Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,238
Kama kuna zawadi kubwa naweza kuwapa watu
wengi kwa wakati mmoja basi ni hii.
Fireproof,...haimaanishi ukiwa na fireproof hautapatwa na ajari ya moto
bali ajali ikitokea utaweza kutoka salama.
Fireproof ni movie inayo ongelea mahusiano katika mapenzi na nini ukitegemee
kabla ya kuingia huko au kama uko huko ufanye nini ili kutatua matatizo ya mahusiano
yako.....Haimaanishi ukiiangalia hautapata matatizo kwenye mahusiano yako,ila
matatizo yakitokea utaweza kuya overcome kwa njia iliyo nzuri zaidi.
Mara nyingi tuna pitia katika nyakati ngumu sana,...na wengine
tunapo kuja kuomba ushauri,unakuwepo utani na kupoteza mwelekeo wa
topic hadi ushauri ulio hitajika una kosekana.
Wengi mko kwenye ndoa,wengine mko single lakini mna tarajia kuingia
kwenye ndoa hivi karibuni.
Ndoa zina matatizo mengi na raha nyingi vile vile,..lakini kabla ya kuingia katika
ndoa ni vyema ukajua kwa uhalisia kabisa yote utakayo kutana nayo.
Wengi wanapotoa viapo vyao kwamba "nitakuwa nawe kwa shida na raha bla bla bla"
actually sidhani kama huwa wana waza "shida" wanayo itamka ni nini.
Kumekuwa na tangazo sana mahali ninapo abudu kwamba week hii ijumaa
all married couples wataenda for a movie katika ukumbi walo chagua.
Bahati nzuri,walitaja jina la movie hiyo nami nikaitafuta harakaaa ili nione kuna nini
ndani yake.
Please,hupaswi kuikosa,uwe umeoa/umeolewa au una mpango wa kuingia kwenye ndoa
karibuni,please itafute hiyo movie uangalie,hautajuta kuutumia mda wako on it.
Naamini kuna mambo yameongelewa humo ambayo unaweza kuyatumia kama ushauri
kwako binafsi au kwa mwingine,lakini ni vyema ukaenda kisimani mwenyewe kuchota maji
upendavyo.
Speaker.