Alloyce PR
JF-Expert Member
- Nov 15, 2020
- 590
- 706
"Pale ambapo taifa linashuhudia kuibuka kwa wanasiasa na viongozi wa dini wenye hulka ya kuropoka, kueneza uongo, na kuchochea hisia bila mantiki, huo ni uthibitisho wa kuwepo kwa changamoto ya afya ya akili katika jamii. Endapo hali hii haitadhibitiwa kwa maarifa na maamuzi magumu, ipo hatari kwamba siku moja wataamrisha waumini kuchinjana, na kwa upofu wa kiimani au ufuasi, wengi wataitii amri hiyo bila hata kuhoji uhalali wake. Huu si udhaifu wa mtu mmoja, bali ni ishara ya kuzorota kwa uwezo wa kijamii wa kutafakari, kupambanua, na kuchukua msimamo wa kimaadili." — Alloyce, P.R.