FINCA wanaziogopa Upper second hasa za UDSM!?

Status
Not open for further replies.
Tatizo watu wengi wanaichukia UDSM kwasababu walikua na dreams za kusoma pale ila wakakosa nafasi sababu ya ufaulu mdogo,ni ukweli usiopingika kile ni chuo bora east africa na kina historia na heshima kubwa ndani na nje ya nchi! wakufunzi wa viwango vya juu mfano prof shivji,kabudi,dr lwaitama.. na kimetoa na kinaendelea kutoa wanaharakati makini kama kina tindu lisu,zito kabwe,josh nassari na wengineo..
 
Jamani kuwa great thinker c kitu kidogo, mbn FINCA inajulikana na wengi tuliwahi apply,tukaitwa, tukafanya kazi na kuacha na sasa tuko Serikalini,vigezo vya kuitwa viko vingi mostly wanaangalia ulisoma nini si ulipata nini mfano hivi inaingia akilini umesoma mambo ya laboratory science au forestry ama fine and performing arts uende kuomba kuwa loan officer wakati hata idea ya ratios huna,hujui asset au liability ni nini!you must be a joke maombi yako wanatupa kwenye dust bin,as i said vigezo ni vingi mkuu kuna case ya umri based on the nature of the work itself au hilo pia hufahamu?pia kubwa ni personal biasness ya yule au wale waliopewa jukumu la kuselect nk nk,fanya utafiti wa kina mkuu before you put your poorly researched kama si poor minded threads jamvini na matokeo mnaleta ubishani wa vyuo usio na tija wala faida kwa wadau,over
 

mkuu cjakuelewa wanawaogopa kwakuwa mnaboronga kazi au mnadai mshahara mkubwa? Au ni kitu gani hasa kinafanya wawaogope?
 

Ilikuwa enzi hizo siyo sasa kinaporomoka kila kukicha na viongozi wa chuo hicho wasipoacha kutumika kisiasa kitapotea kabisa. Pia 7bu ya mtu kutaka kusoma hapo na kushindwa kwa 7bu ya ufaulu mdogo sio 7bu yakuwanyima ajira
 

Mkuu nashukuru kwa kuwapa ukweli heko kwa hilo
 
Naomba wasomi na wachambuzi mtambue kuwa huyu kijana hoja yake inawakilisha ''mentality'' ya vijana wengi wanaomaliza vyuo hapa nyumbani. Hili ni tatizo la attitude na certificate arrogance, nawaambia ni tatizo kubwa sana. Kudhani ukisoma UDSM au SUA,au Mzumbe basi wewe utakuwa ni bora kuliko mwingine. Vyuo vyote vya Tanzania hasa undergraduate ubora wake ni sawa kabisa, kwahiyo ubora wa mhitimu unatokana na mtu mwenyewe na sio kubebwa na jina la chuo.

Bahati nzuri nilikuwa kuwa mojawapo ya wahusika wa kuajiri wafanyakazi kwenye kampuni kubwa sana kwa zaid ya miaka kumi. Sijaona tofauti ya ubora wa mwanafunzi eti kwasababu ya chuo alichosoma hapa nyumbani. Hii arrogance ya vyuo, sijui GPA, sijui nini haikusaidii kwenye sokola ajira, actually nilikuwa nakasirika sana nikiona mtu kaandika GPA yake kwenye barua yake......ni dalili tosha ya kuniosha kuwa huyu mtu ni arrogant

Vijana wangu sasa hivi kuna vyuo vingi sana hapa TZ, wahitimu ni wengi sana, kuwa na shahada yenye GPA yenye akili sio issue, suala je una soft skills? maaana hayo mavyeti kila mtu anayo. Ningewashauri wahitimu wa sasa wajielekeze zaidi katika kutafuta ujuzi wa kuwawezesha kutenda kazi, mfano kujua matumizi ya kompyuta vizuri, kuandaa ripoti mbalimbali, namna ya kuandika emails, namna ya kuandaa business plan, kuandaa presentation, kuandika CV etc.

Ukishajua hivyo, hata ukienda kwenye usaili, hakuna kampuni itakuacha maana utakuwa na vitu vya ziada- kama tangazo moja linavyosema......ziada na attitude ndio watu wanaajiri siku hizi sio vyeti....maana kila mtu anavyo
 
mkuu unaweza ukanipa sababu zinazofanya waajiri watu wapya kila mara? maana huwa haipiti hata miezi miwili wanatangaza nafasi mpya...

staff management and motivation style yao ni mbovu sana. Kwa mtu mwenye akili sawia sikushaur ukafanye kazi na hawa jamaa. They know how to demoralise employees.

Hiyo employment turnover rate kwao ni kitu cha kawaida sana na kiukweli wanaingia hasara sana, sema tu hawawezi kuacha, lazima waendelee na biashara yao!
 

Pia kikawatoa akina Bana, Chenge, Lowasa na wengineo. Mkuu sio kila mtu anayepinga mawazo yenu anaichukia UDSM au alikuwa na ndoto za kusoma kwenye hicho chuo chenu. Pia fuatilia vizuri UDSM sio chuo bora zaidi hapa Afrika Mashariki.
 
mimi sio mwana udsm ila hapa umechangia kwa hisia. kwan gpa kitu gani m2 mwenye gpa ya 4.5 na 2.3 wote wana uwezo wa kufanya kazi gpa madesa tu yale

Vilevile inategemea kabla ya pepa ulikuwa na boom au hamna au ulikuwa jana yake umepiga kiroba kwa mama mosha au la...kuna factors kibao na GPA yenu
 
hii mitoto ya sikuhizi bana, yaani wewe umeona ukitaja udsm na upper second ndiyo watu wataogopa? sijui ni bangi ama petroli, jinga kabisa!
watu wanaajiriwa kwa vigezo, kama umekosa maana yake haujakidhi viwango
umekula ban kihalali kabisa
 
Wabongo mbona mnapenda porojo? Kama hujui lolote kuhusu FINCA si bora ukae kimya....jaribu kuelewa post. Habari za kubebwa na chuo zinatoka wapi?

dogo mbona watu wanakuelewesha hutaki kuelewa, unaambiwa swala la gpa kwenye real job environment sio ishu, kinachomata ni competency yako na ueledi wa hali ya juu katika kazi! ninao ushahidi wa watu wengi wenye hiyo hiyo upper second kutoka udsm kuajiriwa katika makampuni mengi nchini! na pia wapo wenye below pia wameajiriwa, na pia swala la kazi halijalishi umesoma chuo gani, kinachoangaliwa umesoma nini na unajua nini, nafurahi kuona sasa makampuni mengi yameanza kutoa WRITTEN INTERVIEW coz vijana wengi siku hizi mnapata gpa za chupi wengine za kununua afu mnakuja kutupigia kelele huku
 

Wanajamii nasukuru kwa kumwelimisha huyu jamaa aliyekuja na hii topic ya uongo, mi ninawashkaji watatu wanafanya kazi pale FINCA na kati yao wawili wana first class sasa iweje hawa hawakuwaogopa? Kama wengi walivyosema issu ya ajira inavigezo vingi na kila kampuni inavitu vyake vya kuangalia kulingana na aina ya shughuli wanayofanya, na kwa wakati huo wanahitaji mtu wa aina gani. Kwanza hata recruitment page yao unazidi kudanganya jamii sahihi ni http://fincatz.simplicant.com hata juzijuzi hapa nimeisikia clouds radio kwenye power breakfast wakati wanaongelea juu ya FINCA. Halafu issue ya kuajiri mara kwa mara inaweza sababishwa na mambo mengi mzee je unajua wameongeza huduma gani au matawi mangapi mapya wamefungua au clients base yao imeongezeka kwa kiasi gani, fanyia utafiti wa kina hoja yako kabla hujatuleta humu. Nawakilisha
 
Mkuu unaongelea kuogopa sababu umeshaogopa? ujinga upi unaouongelea au unakuja tu nawe upate cha kuongea? Umeona upper second na UDSM peke yake?
kijana, unabahati sana nilikuwa likizo, KUDADADEKI, siku nyingine usilete utumbo kama huu wa kuongelea chuo badala ya ujuzi, weledi, maarifa na n.k. KUDADADEKI zako
 
huyu dogo anakera sana na elimu yake ya madesa, anabahati sana nilikuwa kwenye BAN, ninge.....
 
nawewe ulikuwa unaandika huku umekalia jambia, eeh? udsm kitu gani bana, watu tulipita hapo miaka ile, enzi za kina prof. mayunga nkunya, lakini hatuoni sababu ya KUPAYUKA hovyo, kwakuwa hicho ni chuo kama vingine. isitoshe umaarufu wake unazidi kushuka kwasababu ya kizazi chenu hiki cha nyoka, mnakazania madesa badala ya uelewa, ndiyo sababu kutwa mnalalamika tu humu, ajira, ajira , ajira... nani anataka kuajiri MBUMBUMBU?
hata mimi siwataki kabisaa watoto wa ud kwenye kampuni yangu!!
 
 
Muanzisha mada nna mashaka kama kweli umesoma,na kama kweli umesoma nna mashaka kwamba elimu uliyoipata haikukusaidia meaning haujaerevuka,zama za kusifia vyuo zimepita mkuu dah unaona UDSM yenu kama iko mbinguni ungelisoma HAVARD au OXFORD nahisi watu tusingelala,fanya utafiti kabla hujaanza kupayuka na kuandika post zisizo na mashiko,kwa ajili ya watu kama nyinyi ndo maana watu wanahoji kuhusu pride ya hiyo UDSM yenu,pole
 
kijana, unabahati sana nilikuwa likizo, KUDADADEKI, siku nyingine usilete utumbo kama huu wa kuongelea chuo badala ya ujuzi, weledi, maarifa na n.k. KUDADADEKI zako

busara huna..mwenye akili timamu huongea kwa facts na si kutoa mijitusi kama mwehu...ulikula ban kihalali na naona unaitafuta tena.
 

Hivi wapi nimesifia chuo. Kwanini usiende kwenye mada na unaishia kunishambulia mimi? Au ndiyo kile kinachoitwa "inferiority complex" ? pole sana
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…