Eu yasifia uchaguzi Uganda

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,379
4,039
KIONGOZI wa ubalozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Uganda, balozi Atillio Pacifici, ameelezea kufurahishwa na jinsi uchaguzi mkuu nchini humo ulivyopangwa vizuri na kuandeshwa katika mazingira ya amani.

“Tuliona uchaguzi ambao ulipangwa vizuri na watu wakiwa watulivu wakisubiri kupiga kura zao na shughuli hiyo ikaendelea kwa amani. Tumefurahi. Maafisa wa Uchaguzi walioajiriwa na Tume ya Uchaguzi walifanyakazi yao kwa utaalamu mkubwa,” akasema balozi Pacific.

Kiongozi huyo wa ujumbe wa EU alitoa kauli hiyo Ijumaa alipokuw akizungumza na wanahabari katika uwanja wa Kololo Ceremonial Grounds. Ni hapo ambapo kulikuwa kituo cha tume ya uchaguzi ya Uganda cha kujumuisha matokea ya kura za ubunge kutoka kwa tarafa nne za Kampala.

“Inafurahisha kwamba vijana wengi, raia wa Uganda walielimika vizuri, ambao wanahudumu katika uchaguzi huu,” aliongeza wakati alipofanya ziara ya ghafla katika kituo hicho.

Mwaka huu EU haikutuma waangalizi wa uchaguzi, kama ilivyo kawaida yake. Hii ni kwa sababu serikali ya Uganda haijatekeleza mapendekezo yaliyotolewa na waangalizi wa EU katika chaguzi zilizopita.

Badala yake mwaka huu, EU ilituma kundi la wahudumu wa kidiplomasia kutoka afisi za kibalozi za mataifa kadha wanachama wa muungano, zilizoko Kampala.

Wajibu wa wanadiplomasia hao ulikuwa “kuona vila mambo yanavyoendelea katika uchaguzi huo.”

Tofauti na waangalizi wa uchaguzi ambao ni wataalamu, wanachama wa kundi hilo la wanadiplomasia hawatatoa ripoti rasmi na mapendekezo hasusi.

Miongoni mwa maeneo ambako kundi hilo la wanadiplomasia walizuru ni Mbale, Moroto, Arua, Lira na Rukungiri.

Isipokuwa visa vichache kwa makabiliano katika ya makundi hasimu ya wanasiasa na watu kadhaa kukamatwa wakiwemo waangalizi wa makundi ya kijamii, polisi na tume ya uchaguzi walisema kuwa uchaguzi huo wa Alhamisi uliendeshwa katika mazingira ya amani.

Wakati huo huo mnamo Jumamosi saa kumi kamili alasiri, tume ya uchaguzi ilimtangaza Rais Yoweri Kaguta Museveni mshindi kwa kupata jumla ya kura 5,851,037, sawa na asilimia 58.6 ya kura zilizopigwa.

Naye mpinzani wake wa karibu Robert Kyangulanyi, almaarufu Bobi Wine, alipata kura 3, 475, 298, sawa na asilimia 34.8 ya kura zilizopigwa.

Museveni aliyedhaminiwa na chama cha National Resistance Movement (NRM) amekuwa mamlaka kwa miaka 35, tangu 1986 alipoingia afisi kupitia mapinduzi ya kijeshi.

Hata hivyo, Bobi Wine alipinga matokeo hayo kwa misingi ya kile alichodai ni wizi wa kura na hatua ya serikali kutumia wanajeshi na polisi kunyanyasa wafuasi wake.
 
Credibility credibility it's all about ,who ?what's their reputation? credibility,trustworthiness?
 
Mamluki, Bob Amsterdam, anawaibia wateja wake! Hana impact yoyote, lakini ndiyo hivyo, wajinga ndio waliwao.
 
Back
Top Bottom