Fedha iliyo chafu ni hatari kwa afya

Fedha iliyo chafu ni hatari kwa afya

mwengeso

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2014
Posts
9,286
Reaction score
6,727
Nimeona na kusoma habari yenye kichwa hapo juu, kutoka gazeti la Mtanzania, Jumanne Septemba 20, 2016, nikashindwa kujizuia kutokuileta humu JF ikizingatiwa wengi wetu humu hupenda stori za watu na matukio. Ushahidi wake ni jinsi mada za aina hiyo zinavyochangiwa na wengi.

Habari yenyewe inasema kwamba wataalamu wa afya wanatahadharisha kuwa mzunguko wa fedha ni hatari kwa afya ya binadamu, hasa noti ndogo ndogo kama za shilingi 500, na sarafu za 100 au 200 kwa kuwa zinapita kwenye mikono ya watu wengi.

Watu wengi hupokea chenji na kuiweka mfukoni kienyeji, kufunga kwenye upande wa kanga, nguo za ndani (km sidiria, soksi, na chupi). Haijalishi zimetoka kwa nani, awe muuza nyama buchani, mkaa, chips, mwendesha bodaboda, kondakta wa gari la abiria, mama nitilie, mmachinga, nk.

Fedha ni chafu kiafya kwa kuwa zinabeba bacteria ambao hawaonekani kwa macho. Hivyo baadhi ya magonjwa ya tumbo (kuharisha na harahara)na mengine ya ngozi, hayaletwi kwa kula chakula cha sumu (food poising) bali kwa kuwa ulipokea pesa chafu na hukuchukua tahadhari ya kusafisha mikono yako kabla ya kushika chakula na kukiweka mdomoni.

TUCHUKUE TAHADHARI NA JINSI YA KUSHIKA NA KUTUNZA FEDHA.

Fedha iwekwe kwenye pochi muda wote na siyo mfukoni au kwenye nguo za ndani ya mwili.
 
Nimeona na kusoma habari yenye kichwa hapo juu, kutoka gazeti la Mtanzania, Jumanne Septemba 20, 2016, nikashindwa kujizuia kutokuileta humu JF ikizingatiwa wengi wetu humu hupenda stori za watu na matukio. Ushahidi wake ni jinsi mada za aina hiyo zinavyochangiwa na wengi.

Habari yenyewe inasema kwamba wataalamu wa afya wanatahadharisha kuwa mzunguko wa fedha ni hatari kwa afya ya binadamu, hasa noti ndogo ndogo kama za shilingi 500, na sarafu za 100 au 200 kwa kuwa zinapita kwenye mikono ya watu wengi.

Watu wengi hupokea chenji na kuiweka mfukoni kienyeji, kufunga kwenye upande wa kanga, nguo za ndani (km sidiria, soksi, na chupi). Haijalishi zimetoka kwa nani, awe muuza nyama buchani, mkaa, chips, mwendesha bodaboda, kondakta wa gari la abiria, mama nitilie, mmachinga, nk.

Fedha ni chafu kiafya kwa kuwa zinabeba bacteria ambao hawaonekani kwa macho. Hivyo baadhi ya magonjwa ya tumbo (kuharisha na harahara)na mengine ya ngozi, hayaletwi kwa kula chakula cha sumu (food poising) bali kwa kuwa ulipokea pesa chafu na hukuchukua tahadhari ya kusafisha mikono yako kabla ya kushika chakula na kukiweka mdomoni.

TUCHUKUE TAHADHARI NA JINSI YA KUSHIKA NA KUTUNZA FEDHA.

Fedha iwekwe kwenye pochi muda wote na siyo mfukoni au kwenye nguo za ndani ya mwili.
Yaani ni kweli kabisa unakuta mtu analamba kidole ndio ahesabu hela kumbe analamba uchafu mtupu
 
Yaani ni kweli kabisa unakuta mtu analamba kidole ndio ahesabu hela kumbe analamba uchafu mtupu

Wengine wanakusanya noti na kuzibana mdomoni huku akiendekea na shughuli zake. Ni vidudu vingapi anaingiza mwilini!
 
binafsi huwa siwezi kula chochote kwa kutumia mkono bila kunawa hasa ninapokumbuka kuwa nilishika pesa hasa noti... au siti za magari hasa public cars, vitasa vya milango ya maofisi mbalimbali, hata simu.. . hivi vitu huwa naona ni vichafu sana japo hakuna namna ya kuepuka kuvishika.
 
Hao ndo watafiti wa bongo ,,,baada ya kufanya utafiti kwamba majani ya mwembe ni mboga yafaa kuliwa INA vitamini ili kuwapunguzia watu garama za maisha!!!!! Wanasema uchafu was hela looo?????? Mungu awape roho ya ufunuo wasomi wetu
 
WE ENDELEA KULAMBA HIZO FEDHA

OVA
Hao ndo watafiti wa bongo ,,,baada ya kufanya utafiti kwamba majani ya mwembe ni mboga yafaa kuliwa INA vitamini ili kuwapunguzia watu garama za maisha!!!!! Wanasema uchafu was hela looo?????? Mungu awape roho ya ufunuo wasomi wetu
 
Nakumbuka nilipo kuwa mdogo nifundishwa kutoweka ela mdomon, asante sana mama CU
 
Back
Top Bottom