Felix Mkosamali (Case study)

Felix Mkosamali (Case study)

H20

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2013
Posts
341
Reaction score
170
1667.jpg

Felix Francis Mkosamali, Mbunge wa Jimbo la Muhambwe kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, ni mbunge mdogo wa Jimbo katika Bunge la sasa, ambapo ana miaka 27.

Mwanasheria Msomi kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kilichopo jijini Mwanza.

Kijana huyu mbunge aliweza kugombea na kupata jimbo la Muhambwe kwa kutumia fedha alizokopeshwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kumsaidia kuzunguka huku na kule ili kuwafikia wapiga kura. Pia

fedha nyingine zilizomsaidia wakati wa harakati za kampeni alizipata kwa kufundisha katika shule ya sekondari ya wasichana Boniconcili, ambapo alikuwa mwalimu wa muda (Part Time).
Pamoja na kuingia bungeni kwa taabu kijana huyu tunamwona kila siku anavyojitahidi kuisimamia serikali bila woga kwa kuchangia hoja zenye mashiko na kuonesha upeo wa kisomi katika uchangiaji hoja kwa nidhamu ya hali ya juu.
Somo (case study) kwa vijana kutoka kwa Mkosamali :

1. Siku zote penye nia pana njia. Pamoja na kidogo ukipatacho ukiwa na nidhamu na malengo dunduliza utimize
malengo yako. Kwani haba na haba hujaza kibaba.
2. Acha maisha tegemezi na uangalie fursa ulizo nazo uzitumie ili kutimiza malengo yako. i.e kama una kipaji
chochote jitahidi kukifanyia kazi na usibweteke
3. Woga ni dhambi kubwa sana, siku zote usitishwe na kitu chochote unapokuwa umesimamia ukweli, jidhihirishe wazi
nia yako na tetea haki yako bila kusaliti wenzio. Kumbuka kuwa mzalendo na kuitetea nchi yako kwani vijana ndio
watakaoleta mabadiliko katika nchi yetu. Naomba kuwakilisha.
 
Kijana ana hoja kali sanaaaaaaaa zenye mashiko...

Na rafudhi yake mpaka raha kumsikia.
 
Hao ndio twawahitaji kwenye bunge letu na nchi yetu kwa ajili ya maendeleo. Twataka watu wanaoTHUBUTU
 
... Sijawahi kumsikia sana; lakini JINA lake sio geni Ina Maana lipo na linasikika na ni IMARA; na Sehemu Pekee ambayo Mimi ningeweza kulisikia Jina MKOSAMALI a UNIQUE but FAMOUS ni BUNGENI...

Bravo... More Power 2 you... As you know
Destiny is not a matter of chance, it is a matter of choice; It is not a thing to be waited for, it is a thing to be achieved."
 
Zambi kubwa kuliko zote ni uoga na ukiwa na uoga hata mungu ukaa mbali nawe jithd kaka tupo pamoja
 
FELIX MKOSAMALI, ZITO KABWE, MOSES MACHALI, DAVID KAFULILA wabunge vijana kutoka mkoa wa kigoma, mikoa mingine igeni mfano wa wapiga kura wa kigoma kuwaamini vijana.
 
Usisahau pia kuwa mafanikio yake Kisiasa yametokana sana na juhudi na msaada mkubwa sana kutoka kwa Zitto Kabwe wakati wa uchaguzi wa 2010.
 
Ameingia bungeni akiwa 24 safi sana mkosamali cdm imejenga watu vizuri.
 
Namkubali sana huyu kijana hasa pale alipowachana mawaziri
 
Tatizo la huyu ni kila anapotaka kujenga hoja kujitapa kuwa alipata Div. I ya digrii ya sheria! Namkumbusha kuwa Div.I aliyopata isiwe nguvu ya hoja ya kutaka mawazo yake yakubaliwe!

Kuna wengi ambao wahakufanikiwa kupata Div. I au kuwa na elimu ya chini kuliko yake lakini wanajenga hoja za nguvu katika kutetea wananchi wao na maslahi ya Taifa!
 
Yaani siku alipoongea hivyo nilicheka mpaka basi, eti wapo wapo tuuu, wanakaaa tuuu, wanafanya nini???? Anaongea kama ana dharau fulani hivi ila anafikisha ujumbe haswa. kusema ukweli akianza kuongeaa uwa nakuwa makini kumsiliza.

Wanakaakaa tuuuu yaani wapowapo tuu
 
Back
Top Bottom