Financial Community (FICO) / Jumuiya ya kifedha

Financial Community (FICO) / Jumuiya ya kifedha

TheDealer

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2012
Posts
2,424
Reaction score
1,132
Salaam!

Mwaka wa 2014 unaisha mwaka wa 2015 ni wa kiuchumi zaidi. Wote nawakaribisheni kwa ajili ya kujumuika pamoja!

NB:
KUNA WATU AMBAO HAWATAELEWA KITAKACHOANDIKWA HAPA NA WATAANZA KUWAKATISHA WATU TAMAA, JF YA SASA IMEVAMIWA. HATA HIVYO WATU WEREVU WATAELEWA LABDA WASIRIDHIKE NA HUU MKAKATI:

Mkakati wenye huu hapa:

UTANGULIZI:

Tunaunganisha nguvu zetu za kiuchumi kwa kuunda Jumuiya yetu ya Kifedha. Kwa kiingereza tutaita FINANCIAL COMMUNITY (FICO) na kwa kiswahili tunaita JUMUIYA YA KIFEDHA. Jumuiya hii inakuwa na wanachama kati ya 50 na 100. Sio zaidi ya wanachama 100 na sio pungufu ya wanachama 50. Kila mwanachama atachangia sh 1,000,000 kwa mwaka. Mchango huu ni wa mara tu katika uanachama wake wote.

Kwa wanachama 50 kutakuwepo na sh 50,000,000 na kwa wanachama 100 kutakuwepo na sh 100,000,000. Hizi hela ni nyingi sana zinakaribiana kabisa na escrow ya tegeta. Kwa pesa hizi tunaweza kufanya uwekezaji wa maana na kuvuna hela nyingi kwa kadri juhudi zetu zinavyotutuma. Aina ya uwekezaji wetu ni wa assets zaidi. Hatufanyi uwekezaji wa ki maghumashi tunafanya kwa uhakika. Kumbuka hii Jumuiya sio y kibiashara ila inatumia loopholes za kiuchumi kutengeza hela. Haitalipa kodi na haitaki kusumbuana na serikali. Itajishughulisha na deals za mjini na economic frustration za jamii ya watanzania kutengeza pesa zake.

HAKUNA PESA YOYOTE ITAKAYOTOLEWA HADI SOTE KWA PAMOJA TUKUTANE TUFAHAMIANE HALAFU SOTE TUKUBALIANE NAMNA YA KUANZA KUTOA HELA KWA AJILI YA JUMUIYA YETU YA FICO. MATARAJIO YANGU NI KUKUTANA JANUARY, 2015.

Haitajishughulisha na masuala ya kijamii. Wanachama wajishughulishe wao kama wao kwa ubinadamu wao lakini sio ki FICO. Haiepukiki kujishughulisha na masuala ya kijamii; lakini kujishughulisha huko si kwa kanuni za FICO la hasha, ni kwa ubinadamu wa wanachama wa FICO tu.. FICO ni uchumi tu, ni pesa tu baaaaasi.

FAIDA YA KUJIUNGA NA FICO:

1. KUJIHAMI KIUCHUMI:
Wapambanaji wa masuala ya kiuchumi wanafahamu wazi kuwa uchumi huyumba na huimarika. Unaweza ukawa na biashara yako nzuri sana lakini ghafla bin vuu mtikisiko unakukumba. Unaweza kuwa na kazi yako nzuri, lakini ghafla bin vuu mtikisiko unakukumba utakuwa mgeni wa nani?.

Lakini ukiwa ndani ya FICO ukielea ndani ya ulinzi wa kati ya sh 50,000,000 hadi sh 100,000,000 na kama haitoshi upo ndani ya ulinzi wa binadamu kati ya 50 hadi 100 nini kitakusumbua buana! Unakuwa na uwanja mpana wa ku access mkopo kwa riba nafuu na kurudisha maisha yako katika heshima yake iliyokuwa nayo hapo mwanzo.

2. KUONGEZA KIPATO
Hizo 50,000,000 ama 100,000,000 zinatumika kuzalisha hela kila inapoonekana inafaa. Kwa mfano mdogo tu. Tukanunua kiwanja kama cha sh 10,000,000 sehemu nzuri mjini baada ya muda kama miezi mitatu tunaweza kuiuza sh 15,000,000. Hapa tuna deal na economic frustration hivyo inakuwa rahisi sana kupata vitu kwa bei rahisi zaidi kuliko kawaida! Kuna mifano mingi ya kiuchumi lakini hapa leo sitaweka hadharani.

Kwa ajili ya kuiteka nchi kiuchumi. Kila mwanachama anakabidhiwa kanda yake kwa ajili ya kufukuzia deals zinazopatikana upande wa kanda yake. Kwa mfano kanda ya masaki, kanda ya buguruni, kanda ya ubungo, kanda ya ilemela, kanda ya dodoma mjini, kanda ya arusha mjini, kanda ya gongo la mboto, kanda ya mwanza mjini, nk nk. Lengo ni kuhakikisha kuwa Jumuiya yetu imekumbatia deals mbalimbali ndani ya nchii hii.

Ikumbukwe FICO sio taasisi inayojiendesha kwa miongozo ya kiserikali, inajiendeha yenyewe katika dunia yake yenyewe. Sijui tuiiite ki fremason hata siijui lakini haipo kwenye mfumo rasmi wa kiserikali; ila tu ipo katika mfumo wa kisheria kwa ajili ya wanachama kuandikishana makubaliano yao kwa wakili kwa ajili ya kuimarisha uaminivu baina ya wanachama.

KANUNI NA TARATIBU ZAKE:

Wanachama wataunda kanuni za FICO yao wenyewe lakini muasisi wa FICO kwa maana ya TheDealer anapewa veto ya kanuni tano muhimu kwa ajili ya kulinda idea isipotee njia na pia kwa ajili ya kulinda usalama wa wanachama na mali zao. Huo ndio msingi wa veto ya muasisi wa Jumuiya hii.

Pia, kila mwanachama wa FICO ndani ya miaka 10 ya uwepo wake ndani ya FICO awe na uwezo wa kumiliki nyumba na usafiri. Kwa mipango iliyopo kuna kila hali ya mwisho wa mwaka kila mwanachama akachukua sh 20,000,000. Humu ndani ya FICO hatuendekezi umaskini.

SIFA ZA KUJIUNGA:
1. Ajue kusoma na kuandika
2. Awe na uwezo wa kuchangia sh 1,000,000
3. Asiwe mbaguzi wa kidini ama wa kikabila ndani ya Jumuiya

Sifa zingine watatengeneza wanachama wenyewe!

Kuna mengi mazuri sana ya kuyaweka wazi lakini siku tukikutana kwenye kikao ndio siku sahihi kwa ajili ya kuweza kuweka mikakati yetu yote hadharani!

Muda si mrefu Jumuiya hii itajaa, wahi nafasi kabla haijajaa!

NB: HAKUNA HELA YEYOTE UTAKAYOTOA HADI SOTE TUKAE KIKAO CHA PAMOJA NA KUKUBALIANA JUU YA UTARATIBU WA KUAMINIKA. JANUARY KUTAKUWA NA KIKAO KWA MARA YA KWANZA.

KWA YEYOTE ATAKAYEKUWA AMEVUTIWA NA JUMUIYA YETU HII AWASILIANE NAMI:

KARIBUNI SANA! FICO!

==============
UPDATES:
==============

Hadi leo tarehe 11.01.2015 tumefika wanachama 25 kikao mwishoni mwa mwezi huu. Bado kuna nafasi 25 zingine, hala hala wahi nafasi kama idea hii umeilewa ama unataka kueleweshwa!

=============
UPDATES
=============

Hadi leo hii 17.01.2015 mambo yanakwenda vizuri sana, tayari tumeshapata bonge la website kwa ajili ya kutumia kuwahabarisha umma kuhusu masuala yetu ya bidhaa tutakazouza baada ya kuzinunua. Ni site ya ukweli sana! Tayari pia tumeanza mawasiliano na kampuni moja ya masuala ya matangazo ya kibiashara tufanye nao kazi kama partners! Yote hayo ni kwa ajili ya kupanua wigo uwe mkubwa zaidi na zaidi!

Bado hujachelewa ndugu, wahi nafasi bado ipo!

FICO mkombozi wako wa frustration za kiuchumi! Karibuni sana!
 
Mkuu The Dealer anataka vetto na kanuni zake tano za kumlinda,ubarikiwe sana mkuu.

Mkuu pusha la magogoni !

Sio za kunilinda nadhani umesoma kwa haraka zaidi. Ni za kulinda idea na wanachama wa FICO. Sio kunilinda mimi; mimi ni mwanachama wa kawaida kama walivyo wengine. Watu 100 ni wengi sana usipoangalia wazo linaweza kupotea mkondo.
 
Last edited by a moderator:
Yes!

Naona wananchi wameanza kupiga simu na kutuma sms. Safi sana nawashauri mjiunge na whatsapp ili iwe rahisi sana kuwasiliana. Karibuni sana!
 
Nani mweka hazina?watu wataweka fedha zao kwa guarantor gani?mean TheDealer lazima uwe na kitu ambacho kitawapa watu tumaini na imani/Ni idea nzuri!
 
Last edited by a moderator:
wazo zuri sana,tunaomba mods hii kitu muiweke kiofisi zaidi na isiwe wazo la TheDealer peke yake (sijui kama nime eleweka)
 
Last edited by a moderator:
Nani mweka hazina?watu wataweka fedha zao kwa guarantor gani?mean TheDealer lazima uwe na kitu ambacho kitawapa watu tumaini na imani/Ni idea nzuri!

Tukikutana january 2015 kwenye kikao wanachama watatoa mwongozo kuhusu kuhifadhi hela. Lkn kwa sasa nadhani ni kuwa na account benki. Account hio itawekwa hela zote watu wanakuja na slip peke yake. Tutaweka utaratibu wa kuwa na signatories kwa mfumo maalum zaidi. Sh 50,000,000 haziwezi kuwekwa chini ya watu wachache lazima iwe chini ya walau robo tatu ya wanachama. Kwa kifupi wao wenyewe watapendekeza namna wanavyoona inafaa.

Ahsanteni sana kwa kunielewa. Maombi ni mengi sana, hata sikutegemea kwa kweli!
 
Last edited by a moderator:
wazo zuri sana,tunaomba mods hii kitu muiweke kiofisi zaidi na isiwe wazo la TheDealer peke yake (sijui kama nime eleweka)

Chinga one umeeleweka sana. Kwanza ume appreciate idea na pili umependekeza idea iwe framed kiofisi zaidi. Lkn wazo hili ni public sio la JF, japo limezaliwa na TheDealer lakini any individual anaweza kulitumia kwa ajili ya ku conquer hekaheka za kiuchumi. Kwa mtu yeyote mwenye kutaka details asisite kuwasiliana nami nimpe a to z!

Karbuni sana, msikawie ku respond muda unakimbia na wanachama wanazidi kufanya application kwa wingi!
 
Last edited by a moderator:
Huu utapeli mtupu

Ningeweza kuacha bila kukujibu, lkn nafsi yangu inanisuta. Ngoja nikujibu walau kwa kuuliza swali. Utapeli hapa unaingiaje wakati mamlaka yote umepewa wewe na wanachama wenzako?! Watu 50 na ushee sio rahisi kuwatapeli mali zao kijingajinga watu wana hasira na mali zao, umesikia kijana?!?!
 
FICO ndio mkombozi wako wa kiuchumi. Jiunge sasa! January 2015 kikao kikuu cha wanachama kwa ajili ya kujiwekea utaratibu wao namna ya kuendesha FICO yao!
 
Ningeweza kuacha bila kukujibu, lkn nafsi yangu inanisuta. Ngoja nikujibu walau kwa kuuliza swali. Utapeli hapa unaingiaje wakati mamlaka yote umepewa wewe na wanachama wenzako?! Watu 50 na ushee sio rahisi kuwatapeli mali zao kijingajinga watu wana hasira na mali zao, umesikia kijana?!?!

Mmmmm.... Community loan wengine hawa
 
ni ideal; nzuri sana tenasana bigup kwa kuwaza jambo jema hili
 
Back
Top Bottom