Experience: Wanawake WASIO na uvungu mguuni

Experience: Wanawake WASIO na uvungu mguuni

DeepPond

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2017
Posts
43,313
Reaction score
109,381
Umewai kusikia Nini kuhusu mahusiano na mwanamke asiye na uvungu mguuni (chini ya unyayo.

CHANZO CHA KULETA HII MADA ni hiki,
Kuna jamaa yangu jana nilimsindikiza hospital kumwona Kwa mama yake mzazi alilazwa.

Njiani tumekutana na mwanamke wake (Wana mahusiano Ila sio rasmi) anatoka kazini akatupiga mkono, jamaa aKaona sio mbaya tuongozane nae mpk hospital.

Kule hospital yule Binti akawa anajitahidi sn kumchangamkia mama WA watu, kuangalia faili lake, KUULIZA Kwa madokta na manesi wanaoingia maendeleo yake na Kama Kila kitu wodini pale kinakwenda sawa. (Yule binti kumbe Ni daktari by profession).

Kuna mda Binti ametoka nje kwenda kumfuatia matunda flani mama WA watu ili yamsaidie kwenye Afya yake.

Yule mama akamuuliza mwanae mbele yangu, kua yule Binti ni nani, mbona hatambulishwi? Jamaa akamjibu straight kua ni mchumba wake japo Bado haijawa rasmi. Ila Anatarajia kumrasimisha Kisha kumuoa awe mkewe wa ndoa.

Yule mama hakupepesa akamwambia jamaa,
"Sawa Kama mmeshapendana, Ila Mimi sioni Kama una mke pale"

Jamaa akauliza,
"Kivipi sasa mama angu, Leo Leo Tu ndo umemuona na tayari ushahitimisha kua hamna MKE apa!"

Yule mama akamjibu,
"Kwani humuoni kua mguuni Hana uvungu yule?"

Hayo majadiliano hayakuendelea tena maana ghafla mlango ulifunguliwa, nesi aliingia kumbadilishia dripu na sio MDA yule Binti nae alirejea wodini na Yale matunda aliyoyafata,

story nyingine zikaendelea na MDA ulivoisha, wote tukaondoka wodini Kwa pamoja kutoka pale hospitali, wamenishusha dukan kwangu, wao wameendelea na safari zao.

Jioni nmempigia jamaa namuulza vipi khs suala lile la yule bi.mkubwa wake kuhusiana na uvungu mguuni mwa mwanamke wake.

Jamaa akasema "mambo ya mila hayo kaka, kwetu wanaamini mwanamke asiye na uvungu mguuni ana mkosi, kua nae kimahusiano hawezi kua mke Bora"

Nilipoomba ufafanuzi zaidi, jamaaa akasema
"wazee wanaamini wanawake WA hivyo wameumbwa abnormal, na akili zao ziko kushoto Sana, mahusiano nao ni changamoto Sana, migogoro Kila kukicha"

Jamaa akaongezea,
"Zaman Tokea tuko watoto tumekua tunafundishwa na tukatazwa Hilo. kuna Mjomba wetu mmoja alikaidi akamuoa mke WA hivyo Ila walisumbuana sana Hadi mjomba wetu akajinyonga tukamzika, Mali zote zilipotea kusikojulikana, mwanamke yule aliuza Bei ya kutupa na akapotea kusikojulikana na watoto WA marehemu mjomba wetu, tumekua hatujui wako wapi na wao Hawana mawasiliano na ukoo wetu kabisa".

"Kwaiyo Kwa wazee kwetu imekua Kama reference kwenye ukoo, Ila mi sijali Sana, nnachoangalia Ni tabia ya mtu mwenyewe binafsi. Maisha yamebadilika Sana"

Nikamuuliza jamaa,
"kwani wee unamuonaje mwanamke wako ukilinganisha na hayo ulikuwa umekua unaambiwa, kufundishwa na kuonywa na wazee wako Tokea uko kwenu"

Jamaa akajiibu,
"Hatuna MDA mrefu sana kimahusiano kumjua zaidi (4months) ilaTukishindwana tutaachana TU, sijazaliiwa nae tumbo Moja yule mwanamke"

Nkamjibu "sawa" Kisha tukaendelea na story zetu nyingine.

Sasa Kuna MDA nmekaa peke angu, nikawaza Sana maneno ya yule bibi (mama aKe jamaa) kule hospitali, pia story alizonipa uyu jamaa, nikaona Kama Kuna kitu hakiko sawa kwenye mahusiano yangu na mtu wangu.

KIUKWELI nna mwanamke wangu mmoja nae Hana uvungu mguuni Kama uyu mchumba WA jamaa, aisee huyu mwanamke ni pasua kichwa balaa.

Yaan ukiskia kua na mwanamke mwenye akili zilizo kushoto, Basi huyu WA kwangu mamaJ,Ile ni namba nyingine kabisa.

Kuna mda haeleweki anataka Nini kwenye mahusiano, Kuna MDA alikua ananivuruga kichwa Hadi nashindwa kufanya baadhi ya Kazi zangu. Nowdays nashkuru nmemzoea sana na Nmeamua kumpuuza.

Ilifikia kipind nikasema humu, hata bahati mbaya wife amefariki au tumeachana, mamaJ atabaki kua mchepuko wangu forever, ntaingia mtaani upya kusaka MKE mwingine mwenye sifa WA kuoa.

Sio jambo zuri kulitamka mbele ya watu, Ila Kwa ustawi wangu,Afya yangu na maisha yangu, ni jambo jema sn nikajiandaa nalo kisaikolojia ili nisije kufa kubaki historia nikaacha wanangu wadogo wanateseka na hii dunia (Kama marehemu mjomba wake na jamaa) bila msaada wowote.

Sasa Wana jf,
Plz Waliowahi kuliskia hili la uvungu mguuni, wenye experience nalo kwenye maisha yao,

Au wenye wanawake WASIO na uvungu mguuni, leteni ushuhuda, uko upande WENU Hali ikoje.

Madaktari nanyi mnambie uvungu mguuni unauhusiano vipi kimahusiano na akili au socialization ya mtu, Kwanini wengine wanao, wengine Hawana.

Nawasilisha wakuu🙏
 
Hata jeshini hawapokei kuruta asiye na uvungu wa mguu. The reason behind wanasema mtu asiye na uvungu wa mguu akisimama mishipa ya damu ya unyayo inakandamizwa na sakafu/ kiatu hivyo damu haitakuwa na mzunguko mzuri.

Damu isipokuwa na mzunguko mzuri manake haitafika kwa wingi Sehemu za juu za mwili ikiwemo ubongo hivyo humsababishia mtu huyo kukosa focus katika mafunzo au wakati mwingine kuanguka ghafla endapo atasimama muda mrefu.
 
 
Watu wenye Flat foot!
 

Attachments

  • images (3).jpeg
    images (3).jpeg
    12.7 KB · Views: 35
Back
Top Bottom