Fomu za Edward Lowassa zilitimia?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,143
Jana,wagombea wa CCM na CHADEMA walikwenda Mahakama Kuu ya Tanzania kusaini fomu za kuwasilisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulingana na matakwa ya Sheria za Uchaguzi. Wote wawili walijitokeza mbele ya Jaji Kihiyo.

Wakati Magufuli akiwasilisha fomu 40 za kusainiwa,Lowassa aliwasilisha fomu 6. Hiyo ni kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania,Mh.Kayoza. Kimahesabu,Lowassa hakuwasilisha fomu 34.

Fomu nyingine za Lowassa ziko wapi? Kwanini siziwasilishwe nazo kwa kusainiwa? NEC yaweza kumuengua asipotimiza masharti.

=================================


Chanzo: Mtanzania
 
Mkuu, hiyo hoja hata mimi imenichanganya. Ina maana NEC walifanya makosa kumpatia fomu pungufu ama kuna fomu ambazo hakutimiza masharti yake? Tatizo ninaloliona mimi kwa miaka mingi ni masharti ya ujazaji fomu kuwachanganya wagombea. Nakumbuka kesi ya Sambwee Shitambala
 
Sijaelewa kinachoendelea.Labda wanasheria itabidi watueleze.Forms 40 na forms 6.Inamaana zote zinatakiwa zisainiwena MAHAKAMA au kuna zile za muhimu zinazotakiwa kuwasilishwa?Kama ni kweli inamaana mwanasheria aliyeenda naye hakujua hayo?

Ni kitendawili???Au ni ile ya kwamba ametumwa kuua upinzani????:scared::scared:
 

Kwenye picha alionekana Wakili Mabere Marando
 
Yuko sawa kwa kua fomu zinazosainiwa ni zile alizoombea wadhamini tu katika mikoa aliyopita
 
Kimsingi hua wanapewa fomu zote 40 kwa ajili ya kukusanya wadhamini lakini fomu 6 tuu ndizo zinakua na haja sana NEC ingawaje hata ukipeleka zote 40 wanapokea

Mkuu mbona pana umbali mkubwa kati ya 6-40…!! Ni kweli hizi 34 zote ni makapi tu…!???? Mhh sijui labda kweli
 
Kimsingi hua wanapewa fomu zote 40 kwa ajili ya kukusanya wadhamini lakini fomu 6 tuu ndizo zinakua na haja sana NEC ingawaje hata ukipeleka zote 40 wanapokea
Umeandika ukweli kabisa wale wanaojua watakuwa wamekuelewa
 
Petro E.Mselewa kwa bahati nzuri gazeti la Mwananchi walitaka ufafanuzi NEC na wakaambiwa fomu zinazotakiwa kurejeshwa NEC ni nne tu. Usihofu kwani tunao wanasheria mahiri waliobobea na ndio wanaotuongoza. Tutafika tu...
 
Ndiyo maana nasema siielewi maana simuamini Lowassa isije ikawa kaja kuua upinzani kabisa

Usiwe na wasi wasi kila kitu kiko sawa mwaka huu hakuna hujuma zozote za kuua upinzani sitazofanikiwa tuna wanasheria makini sana .mwaka huu lazima ccm iondoke madarakani
 

Acha uoga ndugu! Jiaminiiiiiii!!!!!!
 
Kuna wagombea kila wanachofanya ni habari:mod:, hii inadhihirisha kwamba mgombea husika anawapa hofu washindani wake?
 

Wakuu angalieni lisijekuwa ndo bao la mkono lenyewe hilo!! Wakizingua tunahamishia kura zetu kwa Mwigamba (ha ha ha ha haaaaaaa!!)
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…