila kwa thred hii nimeghairi. Thanx Paroko!
 
ujumbe mzuri baba paroko keep it up
bora uwaambie maana wengine wanaweza watu walioko jf ni wa viwango vya juu kumbe wengine ni wakawaida tu

Kweli kabisa miss neddy

Wengine tunaishi uswazi sasa mtu akifikiria siku akinitembelea nitamfuata na lexaz imekula kwake!
 
Last edited by a moderator:
Kweli kabisa miss neddy

Wengine tunaishi uswazi sasa mtu akifikiria siku akinitembelea nitamfuata na lexaz imekula kwake!

hahahahahhahaha umeona eeeeeh me nadhani bora matazamio ya kiasi hata ukikutana na ya juu sio mbaya kuliko kuweka ya juu ukikutana na mtu chini ya viwango utavunjika moyo
 
Last edited by a moderator:
Sawa baba paroko!!! Dah! Nilitaka kuanzisha uzi kuwa nimevutiwa na wewe Eiyer ila mmmmh! Nimerudi rivas mwanawane!!!
 
Last edited by a moderator:
hahahahahhahaha umeona eeeeeh me nadhani bora matazamio ya kiasi hata ukikutana na ya juu sio mbaya kuliko kuweka ya juu ukikutana na mtu chini ya viwango utavunjika moyo

Mi nadhani ni bora kutrokuweka matazamio kabisa

Maana unaweza kuwaza mtu anajitegemea kumbe analelewa na dada yake

Unaweza kudhani naishi kwenye nyumba ya kiwango kumbe naishi kwenye nyumba ambayo hata choo chake ni cha shimo na ili ujisaidie inabidi uwe makini na gogo linapodondokea ndani maana "ngoma" inarudi juu ukishangaa inakurukia

Utaweza kulala kwenye nyumba hiyo?
 
Baba paroko umenena kweli tupu,wengine ukituona live utatamani kurud kinyumenyume.
 
Mi nadhani ni bora kutrokuweka matazamio kabisa

Maana unaweza kuwaza mtu anajitegemea kumbe analelewa na dada yake

Unaweza kudhani naishi kwenye nyumba ya kiwango kumbe naishi kwenye nyumba ambayo hata choo chake ni cha shimo na ili ujisaidie inabidi uwe makini na gogo linapodondokea ndani maana "ngoma" inarudi juu ukishangaa inakurukia

Utaweza kulala kwenye nyumba hiyo?

hahahahahahaha baba paroko utavunja mbavu zangu
gogo kuludi juu majanga

lakini mimi naweza kulala popote
 
Back
Top Bottom