Goliath mfalamagoha
JF-Expert Member
- Aug 3, 2012
- 601
- 2,508
Fumbeni macho yenu na usingizi uwapitie. mbongo zenu zitulie ili kesho mfikiria ujinga mwengine zaidi, enyi watanzania weusi, alama halisi ya mwafrika wa kughushi aliyeharibiwa akili na ukoloni, hata naye awe mkoloni kwa wenzake.
Ambao, mkipewa mbegu mtazipika na kuzila kwa uroho, halafu mkaombe tena. Kwakuwa matumbo yanataka zaidi huku mbongo zenu zinataka kidogo.
Usingizi uwapitie, ili angalau sasa, huko ambako jua linachomoza, viumbe wateule waendelee kujidhihirishia uteule wao.
Usingizi uwapitie; Enyi wenye maradhi, masikini na wajinga!
Na msidhani kama mtaamka mkiwa tofauti, Bado sana.
Mtabaki watumwa wa watu wa Ulaya Asia na Amerika. Hata watoto wenu na watoto wa watoto wao wataendelea kuwa vijakazi wa watu wengine, wateule.
Kwa kuwa nimeshindwa kujitaabisha kwa faida yenu wenyewe, mtataabika kwa faida ya wengine.
Usingizi uwapitie, ili dunia sasa ipumzike baada ya kuvumilia ujinga wenu mchana kutwa.
Kesho! Tunatarajia kusikia ujinga mwingine zaidi.
Ex Afrique Semper, Aliqui Novi
Ambao, mkipewa mbegu mtazipika na kuzila kwa uroho, halafu mkaombe tena. Kwakuwa matumbo yanataka zaidi huku mbongo zenu zinataka kidogo.
Usingizi uwapitie, ili angalau sasa, huko ambako jua linachomoza, viumbe wateule waendelee kujidhihirishia uteule wao.
Usingizi uwapitie; Enyi wenye maradhi, masikini na wajinga!
Na msidhani kama mtaamka mkiwa tofauti, Bado sana.
Mtabaki watumwa wa watu wa Ulaya Asia na Amerika. Hata watoto wenu na watoto wa watoto wao wataendelea kuwa vijakazi wa watu wengine, wateule.
Kwa kuwa nimeshindwa kujitaabisha kwa faida yenu wenyewe, mtataabika kwa faida ya wengine.
Usingizi uwapitie, ili dunia sasa ipumzike baada ya kuvumilia ujinga wenu mchana kutwa.
Kesho! Tunatarajia kusikia ujinga mwingine zaidi.
Ex Afrique Semper, Aliqui Novi