afkombo
Member
- Feb 9, 2008
- 93
- 11
Sifurahii ajali kutokea lakini nashukuru kwamba wamekutana wenyewe kwa wenyewe sasa sijui nani ni m'babe,shauri zao wenyewe.
FFU Dar ajalini
Gari moja lililosheheni askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) limepata ajali mbaya leo asubuhi na kusababisha kifo cha askari mmoja huku wengine 11 wakijeruhiwa vibaya.
Tukio hilo la kusikitisha, limetokea mishale ya saa 11:45 asubuhi baada ya gari hilo la FFU aina ya Landrover Deffender kuvaana na lori la Jeshi la Wananchi (JWTZ), lenye namba za usajili 5609 JW 08.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Libaratus Sabas, ameliambia Alasiri leo asubuhi kuwa ajali hiyo imetokea katika makutano ya barabara za Changombe, Nyerere na Kawawa.
Akasema askari hao wa FFU walikuwa wakitokea katika kambi yao iliyopo Ukonga Jijini Dar es Salaam na walikuwa wakielekea kwenye malindo mbalimbali ya viongozi.
Akasema nalo lori la jeshi lilikuwa likitokea Changombe kuelekea barabara ya Kawawa.
Akasema dereva wa lori la JWTZ alikuwa peke yake garini na aliligonga gari la FFU ubavuni.
Akasema kuwa hadi sasa, majeruhi wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
"Jina la anayedhaniwa kufa na taarifa nyingine zaidi tutazitoa baadaye," akasema Kamanda Sabas.
CHANZO: ALASIRI
FFU Dar ajalini
Gari moja lililosheheni askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) limepata ajali mbaya leo asubuhi na kusababisha kifo cha askari mmoja huku wengine 11 wakijeruhiwa vibaya.
Tukio hilo la kusikitisha, limetokea mishale ya saa 11:45 asubuhi baada ya gari hilo la FFU aina ya Landrover Deffender kuvaana na lori la Jeshi la Wananchi (JWTZ), lenye namba za usajili 5609 JW 08.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Libaratus Sabas, ameliambia Alasiri leo asubuhi kuwa ajali hiyo imetokea katika makutano ya barabara za Changombe, Nyerere na Kawawa.
Akasema askari hao wa FFU walikuwa wakitokea katika kambi yao iliyopo Ukonga Jijini Dar es Salaam na walikuwa wakielekea kwenye malindo mbalimbali ya viongozi.
Akasema nalo lori la jeshi lilikuwa likitokea Changombe kuelekea barabara ya Kawawa.
Akasema dereva wa lori la JWTZ alikuwa peke yake garini na aliligonga gari la FFU ubavuni.
Akasema kuwa hadi sasa, majeruhi wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
"Jina la anayedhaniwa kufa na taarifa nyingine zaidi tutazitoa baadaye," akasema Kamanda Sabas.
CHANZO: ALASIRI