Fahamu fursa za kilimo cha Nyoka

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,007
9,873
FURSA YA KILIMO CHA NYOKA
Kilimo cha nyoka ni moja ya kilimo chenye faida sana ,mmoja anaweza akaanzisha kilimo hichi ukizingatia thamani ya "snake venom" ipo juu sana.Sumu ya nyoka inatumika kwa wingi kwenye viwanda vya famasia na viwanda vya vipodozi hivyo thamani ya "snake venom " ipo juu sana kutokana na uhitaji wake.

1601287102566.png

Gram moja ya "snake venom " kwa soko la kimataifa inauzwa $1880 ,na kwenye soko la Afrika kusini inauzwa kwa makadirio ya Rand 25,000
*Kama unafikiria kuanzisha shamba lako la nyoka ,yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia ili uweze kupata faida ya kutosha kutokana na venom wanayozalisha Nyoka
1.Zingatia hali ya joto na hewa .

Nyoka wanahitaji joto ya kiwango cha 24-29 degrees Celsius nyakati ya siku na 21-24 nyakati za usiku.
2.Mabanda na nyumba za nyoka zinahitaji kusafishwa mara kwa Mara

Hali hiyo itasaidia kukuza uzalishaji wa nyoka kwa wingi.Nyoka wanahitaji kuwekwa mahali salama kuzuia matatizo yeyote ile ya kiafya kuwapata.

3. Nyoka kwa kawaida hula panya 3-4 na hulishwa kwa wiki 3-4 .Nyoka hula panya walio hai lakini wanaweza kula waliokufa pia ,Nyoka hupenda kucheza na panya mwanzo kabla ya kuwala hivyo ni vema kuwapatia walio hai.

Faida za ufugaji wa nyoka
1. Uzalishaji wa venom ambayo ukiuza unapata kiasi kikubwa cha pesa.
2. Hupunguza na kutokomeza wadudu waharibifu kama panya nk. Nyoka chakula chao kikuu ni panya hivyo husaidia kutusafishia shamba au nyumba kwa kuwamaliza wadudu hawa.

**Mwisho nawashauri ndugu zangu sio kila tukiwaona nyoka tunawaua ,nyoka ni rafiki zetu na sio maadui. Tuwatumie ipasavyo watatusaidia sana

1601287243420.png
 
Hivi ile dhana ya kuwa Nyoka wanakula unga ni ya kweli jamani...... hii kazi ya kufuga nyoka wanaweza wachina na Banian
 
Mtoa mada kuna watu mwaka huu tumepanga kuwa serious sasa naona unatukwamisha mepemaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom