William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,466
Raisi akizungumzia neno misaada!, watu mnakuja juu, akichukua hatua ili kujikwamua kwa kujitegemea, watu mnakuja juu, ningekuwa mimi Kikwete kwa hoja zenu hizi dhaifu ningewacheka halafu kimoyomoyo ningejisemea "these people dont know what they are talking about".
kaalika nchi chache, lakini nchi nyingine zenye uchumi mzuri kidogo kuliko sisi
zinawania kushiriki hamuoni kuwa hili ni jambo positive.
Acheni hoja za Chuki, na msifuate mkumbo, kuweni huru wa fikra siyo kila kitu mnalaumu tu, Hili la kikao ni muhimu sana, kwa sababu hizi nchi za jirani tunafanya nazo biashara kwa hiyo ni lazima mipango isukwe kuona tunajiokoa vipi kutoka katika hili tatizo la economic crisis iliyoikumba dunia.
DOWN WITH ARROGANTS, HATERS, WHINNERS, THUMBS UP FOR TRUTH SEEKERS AND POSITIVE CONTRIBUTORS
I do not get it! If Tanzania can get Dollars 400million to contribute to the group, why don't it go alone and work out projects which are pending in Tanzania? These countries are among the poorest and have the same level of development, what value will they add to each other; why an individual country not take issues alone? Why all this bureaucracy?
Guys, guys, guys! Do not get carried away with Mzee Mwanakijiji's fantasy!
This is one of Mwanakijiji's personal view on issues of the moment, and being a good writer, he has gone ahead and put forward one of his own fantasy to JF to discuss. All y'all are currently discussing a phantom - hakuna kitu hapo nyie, ohooooo!!!
Wanabodi,
Kusema kweli inabidi tuzame zaidi ktk kufikiria hili na wala sii non issue kabisa..Hali ya chumi duniani ni mbaya na tupende tusipende kuna kimbunga kinakuja..
Tatizo la wazo zima la Mkutano huu wa G5 ambazo ni nchi maskini kuliko zote dunani, una chemsha bongo zangu kujaribu kufahamu watazungumzia kitu gani..
Pengine JK anataka kuwauliza Kenya na Uganda waliweza vipi kupita kipindi kigumu cha mwaka 1982 ingawa sababu za recession hizi mbili hazifanani?
Pili, laukama kuna nchi tajiri zitaalikwa ktk mazungumzo hayo na tumika baadhi ya mazungumzo ya IMF ktk kujitangaza labda inaweza kusaidia, lakini sisi maskini kukutana wakati hatuna ndururu mfukoni, kula yetu shida, kila mtu anatazama tumbo lake na kusubiri nani ata cover the bill ni kujitafutia matatizo tu..
Kama walivyosema wanabodi wengine huko nyuma,
Ni muhimu kwa Tanzania leo hii kutazama matatizo yetu na jinsi gani tumejiandaa sisi wenyewe kabla ya kuwakilisha hoja nzima..Kenya haiwezi kutusaidia wala hakuna maandalizi yoyote yanayoweza kufanywa na nchi zetu kwa pamoja ktk ku create ajira ambazo zinapotea kwa kasi kubwa..Chumi zam nchi tajiri zinamilikiwa na watu wachache sana lakini wanaozalisha ni zaidi ya asilimia 95..Hivyo kukosekana kwa kazi ni pigo kubwa sana ktk uchumi wao, mzunguko wa fedha ktk asilimia hiyo 95 ukiyumba tu basi nchi hizo huteteleka kiuchumi, wakati sisi wamiliki wa mali zetu ni wageni na wafanyakazi ni aslimia chini ya 50 miaka nenda miaka rudi.. As a fact, serikali (huduma) zetu zinaajiri over 60 ya ajira zote za kila nchi..Tutazalisha wapi na lini?..Mungu ndiye anajua.
Haya ndio maswali ya kujiuliza sisi wenyewe na kuutazama mzungumko mzima kwa kila nchi..kila nchi ni lazima itazame mzunguko wake unaanzia wapi na kukwazwa wapi ili kupata kuelewa wapi utakapo anzia..laa sivyo ni kujaribu kuunganisha mizunguko mitano ya Olyimpic rings in a real world!.. kweli tunaweza au mazingaombwe yenyewe hayo!
Leo hii mkutano wa G5 hata kama ni kuvutia nchi tajiri ktk Utalii au uwekezaji tutafanya nini kwa pamoja ilkiwa hatuna ushirikiano toka mwanzo..kila nchi inajiendesha kivyake tena tunagombania wateja na sii ruksa wala rahisi kwa shirika la Kenya kufanya biashara Tanzania..Utafikiria maskini ombaomba pale msikitini wa Ujumaa baada ya sala..
Soko la mali zetu limeporomoka kutokana na ughali wa maisha nchini..Pamoja na umaskini wetu mali zinazotengenezwa nchini ni ghali mara 10 ya ile inayotoka China, Taiwan na India..Sisi tumekuwa Obsessed na mali za nje kiasi tumetupa hata majembe..tuna consume 90 % ya junk products..mpango ni misheni town tu, mikataba feki, kusaka madini, kununua mitumba hata chakula na madawa leo tunaagiza toka nje tena feki..toka mchele hadi chunvi tunaagiza toka nje ya Uvinza haifai tena..Sii Kenya wala Tanzania sote ni importers wakubwa toka tunaamka asubuhi hadi tunalala usiku asilimia 80 ya matumizi yetu ni mali toka nje..sasa hapa tutajadiliana kitu gani ikiwa sisi ndio soko la mali mbovu na kwa kiasi tumechangia kupandisha bei za mali nyingi za nje kinyume cha actual value ya vitu hivyo.
Kama walivyosema wengine mikutano kama hii kwa wakati huu haina manufaa hata kidogo. Ni muhimu tutafute mbinu za kuinua upya uchumi wetu ktk sekta ambazo tunafahamu zinaongeza kazi na mavuno yake yatakuwa na manufaa kwetu baadaye..NGUVU za UMEME, MAJI, KILIMO cha Umwagiliaji, UFUGAJI, UVUVI, UTALII wa kisasa na mikataba ya Madini ni sehemu ambazo zinatakiwa kupewa nafasi ya kwanza ktk mazungumzo yetu ya ndani..
Nadhani kubwa ni uamuzi wa sisi wenyewe kuamua kujenga nchi tunazozitaka, kuunganisha resources, kushirikiana uwajibikaji na kwa kufanya hivyo kufungua the nuclear-like potential ya watu wetu. Wenzetu mara zote wamekuwa wakifanya mambo kwa pamoja and that is the whole point ya G20.
Leo hii makampuni ya GM na Chrysler yanashughulikiwa matatizo yao siyo Marekani tu bali Canada na Ulaya vile vile. Wenzetu wametambua kuwa ni kwa kuunganisha nguvu zao ndiyo wanaweza kukabili wimbi hili la uchumi mbovu linaloendelea.
Kwetu sisi cha kushangaza ni kuwa wenyewe hatujafanya juhudi za Afrika kutatua matatizo yao wenyewe. Siku tukiweza kutegemea soko la ndani kwa karibu asilimia 70 ya bidhaa zetu zote, ndipo kwa mara ya kwanza tutaona nguvu kubwa ya kiuchumi tuliyonayo.
Fikiria makamapuni ya simu kwa mfano, haya kwa kiasi kikubwa yanatumia walaji wa ndani kwa bidhaa yao na tunaona jinsi gani wanajitengenezea utajiri kutoka ndani. Utajiri ambao kiukweli kabisa ni wa kinyonyaji kwani yanayofanywa na makampuni hayo yanaweza yasifanyike mahali popote duniani!
Sasa, endapo mkutano huu utafanyika hata kwa ajenga zaidi ya hizo tulizodokezwa lakini ukaonesha nia ya watu wa Afrika ya Mashariki kuunganisha nguvu zao katika kukabilia matatizo yao ya kiuchumi badala ya kuacha mambo yatokee kwa nasibu tutakuwa tumeanza kuelekea kwenye uhuru wa kweli.
Hofu yangu ni kuwa watawala wetu hawana mawazo hayo kwani wao kuendelea bila misaada ya kigeni hakuwezekani. Ukiondoa Kagame hakuna RAis mwingine wa Afrika ya Mashariki ambaye anaweza kufikiria njia mbadala ya kupata kipato, mfumo mzuri wa udhibiti wa kodi na mapato, na uboreshwaji wa utawala wa sheria ili kuhakikisha kuwa misaada ya kigeni kwenye bajeti zetu inakoma, na badala yake nchi zetu ziweze kuhudumia bajeti zao kwa asilimia 100 kutokana na mapato yao ya ndani. Wazo hili kwao haliwezekani kwani kile linapotolewa hoja yao inakuwa "misaada inahitajika kwa maendeleo". TAtizo ni kuwa baadhi (kama siyo mingi zaidi) ya misaada hii ni misaada ya kijinga!
Misaada ya kujenga kisima cha maji, choo cha shule, cliniki ya kuhudumia watu 1000 ni misaada ambayo inadekeza watawala, inabutisha ubunifu, na inachochea utegemezi.
"Viongozi wametambua kuwa hawawezi kusubiri nchi wafadhili kuja na mipango ya kuokoa nchi za Kiafrika kiuchumi wakati wao viongozi wa Taifa wana uwezo wa kufanya mambo kadha wa kadha kwa juhudi zao wenyewe" amesema mdokezaji wetu kwa masharti ya kutotajwa jina kwani habari hizo hazijatangazwa rasmi.
Raisi akizungumzia neno misaada!, watu mnakuja juu, akichukua hatua ili kujikwamua kwa kujitegemea, watu mnakuja juu, ningekuwa mimi Kikwete kwa hoja zenu hizi dhaifu ningewacheka halafu kimoyomoyo ningejisemea "these people dont know what they are talking about".
kaalika nchi chache, lakini nchi nyingine zenye uchumi mzuri kidogo kuliko sisi
zinawania kushiriki hamuoni kuwa hili ni jambo positive.
Acheni hoja za Chuki, na msifuate mkumbo, kuweni huru wa fikra siyo kila kitu mnalaumu tu, Hili la kikao ni muhimu sana, kwa sababu hizi nchi za jirani tunafanya nazo biashara kwa hiyo ni lazima mipango isukwe kuona tunajiokoa vipi kutoka katika hili tatizo la economic crisis iliyoikumba dunia.
DOWN WITH ARROGANTS, HATERS, WHINNERS, THUMBS UP FOR TRUTH SEEKERS AND POSITIVE CONTRIBUTORS