Mwana Kwetu
JF-Expert Member
- Jul 12, 2011
- 652
- 607
Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Ndg Mramba juzi alijitetea alipoulizwa kwa nini umeme ulikatika wakati Lowassa akitangazwa Live na ITV.
Alisema hajihusishi na siasa na pili kukatika kwa umeme kumesababishwa na matengenezo.
Mimi concern yangu ni uongo aliosema kuwa kukatika kwa umeme kutokana na matengenezo. Ninachotaka kieleweke wazi ni kuwa kunamgao wa umeme haswa hapa ARUSHA na ushahidi upo ila kwa sababu walishasema nchi hii hautakuwepo mgawo tena wanasingizia matengenezo.
Uzoefu unaonyesha kuwa matengenezo hufanyika hadi saa 12 au saa 1 jioni lakini kwa hapa Arusha umeme unakatika kwa zamu. Siku tatu unakatika mchana kutwa na siku tatu usiku.
Je kuna matengenezo gani yanafanyika usiku kama sio kudanganya. Kama siyo kudanganya matengenezo gani yanasababisha umeme kukatika zaidi ya mwezi mzima bila taarifa?
Kama kweli ni matengezo kwa mfano hapa Arusha atueleze yanafanyika wapi na kwa nini umeme unakatika hadi usiku ina maana TANESCO wanafanya kazi 24 hrs.
Mateso ni ya zaidi ya mwezi kwa hapa Arusha mjini na vitongoji vyake kwani kwa uzoefu wangu hali kama hii haijawahi tokea ambapo umeme unakatika kwa masaa 10 kwa zaidi ya mwezi sasa bila kuwepo taarifa zozote.
Alisema hajihusishi na siasa na pili kukatika kwa umeme kumesababishwa na matengenezo.
Mimi concern yangu ni uongo aliosema kuwa kukatika kwa umeme kutokana na matengenezo. Ninachotaka kieleweke wazi ni kuwa kunamgao wa umeme haswa hapa ARUSHA na ushahidi upo ila kwa sababu walishasema nchi hii hautakuwepo mgawo tena wanasingizia matengenezo.
Uzoefu unaonyesha kuwa matengenezo hufanyika hadi saa 12 au saa 1 jioni lakini kwa hapa Arusha umeme unakatika kwa zamu. Siku tatu unakatika mchana kutwa na siku tatu usiku.
Je kuna matengenezo gani yanafanyika usiku kama sio kudanganya. Kama siyo kudanganya matengenezo gani yanasababisha umeme kukatika zaidi ya mwezi mzima bila taarifa?
Kama kweli ni matengezo kwa mfano hapa Arusha atueleze yanafanyika wapi na kwa nini umeme unakatika hadi usiku ina maana TANESCO wanafanya kazi 24 hrs.
Mateso ni ya zaidi ya mwezi kwa hapa Arusha mjini na vitongoji vyake kwani kwa uzoefu wangu hali kama hii haijawahi tokea ambapo umeme unakatika kwa masaa 10 kwa zaidi ya mwezi sasa bila kuwepo taarifa zozote.