activisty
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 315
- 107
Nianze kwa kukuuliza ewe Mtanzania mwenzangu umeshasau? Hauna kumbukumbu au umelewa kifikra? Tegeta Escrow, Katiba Pendekezwa, Mauaji ya Albino, Utekwaji wa Katibu wa JKT, ongezeko la ajabu la Deni la Taifa, Raia kuuwawa na Polisi, Pesa zilizoko Uswizi, na kikubwa zaidi umasikini mkubwa wa Watanzania wengi. Sasa nauliza yote umeshayasahau? Haukumbuki hata kidogo?
Kila sehemu nikipita nasikia habari ya CHADEMA, CCM imepanda, CUF sijui imefanya nini ooh, habari ya Zitto Kabwe, na sisikii tena watu wakikemea Mauaji ya Albino, watu wakijiuliza kwa nini ajali zinaliandama taifa, huku tukishuhudia kila siku tukipoteza nguvu kazi ya taifa ambapo wengi ni vijana.T
umeshasahau Taifa linakabiliwa na janga kubwa la rushwa na ufisadi usio na mfano, deni la taifa ni kubwa kupita maelezo, mbele yetu kuna mchakato wa Kura ya Maoni ya Katiba Pendekezwa, lakina watanzania tumelewa siasa chafu za udaku, badala ya kuongelea masuala muhimu ya kitaifa, kwa kujiuliza tutaendelea kuwa masikini hadi lini, huku wanasiasa hawa hawa wanaofanya siasa udaku, wakitujaza fikra levi, huku wao wakisonga mbele kimaendeleo pamoja na familia zao na kutuacha mamilioni ya Watanzania masikini wakubwa.
Sasa najiuliza je ni kweli tumesahau au tumelala usingizi? Ewe Mtanzania mwenzangu ebu jiulize wewe na muulize jirani yako, juu ya kila jambo ulifanyalo au kulisema lina faida gani kwako na kwa taifa? Je, kweli CCM, CHADEM, CUF, NCCR, ACT ni muhimu kuliko taifa hili? Ni Muhimu kuliko familia yako ambayo inapata mlo mmoja kwa siku?
Je, kweli unashindwa kutenga muda wa kufanya masuala muhimu ya kimaendeleo, na kuziacha fikra zako zitawaliwe na siasa udaku?
Tuamke, tufanye mambo ya msingi kwa taifa hili na tuache kulewa siasa udaku za wanasiasa dhaifu.
Kila sehemu nikipita nasikia habari ya CHADEMA, CCM imepanda, CUF sijui imefanya nini ooh, habari ya Zitto Kabwe, na sisikii tena watu wakikemea Mauaji ya Albino, watu wakijiuliza kwa nini ajali zinaliandama taifa, huku tukishuhudia kila siku tukipoteza nguvu kazi ya taifa ambapo wengi ni vijana.T
umeshasahau Taifa linakabiliwa na janga kubwa la rushwa na ufisadi usio na mfano, deni la taifa ni kubwa kupita maelezo, mbele yetu kuna mchakato wa Kura ya Maoni ya Katiba Pendekezwa, lakina watanzania tumelewa siasa chafu za udaku, badala ya kuongelea masuala muhimu ya kitaifa, kwa kujiuliza tutaendelea kuwa masikini hadi lini, huku wanasiasa hawa hawa wanaofanya siasa udaku, wakitujaza fikra levi, huku wao wakisonga mbele kimaendeleo pamoja na familia zao na kutuacha mamilioni ya Watanzania masikini wakubwa.
Sasa najiuliza je ni kweli tumesahau au tumelala usingizi? Ewe Mtanzania mwenzangu ebu jiulize wewe na muulize jirani yako, juu ya kila jambo ulifanyalo au kulisema lina faida gani kwako na kwa taifa? Je, kweli CCM, CHADEM, CUF, NCCR, ACT ni muhimu kuliko taifa hili? Ni Muhimu kuliko familia yako ambayo inapata mlo mmoja kwa siku?
Je, kweli unashindwa kutenga muda wa kufanya masuala muhimu ya kimaendeleo, na kuziacha fikra zako zitawaliwe na siasa udaku?
Tuamke, tufanye mambo ya msingi kwa taifa hili na tuache kulewa siasa udaku za wanasiasa dhaifu.