mjapanimweusi
Member
- Feb 11, 2019
- 26
- 11
- Thread starter
- #21
Hapo kwenye "Kuunda" hapo.
Ni combination ya IT,NETWORK,ELECTRONICS pamoja na AUTO ELECTRICAL.
System zetu siyo plug and play,ni designed kuanzia katika coding,na wiring system yake.
Mfano ukiagiza tracking nje ya nchi ufungiwe tracking device hyo inakua na model yake mfano MODEL NUMBER PGO2c-310.
Ikifika kwako inakuja na manual yake ww kazi yako ni kufunga na unadownload software yake harafu umemaliza kitu hewani.
Sasa wezi na majambazi nao ni wasomi,kwa kawaida gari iliyofungwa GPS sysem hua ina act kama receiver na transmitter.
Kama mwiz wa gari akiwa na kifaa kinacho track uwepo wa tracking system ktk gari yako,ni rahisi kujua model ya tracking system yako unayo tumia,na akisha ijua model ya tracking sysem yako umeumia!
Wana kifaa ambacho kinaitwa tracking system jammer,wanafeed tu model ya tracking system yako katika jammer yao,kwa bahatimbaya model namba ya tracking system yako ikiwa katika list zao ujue wanauwezo wa aina mbili.
1.kucheat location kupitia gps yako,yani kwenye system mnaweza kuona gari iko Morogoro kumbe gari ipo Mwanza.
2.Kufanya jamming ya track sysem yako,wanauwezo wa kuifanya tracking system yako isionekane kwenye system.unakuta ktk database unaona last updates ya information ni pale tu gari,ilipo ibiwa baada ya hapo kimyaaaa!
Hivyo tunavyo sema tunaunda,ni kwamba model zetu ni unique,hazipo katka global market,hvyo kwenye vifaa vya kujamm au kucheat huwez kuiona model,labda uanze kufumua fumua gari utafute wapi tumeficha black box,uanze kukatakata waya,na muda huo wez hawana.
Na ukumbuke hata kujamm system zako wanafanya kabla hawajalichukua,ukiona gari yenye trackng imechukuliwa ujue wamesha fanya yao ki-IT zaidi


