FFU ajalini Dar!!

afkombo

Member
Feb 9, 2008
93
11
Sifurahii ajali kutokea lakini nashukuru kwamba wamekutana wenyewe kwa wenyewe sasa sijui nani ni m'babe,shauri zao wenyewe.

FFU Dar ajalini

Gari moja lililosheheni askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) limepata ajali mbaya leo asubuhi na kusababisha kifo cha askari mmoja huku wengine 11 wakijeruhiwa vibaya.

Tukio hilo la kusikitisha, limetokea mishale ya saa 11:45 asubuhi baada ya gari hilo la FFU aina ya Landrover Deffender kuvaana na lori la Jeshi la Wananchi (JWTZ), lenye namba za usajili 5609 JW 08.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Libaratus Sabas, ameliambia Alasiri leo asubuhi kuwa ajali hiyo imetokea katika makutano ya barabara za Chang’ombe, Nyerere na Kawawa.

Akasema askari hao wa FFU walikuwa wakitokea katika kambi yao iliyopo Ukonga Jijini Dar es Salaam na walikuwa wakielekea kwenye malindo mbalimbali ya viongozi.

Akasema nalo lori la jeshi lilikuwa likitokea Chang’ombe kuelekea barabara ya Kawawa.

Akasema dereva wa lori la JWTZ alikuwa peke yake garini na aliligonga gari la FFU ubavuni.

Akasema kuwa hadi sasa, majeruhi wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

"Jina la anayedhaniwa kufa na taarifa nyingine zaidi tutazitoa baadaye," akasema Kamanda Sabas.
CHANZO: ALASIRI
 
Poleni majeruhi mliofikwa na ajali hii. Kama kawaida, miundo mbinu yetu inapaswa kuboreshwa zaidi, taa za barabarani ziongezwe kama sio kuimarishwa, bara bara ziwe bora zaidi na elimu zaidi kwa madereva wetu na watumiaji wa bara bara itolewe, though ajali haina kinga ila zaweza kupunguzwa.
 
Huwa naona magari ya polisi yakipita upande wa kulia kwa kuwa yanakuwa na dharura sasa ajali ikitokea kwenye mazingira haya inakuwaje?
 
Sifurahii ajali kutokea lakini nashukuru kwamba wamekutana wenyewe kwa wenyewe sasa sijui nani ni m'babe,shauri zao wenyewe.

FFU Dar ajalini

Gari moja lililosheheni askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) limepata ajali mbaya leo asubuhi na kusababisha kifo cha askari mmoja huku wengine 11 wakijeruhiwa vibaya.

Tukio hilo la kusikitisha, limetokea mishale ya saa 11:45 asubuhi baada ya gari hilo la FFU aina ya Landrover Deffender kuvaana na lori la Jeshi la Wananchi (JWTZ), lenye namba za usajili 5609 JW 08.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Libaratus Sabas, ameliambia Alasiri leo asubuhi kuwa ajali hiyo imetokea katika makutano ya barabara za Chang’ombe, Nyerere na Kawawa.

Akasema askari hao wa FFU walikuwa wakitokea katika kambi yao iliyopo Ukonga Jijini Dar es Salaam na walikuwa wakielekea kwenye malindo mbalimbali ya viongozi.

Akasema nalo lori la jeshi lilikuwa likitokea Chang’ombe kuelekea barabara ya Kawawa.

Akasema dereva wa lori la JWTZ alikuwa peke yake garini na aliligonga gari la FFU ubavuni.

Akasema kuwa hadi sasa, majeruhi wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

"Jina la anayedhaniwa kufa na taarifa nyingine zaidi tutazitoa baadaye," akasema Kamanda Sabas.
CHANZO: ALASIRI
Binadamu ni kiumbe cha ajabu sana. Yaani kwa vile wamegogana wanajeshi tuu unashukuru mungu?
MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Sifurahii ajali kutokea lakini nashukuru kwamba wamekutana wenyewe kwa wenyewe sasa sijui nani ni m'babe,shauri zao wenyewe.

FFU Dar ajalini

"Jina la anayedhaniwa kufa na taarifa nyingine zaidi tutazitoa baadaye," akasema Kamanda Sabas.
CHANZO: ALASIRI


Hii chuki imezidi sasa!

Afkombo, huna ndugu mjeshi mtuwangu?

May their souls RIP!
 
Poleni majeruhi mliofikwa na ajali hii. Kama kawaida, miundo mbinu yetu inapaswa kuboreshwa zaidi, taa za barabarani ziongezwe kama sio kuimarishwa, bara bara ziwe bora zaidi na elimu zaidi kwa madereva wetu na watumiaji wa bara bara itolewe, though ajali haina kinga ila zaweza kupunguzwa.

Hawa jamaa hata ukiwawekea taa hawajali, si mnakumbuka pale ubungo walivyo mdunda trafiki polisi,

huwa wanajifanya wana haraka kuliko wenzao, sasa hili ni fundisho, siwaonei huruma mimi hata kidogo.
 
Hii chuki imezidi sasa!

Afkombo, huna ndugu mjeshi mtuwangu?

May their souls RIP!

Angalia nimeanza na sentensi gani hapo juu,simaanishi kuwa wanajeshi au askari wao wana haki ya kupata ajali au kufa.Km ajali imeshatokea na haiwezi kurudi nyuma,ila ninachokishukuru mm ni kwamba ajali hiyo imetokea miongoni mwa wenyewe watu wa usalama,kwa sababu najua km ingetokea kati ya Daladala na wanajeshi au mtu binafsi na wanajeshi,hao wanajeshi kwa vyovyote vile wangeanzisha kipigo kwanza then mambo mengine baadae.Narudia tena sikumaanisha"NAFURAHIA" nimemaanisha"NASHUKURU" kwamba hiyo ajali imetokea kati ya wanajeshi wa JWTZ na FFU.
Wapo watu wengi tu huwa wanashukuru mungu baada ya kutokea janga lolote kwa kuwa tu limetokea ktk mazingira fulani ya uafadhali.Kwa mfano watu waliokumbwa na Tetemeko Nchini China mwaka jana walikuwa wanasema"TUNASHUKURU" hili tetemeko limetokea kipindi cha summer na hakuna mvua,walisema hivyo kwa sababu km ingekuwa winter au mvua ingekuwa balaa zaidi kwa sababu watu iliwabidi walale nje kwa muda fulni.
 
Binadamu ni kiumbe cha ajabu sana. Yaani kwa vile wamegogana wanajeshi tuu unashukuru mungu?
MUNGU IBARIKI TANZANIA

Binaadam ana haki ya kushukuru Mungu kwa kilajambo linalomtokea,mimi sikufurahia ila nimeshukuru na nimeshukuru kwa sababu mbili
1:Namshukuru Mungu kwa sababu ni katika imani yangu kushukuru kwa kila analofanya Mungu kwani naamini lolote alifanyalo basi lina manufaa kwa wanaadam either direct au indirect.
2:Namshukuru Mungu hiyo ajali imewahusisha FFU na JWTZ kwa sababu ingehusisha JWTZ na raia au FFU na raia,madhara kwa raia yangekuwa makubwa kwa sababu hawa jamaa huwa wanajichukulia sheria mkononi,hasa JWTZ wao huwa wanapiga watu na hata Askari wa usalama barabarani bila sababu zozote,sasa ingetokea km raia amegonga gari lao na askari wa JWTZ mefariki unafikiri ingekuwaje,wangempiga then sheriai ngekuja baadae.Lkn sidhan km wanaweza kumpiga askari wa FFU.Hicho ndicho nilicho kishukuru.
 
Back
Top Bottom