Niliachana nae kwa kashfa tena matusi juu maana alinisaliti baada ya kutembea na muhasibu wa shirika moja akawa ananipiga vijembe ooh mie sasa hivi nipo na mtunza fedha wewe huna shughuli.
Nikaamua kumpotezea ingawa iliniuma sana maana mie maisha yangu yalikuwa ni kuchezea vibuti tu kila siku kipindi icho.
Maisha yameendelea akaanza kutuma sms za mitego mara oohh mwenzio nakukumbuka sana.
Nikawa namchunia ila baadaye nikaanza kuchat nae.Tumeendelea kuchat ananirazimisha tukatiane mie namkatalia coz siwezi kula matapishi yangu ila amekuwa akinihadithia mambo yake mengi na anaombaga nimsaidie.
Mara nyingi ananiomba hela mwezi wa pili nilimtumia laki 1, mwezi wa tatu nikamtumia laki 2 katika vipindi viwili mwezi wa tano huu ameniomba laki 2 tena. Sasa je mimi ni mtu wa aina gani?
Ni mdhaifu au ninampenda huyu mwanamke maana siku hizi akinipigia simu tunaongea masaa mengi tunakumbusha tukicheka na kufurahi i dont know myself na sitaki turudiane kimapenzi.
acaha uzoba sasa unampa hela za nni???
ujue bado unampenda hadi kuja kujaza server humu JF???
Nadhani ungekuwa mwanaume kamili ungempotezea na wala usingeleta huu ----- wako hapa
Sasa ikiwa wewe mwenyewe hujijui ni mtu wa aina gani JF watajua?Sikia kupenda sio upumbavu hata mie natamani,raha zake,tamu yake,penzi lake,tabu zake na tamaa yake weye ndio unae jua hapa sie tutasema wewe mjinga kwa mujibu wa maelezo yako,
usiikalifishe nafsi yako kama unampa basi inawezekana bado unampenda,au unampa kumuonyesha kua wewe sasa mambo safi,au unampa unakumbuka fadhila zake manake hakuna mbaya wa moja kwa moja atakua na mema yake japo MOJA,na kumbuka anaependa kikweli hachoki kuvumilia na habadilishi kauli hata ukimchukia,kila la kheir...