Eti turudi kijijini!

Tu ache kudanganyana kwa mfumo wetu wa siasa na uchumi wa sasa bush noma,kama umestaafu kazi ukaenda bushi pension ikiisha nawewe unakufa.
 
una uhakika kiongozi kuwa hajaanza shule na hatarajii!!huoni anajifunza mafunzo ya vitendo baada ya kutoka shule!!!
 
Mkuu hayo maisha walio wengi tumepitia, binafsi nilizaliwa mjini na nikaanza shule mjini pale uhuru mchanganyiko, chini ya kina mwalimu gumbo, mfaume , kingodi, njooka na wengineo kibao, lakini babu yangu akaja toka kijijini akalazimisha twende kusomea kijijini akisema mjini tutaharibikiwa hakika mara ya kwanza niliyoweka mzigo wa kuni kichwani nilimlaani yule babu vibaya mno, lakini baadae nikazoea maisha yakasonga na kwa kiasi fulani yamenifanya nimejifunza mambo mengi yanayoizunguka jamii hasa waishio vijijini, kama alivyosema mdau mmoja miundo mbinu ikiwekwa vizuri sio kubaya kama wengi wa mjini wanavyozani.
 
kweli kabisa sie wote asili yetu kjjn, ila waishio kijijini ni kama taifa lililofungiwa misaada na kuwekewa vikwazo na nchi zilizoendelea..
 

Kwa hiyo we ukijiapiza kuwa hutaenda huko, nani atapeleka mabadiliko?

Think positive brada!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…