Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,991
Kwa mawazo yako, na inabaki kwenye mawazo yako tu, ila ni kisingizio tu, kwamba "kutenda haki na kufuata sheria ni jambo lenye gharama kubwa na liltaleta madhara makubwa kwa taifa na wananchi wote kwa ujumla" hiki ni kichekesho cha mwaka! Unasema "haina madhara kwa sababu wananchi wameuzoea mfumo huu wa sasa" kichekesho kingine. kwa kuwa jambo baya limekuwa likifanyika muda mrefu, basi liendelee kwa kuwa "watu wamelizoea"?Mwanasheria mkuu wa serikali amekata rufaa kwa sababu utekelezaji wa hukumu hiyo ndani ya kipindi kifupi haitawezekana bila kuleta madhara makubwa kwa taifa na wananchi wote kwa jumla. Mfumo wa Tume ya Uchaguzi hauwezi kubadilishwa ndani ya muda mfupi. Inahitaji maandalizi thabiti hususani ya kibajeti na kubadilisha sheria zetu. Ili kubadili mfumo huu mara moja mwananchi atapaswa kutozwa kodi zaidi za kuwezesha kuanzisha na kuendesha mfumo huo mpya. Haya ndiyo madhara ya kutekeleza hukumu hiyo mara moja......Hii ya Fatuma /Wangwe vs AG, great thinkers hawadhani kama itafanikiwa.
Unajua gharama za kuhamishia makao makuu Dodoma kwa mwendokasi alivyofanya magufuli? unajua gharama za kufanya chaguzi za marudio kutokana na wabunge "wanaoguswa na utendaji wa JPM"? haya yote ni "halali", ila "haramu" ni kuingia gharama kwa ajili ya jambo halali la utendaji haki na kufuata katiba na sheria zetu?
Kwa hakika, ninavyoifahamu serikali hii ya awamu ya 5, inaweza kabisa ku-ignore maamuzi ya mahakama. si mara ya kwanza na si ya mwisho. mbona wananchi waliobomolewa kimara walishinda kesi na bado wakabomolewa nyumba zao?
Kwa jinsi Magufuli alivyowekeza katika kuwategemea wakurugenzi "kumbeba", sidhani kama atakuwa na plan B, na kwa hiyo atakomaa nao iwe isiwe.