Final Decision: Nakimbia ndoa. Naogopa kuua

Final Decision: Nakimbia ndoa. Naogopa kuua

abbas-hassan

Member
Joined
Nov 21, 2013
Posts
11
Reaction score
15
Ndugu wanajf.

Nashukuru kwa michango yenu ya ushauri juu ya swala langu kwenye uzi wa "Nakimbia ndoa-Naogopa kuua". Nawashukuru sana na heshimu sana mawazo yenu.

Kwakua huyu mwanamke amekua sio mstaarabu na katili kiasi hicho nimeamua kufanya yafuatayo lakini kwa uchungu sana kwani ni uamuzi mgumu sana hata zaidi ya waliochukua CDM kwa zito.

Awali ya yote..kama nilivyowafahamisha...licha ya kumsomesha na kumgikisha hapo alipo sasa. Lakin kuna kubwa ambalo sikuliweka wazi ambalo mnaweza kuniona mjinga sana na kunishangaa kwamba mimi ni mwanamme wa namna gani.

Nakumbuka ilikua miaka 5 nyuma..huyu mwanamke nilienda kuchek nae afya(ukimwi). Na majibu yakawa yeye kaathirika. .mimi sijaathirika. Ilikua siku ya huzuni sana na majonzi. Nikamwambia anieleze alikopatia huo ukimwi....na kwann alinificha kwa kipindi chote hicho ili hali anamimba na kajifungua mtoto?..kwann hakua wazi kwangu na kwa mimba yake ili hata mtoto aepushwe na maradhi?

Akaniambia..alikua anaogopa angeniambia ningemuacha na kwamba alikua akinipenda sana. Kuhusu mtoto akasema alifoji vheti vha clinic ili asigunduliwe kua kaathirika. Hajui alikopata ngoma lakini anasema alienda kupima miaka saba kabla haya mimi kukutana nae na akaambiwa kaathirika.

Nilichofanya mimi siku hiyo, nilimwambia ivi:-

"Nimekusamehe...na sitakuacha kwa tatizo ulilonalo;.kwakua tumekua tukisumbuana kwa muda mrefu kupigishana kelele kwa mambo jamii ya umalaya..uzinzi..uongo..unafki. ...Nakuomba usinisumbue tena kuanzia leo. Nahaidi nitakua mfariji wako. Na nitaendelea kufanya mapenzi kama awali na itakua mara dufu. "

Kweli maisha yakaenda...nikawa namhimiza sana mambo ya Mungu. Nikampeleka na chuo kusoma. Huko sasa mambo yakaanza kwenda ovyo taratibutaratibu.....akaanza majibu ya dharau..mara nisikie mastory ya kugongwa na wanamme mara ana marafiki malaya. Nilikua naumia sana...natoka miles nyingi kwenda kunuona pale chuoni. Ilikua ni shida mpaka akamaliza.

Anyways..ni mambo mengi yaliendelea....na nilikua nikizini nae tu na tukaendelea kupata watoto. Cha ajabu kila nikienda kupima...majibu yangu ni negative mpaka leo hii. Sijui ni muujiza wa namna gani huu.

Huu ndio uamuzi wa mwisho ambao nimeamua kuufanya mimi Hasan Abas Abdalah baada ya kuongea na wazazi pande mbili, viongoz wa dini na watu wazima na humu jf.

1: Hassan achana na huyo mwanamke kabisa...ni kafri na muuaji mkubwa...sio mstaarabu hata kidogo.

2. Mwachie kila kitu...kaanze maisha upya. Nenda mbali nae kabisa. Nenda hata Mtwara au Morogoro kaanzishe maisha.

3. Wanawake wapo wengi sana...yupo Mungu aliyekuandalia..ambae atakutii kwa utayokua unamweleza na moyo wako utauona tu koz utakua umetulia wala hutakua na wasiwasi.

4. Ukitaka kuondoka haina haja ya kumuaga na kumtolea maneno makali au ya laana. Mwambie nashukuru...mi naondoka, nitunzie watoto wangu kwa kipindi hiki cha mpito. Na asijue unakokwenda.

5. Kua karibu na Mungu sana...achana na mambo ya wanawake kwasasa Hasan...tafuta hela...Mungu awe rafiki yako mkubwa.
6. Muondoe kabisa katika akili yako...hilo ni joka kubwa ambalo ulikua ukiishi nalo bila kujua.

Nimeongea na kiongoz wa dini mmoja asbh hii.....aisee nimeona akili imefunguka kabisa. Sasa nafua nguo kujiandaa na safari leo hii au kesho au jumatatu.


Mungu nitangulie na nilinde kokote niendako....nakuachia watoto wangu...walinde na waepushe na uchafu wowote. Nakuomba Mungu unajilie huko niendako nipate kibali cha mafanikio ili nije niishi na watoto wangu..wasome katika level yeyote ya elimu na kuwafanikishia kua na maisha bora na familia njema kabisa.


Namsamehe mwanamke huyu kwa yote na mi pia naomba Mungu unisamehe kwa mabaya yote ambayo nimekua nikimtendea. Mlinde pia...muepushe na roho chafu alizonazo....mhurumie. Mpe utashi wa kuelewa anachofanya.


Kwa wanawake wote wanaosoma uzi huu na wanatabia za kunyanyasa wamme zao au kua na majibu machafu ya kuwachanganya wanamme zao...nawasihi waache tabia hizo....sio vizuri kabisa mbele za Mungu.


Asante JF members kwa maoni yenu na ushauri. Mungu awabariki sana.


Nahitaji maombi yenu pia.
 
Nimekaa na mwanamke huyu zaidi ya miaka 6 kwa ugomvi na makelele. Hakuna maelewano yeyote. Hakuna furaha. Nikitaka kwenda kufanya jambo la maana hunipa stress mpka nashindwa kufanikisha jambo hilo. Nikishindwa sehemu yeye ndio anafurahi. Hakua na ushauri mzuri kwangu. Alikua ni mtu wa kunipa challange za mapenzi na sio maisha....kunichonganisha na wanamme wenzangu. Naondoka...naondoka but kwa maumivu makali. ...nilikupenda kwa moyo wote na kwa dhati kabisa. Inshalah!!
 
Pole sana mkuu,nimestuka sana kusikia kuwa kati yenu kuna muathirika lakini bado mmeendelea kuishi pamoja,sielewi hata nikwambie nini kwa sasa,uamuzi unaoufanya ni sahihi kabisi,lakini nakuomba chonde chonde usiende mbali sana ambapo utashindwa kuja kuwaona watoto wako.muombe Mungu akufungulie milango ufanikiwe ili uje uishi na wanao maana ndio wafariji pekee wa maisha yako kwa sasa.tafadhali sana jitahidi uzuie tamaa yako ya kimwili,wala usiwe na wazo la kuoa hivi karibuni.unaweza ukaanguka mikononi mwa mtu ukafanya maamuzi ya kuishinae baadae akaja kuwa kimeo tena,yaani ukawa umekimbia matatizo na umerudi kwenye matatizo tena.

kila la kheri kaka
 
Dah!pole sana kaka yangu,muombe sana Mungu,akupe nguvu,hekima na moyo wa subira kipind hki kigum.
Kwel kuna watu wana mitihan humu dunian..pole sana
 
Kwa upendo ulionao kwa huyo mwanamke, unastahili zaidi ya hayo anayokufanyia, you deserve better than that. Nenda kuna wengi wanatafuta watu watawapenda na kuwaheshimu
 
"So, what can't you take, decide which of the two options is harder and do the other.That way,no matter how hard your choices turn out to be,at least you can find comfort in knowing you're avoiding something even worse" Josephine Angelini. Hongera kwa maamuzi magumu.
 
Dah wewe ni simba kaka...... Una moyo wa chuma. Ishu iko kwa watoto sasa naona kama watapata shida sana. Sijui tuiekeje hii ila kama una mtoto mkubwa anayeweza kutizama wenzake uweke utaratibu wa kumtumia chochote kitu..... Dah inauma na imenigusa sana. Pole kamanda ila mwendo mbele usirudi nyuma.
 
Siku zote hili ndo huw aswali kwa kichwa changu, ina maana mungu wakati anaweka ndoa/mapenzi alikuwa hajui madhara yake?? kwanini alituwekea hii kitu inayotesa dunia kwa sasa, ukigeuka kushoto presha, kulia kilio, nyuma matatizo mbele ndo kifo kabisa unakiona sasa ninini hiki
 
Dah wewe ni simba kaka...... Una moyo wa chuma. Ishu iko kwa watoto sasa naona kama watapata shida sana. Sijui tuiekeje hii ila kama una mtoto mkubwa anayeweza kutizama wenzake uweke utaratibu wa kumtumia chochote kitu..... Dah inauma na imenigusa sana. Pole kamanda ila mwendo mbele usirudi nyuma.

mimi naona kama jamaa atapata faraja huko aendako ila angefanya utaratibu wa kuwachukua watoto huyo mwanamke anaweza akaharibu future nzima ya hao watoto na kila siku watalalamika juu ya uamuzi wa wazazi wao,..
Watamuona baba kama aliewatelekeza..
 
pole sana.
una upendo hadi nimeogopa
yaani hadu unajamiiana na mtu huku ukijua nii muathirika?
 
Mmh jaman kaka unatia huruma mpaka machozi yamenitoka jamani..mhh najuta y nimefungua hii thread...masikini ondoka tu kaka nenda kaanze maisha yako upya..kuna wanawakee wapo wana upendo wa dhati kabisa Mungu atakujalia..for now nenda kasake maisha ukae vizuri....muache tu watoto atawalea mana ukisema uchukue watoto utasababisha ugomvi au atakuomba msamaha tena utajikuta umejirudi umemsamehe wakat yan ni mtu ambae hasameheki jamani so saaad..polee kaka
 
Pole sana na Mungu awe pamoja na wewe na akupe faraja katika maisha yako yaliyobaki hapa Duniani.
 
Fikiria maisha zaidi na futre ya watoto wako kama Mungu ataona inafaa kukupa mwanamke mwigine atakupa tu na utashau yote. Eeeeh Mungu mbariki mja wako na kila mtu aseme ameeen
 
pamoja na maamuzi uliyochukua, kwa tabia na mienendo ya mkeo kama utamuacha na watoto baadae usimtafte mchawi
 
pole sana.
una upendo hadi nimeogopa
yaani hadu unajamiiana na mtu huku ukijua nii muathirika?

yaaani, upendo huu ni wa ajabu. mungu akutangulie abasi katika kila ufanyalo.
 

umejifikiria wewe zaidi
wanao je?si ungefanya utaratibu
uondoke na watoto?mmmmh haya we!!
 
Asanteni sana wadau. Sasa hivi. ...nitamchukua nitaenda nae lunch. ...hotel flani hivi....kupo kimya sana. Nimemuomba nikafanye nae maongezi ili kesho niondoke. Kakubali.........let love lead. To God be the Groly!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom