Katika kikao hicho wananchi na wateja wanaopatiwa huduma hiyo walipinga kuongezewa gharama za malipo ya maji, zikiwemo za kuingiza huduma hiyo majumbani mwao.Walisema tangu mradi huo uzinduliwe miaka miwili iliyopita hata gharama wanazotozwa katika akra zao ni kubwa, na hivyo kuiomba EWURA iwapunguzie kwa kuwa maji hayo hawayatumii kibiashara.